Mwanachama na aliyekuwa Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA, Odero Charles Odero amesema ile kura moja aliyoipata katika uchaguzi huo ni ya mpiga kura sio yake. Kwa maana hiyo hata yeye mwenyewe alishindwa kujipigia kura
Odero alitangaza kusudio lake la kuomba kuteuliwa kugombea Uenyekiti wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania na kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Freeman Mbowe na Tundu Lissu aliyeshinda.