Pre GE2025 Odero amesema ile kura moja aliyoipata ni ya mpiga kura, hata yeye hakujipigia Kura Uchaguzi CHADEMA

Pre GE2025 Odero amesema ile kura moja aliyoipata ni ya mpiga kura, hata yeye hakujipigia Kura Uchaguzi CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Mwanachama na aliyekuwa Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA, Odero Charles Odero amesema ile kura moja aliyoipata katika uchaguzi huo ni ya mpiga kura sio yake. Kwa maana hiyo hata yeye mwenyewe alishindwa kujipigia kura

Soma, Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA 2025: Tundu Lissu ashinda nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa kwa Kura 513 sawa na 51.5%

Odero alitangaza kusudio lake la kuomba kuteuliwa kugombea Uenyekiti wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania na kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Freeman Mbowe na Tundu Lissu aliyeshinda.

 
😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣😂😂🤣🤣Sasa Angeshinda Vp Wakati Hata Yeye Mwenyewe Hakujipigia
 
Kura ya Professor mmoja Nia Sawa na kura ya kuli mmoja
Kura ya mwanasheria mmoja Nia Sawa na Kura ka dalali mmoja

Kimsingi, Kura moja ni moja bila kujali ni ya nani, mtu mmoja Ana Kura moja. Ni muhimu kuwafikia watu wote.
 
Hy n tofauti kwa wanasiasa wa ccm, popote ntakapopiga kura ila wao ndo wataunda serikali.

Source: mama mwenyewe.
 
Back
Top Bottom