Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea

Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257

WhatsApp Image 2024-06-11 at 14.15.02_ef770101.jpg
Siku za hivi karibuni kumekuwepo na mgogoro wa ardhi baina wakazi wa Tungutungu Kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo pamoja na “kigogo”, nimefika mara kadhaa eneo hilo ni vilio vilio.

Mgogoro huo ulikuwa ukifukuta kimyakimya lakini kwa sasa umepamba moto kutokana na nyumba za wakazi wa eneo hilo kuwekewa alama ya X na kuelezwa kuwa kufikia Alhamisi wiki ijayo (Juni 13, 2024) nyumba zitakuwa zimebomolewa.

Nimefuatilia masuala kadhaa kwa ukaribu sakata hili baadhi ya Wananchi wanaeleza kwamba waliuziwa viwanja hivyo kwa utaratibu kupitia mamlaka za Kiserikali kwa kuwa viwanja hivyo vilikuwa ndani ya Manispaa.



WhatsApp Image 2024-06-11 at 14.18.49_f0838ca5.jpg

Wanadai kuwa MMM anayedai kuwa mmiliki halali wa eneo hilo ameshinda kesi na kuonekana mmiliki halali wa eneo hilo licha ya awali kutokuwa na nyaraka za mauziano.

Baadhi ya Wakazi wanadai kwamba walipeleka maombi ya kuweka zuio Mahakamani lakini ombi hilo limetupiliwa licha ya kesi hiyo kuendelea kuwepo Mahakama.

Wanasema kumekuwepo na mchakato wa maridhiano baina ya MMM (anayedaiwa kushinda kesi) na Wananchi, ambao ulianzishwa kwa lengo la kuleta suluhu nje ya utaratibu wa Kimahakama baada ya uwepo wa taharuki baada ya uamuzi.

Wananchi wanadai kwamba Mkuu wa Mkoa wa Pwani aliwaahidi kufanya mazungumzo na MMM kutafuta suluhu lakini wanadai matumaini yao yameisha baada dalali wa Mahakama pamoja na maafisa wa Jeshi la Polisi na kuweka nyumba zote zilizopo kwenye eneo hilo kuweka alama ya X tukio ambalo linaleta taharuki kubwa kwa Wakazi.

Sijapata nafasi ya kusikiliza upande wa MMM lakini ukisikiliza upande wa Wananchi unaona kuna uwalakini, Wananchi wanadai kuwa kuna mazingira ya kugushi nyaraka pamoja na Rushwa.
WhatsApp Image 2024-06-11 at 14.15.04_5a61491b.jpg
Ukisikiliza maelezo yao wanadai kuwa MMM anayesemwa kuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo, ni kama aliibuka tu maana wengi wanadai walianza kumiliki maeneo hayo Mwaka 2006, lakini MMM anadaiwa yeye anadai alianza kumiliki eneo hilo Mwaka 1995 jambo ambalo inadaiwa kuwa kipindi hicho eneo hilo lilikuwa likiendelezwa na raia mmoja wa Kihindi kabla ya kurejeshewa kwa Manispaa.

Kwa namna nilivyofuatilia suala hili nimuombe Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa pamoja na TAKUKURU wamulike suala hili kubaini mazingira halisi yaliyopo, maana imekuwa ikishuhudiwa manung'uniko mengi kwenye jambo kama hili.

Mwenyekiti wa Juma Hashim Kipita, Tungutungu amesema:
Huyo anayedai ni mmiliki alikuja na nyaraka akasema alinunua eneo hilo Mwaka 1995, jina la mtu anayemtaja alinunua kwake alikuwa babu yangu, moja ya majina anayotaja ni tofauti na uhalisia wa majina ya babu yangu.

Ninavyofahamu hapa kuna raia wa India alikuwa anamiliki baadaye akaondoka eneo likabaki wazi, wenyeji waliokuwepo wakaanz kuchukua maeneo na baadaye kuanza kuyauza.

Hivyo, huyu alipojuna na nyaraka za Mahakama, tunatakiwa kumuwekeza zuio lakini kwa kuwa hakuna nyaraka muhimu za umiliki inakuwa ngumu kuweka zuio, pia tunajiuliza tangu Mwaka 1995 kama anavyodai, alikuwa wapi siku zote?

Hata hiyo kesi anayosema ameshinda siyo dhidi ya watu waliopo hapa bali ni watu ambao walishi hapa miaka ya nyuma na kwa sasa hawapo.

Pia soma ~ Waziri wa Ardhi azuia mchakato wa kutaka kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga
 
Bagamoyo nayo ni manispaa? Tunapitwa na mengi!

Manispaa ina la kusema maana ndiyo serikali na kukionekana kuna taarifa za kughushi basi jinai inaendelea Au kuanzia hapo

Hili swala wenye majibu ni serikali (manispaa) na wizara iliyopitisha michoro ya upimaji ili manispaa waweze kuuza viwanja

Sasa MMM kama alighushi nyaraka ndipo hapo mchawi atapatikana na kama kuna sheria serikali ilitumia kujitwalia eneo watasema
 
Tunaomba waangalie maslahi ya wananchi zaidi ya 400. Hii ni hatari.



KAZI ni kipimo cha UTU
 
Huu mstari ulioandika umemaliza stori

"Ninavyofahamu hapa kuna raia wa India alikuwa anamiliki baadaye akaondoka eneo likabaki wazi, wenyeji waliokuwepo wakaanza kuchukua maeneo na baadaye kuanza kuyauza"

Narudia tena umeandika "wenyeji waliokuwepo wakaanza kuchukua maeneo na baadaye kuanza kuyauza"
 
Kama hujajenga Haya mambo yasikie tu kwa watu wanavunjiwa.

Hapo mtu anaanza upya Maisha eti. Mungu awape suluhu nyumba zisibimolewe.
 
Siku za hivi karibuni kumekuwepo na mgogoro wa ardhi baina wakazi wa Tungutungu Kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo pamoja na “kigogo”, nimefika mara kadhaa eneo hilo ni vilio vilio.

Mgogoro huo ulikuwa ukifukuta kimyakimya lakini kwa sasa umepamba moto kutokana na nyumba za wakazi wa eneo hilo kuwekewa alama ya X na kuelezwa kuwa kufikia Alhamisi wiki ijayo (Juni 13, 2024) nyumba zitakuwa zimebomolewa.

Nimefuatilia masuala kadhaa kwa ukaribu sakata hili baadhi ya Wananchi wanaeleza kwamba waliuziwa viwanja hivyo kwa utaratibu kupitia mamlaka za Kiserikali kwa kuwa viwanja hivyo vilikuwa ndani ya Manispaa.

Wanadai kuwa MMM anayedai kuwa mmiliki halali wa eneo hilo ameshinda kesi na kuonekana mmiliki halali wa eneo hilo licha ya awali kutokuwa na nyaraka za mauziano.

Baadhi ya Wakazi wanadai kwamba walipeleka maombi ya kuweka zuio Mahakamani lakini ombi hilo limetupiliwa licha ya kesi hiyo kuendelea kuwepo Mahakama.

Wanasema kumekuwepo na mchakato wa maridhiano baina ya MMM (anayedaiwa kushinda kesi) na Wananchi, ambao ulianzishwa kwa lengo la kuleta suluhu nje ya utaratibu wa Kimahakama baada ya uwepo wa taharuki baada ya uamuzi.

Wananchi wanadai kwamba Mkuu wa Mkoa wa Pwani aliwaahidi kufanya mazungumzo na MMM kutafuta suluhu lakini wanadai matumaini yao yameisha baada dalali wa Mahakama pamoja na maafisa wa Jeshi la Polisi na kuweka nyumba zote zilizopo kwenye eneo hilo kuweka alama ya X tukio ambalo linaleta taharuki kubwa kwa Wakazi.

Sijapata nafasi ya kusikiliza upande wa MMM lakini ukisikiliza upande wa Wananchi unaona kuna uwalakini, Wananchi wanadai kuwa kuna mazingira ya kugushi nyaraka pamoja na Rushwa.
Ukisikiliza maelezo yao wanadai kuwa MMM anayesemwa kuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo, ni kama aliibuka tu maana wengi wanadai walianza kumiliki maeneo hayo Mwaka 2006, lakini MMM anadaiwa yeye anadai alianza kumiliki eneo hilo Mwaka 1995 jambo ambalo inadaiwa kuwa kipindi hicho eneo hilo lilikuwa likiendelezwa na raia mmoja wa Kihindi kabla ya kurejeshewa kwa Manispaa.

Kwa namna nilivyofuatilia suala hili nimuombe Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa pamoja na TAKUKURU wamulike suala hili kubaini mazingira halisi yaliyopo, maana imekuwa ikishuhudiwa manung'uniko mengi kwenye jambo kama hili.

Mwenyekiti wa Juma Hashim Kipita, Tungutungu amesema:
Huyo anayedai ni mmiliki alikuja na nyaraka akasema alinunua eneo hilo Mwaka 1995, jina la mtu anayemtaja alinunua kwake alikuwa babu yangu, moja ya majina anayotaja ni tofauti na uhalisia wa majina ya babu yangu.

Ninavyofahamu hapa kuna raia wa India alikuwa anamiliki baadaye akaondoka eneo likabaki wazi, wenyeji waliokuwepo wakaanz kuchukua maeneo na baadaye kuanza kuyauza.

Hivyo, huyu alipojuna na nyaraka za Mahakama, tunatakiwa kumuwekeza zuio lakini kwa kuwa hakuna nyaraka muhimu za umiliki inakuwa ngumu kuweka zuio, pia tunajiuliza tangu Mwaka 1995 kama anavyodai, alikuwa wapi siku zote?

Hata hiyo kesi anayosema ameshinda siyo dhidi ya watu waliopo hapa bali ni watu ambao walishi hapa miaka ya nyuma na kwa sasa hawapo.
Viwanja vya Bagamoyo vina uhuni mwingi sana
 
Back
Top Bottom