Ogopa Mkopo wa simu Airtel ikishirikiana na Watu Credit, wamsababishia baba shida

Ogopa Mkopo wa simu Airtel ikishirikiana na Watu Credit, wamsababishia baba shida

A Father

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2012
Posts
1,219
Reaction score
380
Wakati Baba anahudumiwa, aliambiwa atarejesha Tsh. 13, 600/= kwa wiki.

Lakini Baba ametumiwa mkataba kwa njia ya mtandao, alipoufungua amekuta amesainiwa fomu yenye makato ya Tsh.14,300/= kwa wiki, tofauti na aliyofahamishwa, na mkataba haubadilishiki. Imekula kwa Baba.
 
Wakati Baba anahudumiwa, aliambiwa atarejesha Tsh. 13, 600/= kwa wiki.

Lakini Baba ametumiwa mkataba kwa njia ya mtandao, alipoufungua amekuta amesainiwa fomu yenye makato ya Tsh.14,300/= kwa wiki, tofauti na aliyofahamishwa, na mkataba haubadilishiki. Imekula kwa Baba.
Tafadhali na mimi nataka kukopa huko,utaratibu upoje??na unakopa Pesa au Chombo sijui Pikipiki au Bajaj??
 
Kuna wale jamaa wa ABSA walionunua Barclay Bank! Baclays ilikopesha watu kwa dhamana ya mshahara na wengi walipoteza ajira kwasababu tofautitofauti! Sasa hawa ABSA vielehele heti wanatafuta madeni ya Barclays! Inamaana wakati wananunua Barclays hawakuyaona hayo madeni?
 
Mwaka 2020 mwishoni nilikopa Pesa CRDB ml.36 ambapo dhamana ilikuwa Mshahara wangu ofisini(ilikuwa nilipe kwa miaka 5).Baada ya miezi 11 tangu nikope nikiwa nakatwa rejesho kutoka kwenye Mshahara wangu,Kampuni ikanipunguza kazi mimi pamoja na wenzangu kama 200. CRDB wakaanza kunipigia kuuliza rejesho nikawa nawatukana mpaka wakakoma,wakatafuta Kampuni ya kukusanya madeni,nao wamenipigia kama mara tatu nawaporomoshea matusi naona wameona maji marefu wameacha kunipigia sitakagi ujinga. Maana niliwauliza wakati nakopa niliweka nyumba yangu au kiwanja au gari langu kama dhamana jibu wakaniambia HAPANA,wakasema dhamana yako ilikuwa Mshahara wako,nikawajibu sasa kama dhamana yangu ilikuwa Mshahara wafuateni ofisini waulizeni kwa nini walinidhamini nikope halafu baada ya miezi 9 wakanipunguza kazini,wanategemea nilipe deni kwa matako??mpaka leo wapo kimya, Kadi ya Bank ya CRDB nikishaichoma na moto

😂😂😂

Unaishi Tandale ipi? maana si kwa vitenzi vikurupushi ulivyotumia...
 
Wakati Baba anahudumiwa, aliambiwa atarejesha Tsh. 13, 600/= kwa wiki.

Lakini Baba ametumiwa mkataba kwa njia ya mtandao, alipoufungua amekuta amesainiwa fomu yenye makato ya Tsh.14,300/= kwa wiki, tofauti na aliyofahamishwa, na mkataba haubadilishiki. Imekula kwa Baba.

Dunia ya leo unakopaje simu mkuu tena kampuni ya simu...

Ni bora udundulize pesa utanunua simu kwa bei chee tu...
 
Uko sahihi bro. Shida ndio zinafanya watu wanaingia kwenye mikopo hii. Mimi nilikopa kupitia vodacom. Nikaambiwa nilipe kianzip shs 100,000 halafu nilipe 12,300 kwa wikii. Sasa 12,300x52 ni shs 639,600. Ukijumlisha na ile 100,000. Ina maana simu nitalipa 739,600.
Simu hiyo hiyo, hapo hapo inauzwa 430,000 na ndio risiti niliyoandikiwa. Ongezeko la 309,600.
Kutokana na shida maana sikuwa na hela yote nalipa.
 
Back
Top Bottom