Tonydigital
Senior Member
- Oct 6, 2014
- 186
- 245
Habari za muda huu wadau?
Siku ya leo ya mapumziko (Muungano) nimeamua kupitia na kusikiliza baadhi ya nyimbo za nguli wa muziki Oliver N’Goma ( sasa marehemu) moja ya nyimbo zake nazozipenda ni hii “Bane” iliyoachiwa rasmi mwaka 1990 na inapatikana kwenye album yake ya kwanza yenye jina hilo hilo.
Nimevutiwa zaidi na contents za wimbo huu.
Nyimbo: Bane
Maana: Watoto (children)
Album: Bane
Kutolewa: 1990
Mwandishi: Oliver N’Goma
Mwandaaji: Manu Lima
-Katika kibao hiki Oliver anakiasa kizazi kipya (watoto) kuhusu umuhimu wa elimu katika maisha yao. Anasisitiza kuwa maisha yamebadilika sana hivyo wawe makini, imara na kusikiliza ujumbe wake. Wajiandae wawe watu wenye msaada kwa jamii baadae kwa kujikomboa kupitia elimu, mali za wazazi sio zao na zinaweza kuwaingiza kwenye matatizo endapo ndugu wenye nia mbaya waingiliapo.
Hivyo wajishugulishe kutafuta vitu na mali zao binafsi na sio kutegemea urithi / wazazi. Oliver N’Goma anaitaja shule “Icole” katika dakika ya (3:57) kama moja ya nyenzo ya kubadilisha maisha na kuwa watu bora katika jamii, hivyo watoto (kizazi kipya) wafanye bidii katika elimu kwani ndo ukombozi halisi.MWISHO.
Mzee wetu Lowassa pia aliwahi kusisitiza “Elimu Elimu Elimu”😀
Siku ya leo ya mapumziko (Muungano) nimeamua kupitia na kusikiliza baadhi ya nyimbo za nguli wa muziki Oliver N’Goma ( sasa marehemu) moja ya nyimbo zake nazozipenda ni hii “Bane” iliyoachiwa rasmi mwaka 1990 na inapatikana kwenye album yake ya kwanza yenye jina hilo hilo.
Nimevutiwa zaidi na contents za wimbo huu.
Nyimbo: Bane
Maana: Watoto (children)
Album: Bane
Kutolewa: 1990
Mwandishi: Oliver N’Goma
Mwandaaji: Manu Lima
-Katika kibao hiki Oliver anakiasa kizazi kipya (watoto) kuhusu umuhimu wa elimu katika maisha yao. Anasisitiza kuwa maisha yamebadilika sana hivyo wawe makini, imara na kusikiliza ujumbe wake. Wajiandae wawe watu wenye msaada kwa jamii baadae kwa kujikomboa kupitia elimu, mali za wazazi sio zao na zinaweza kuwaingiza kwenye matatizo endapo ndugu wenye nia mbaya waingiliapo.
Hivyo wajishugulishe kutafuta vitu na mali zao binafsi na sio kutegemea urithi / wazazi. Oliver N’Goma anaitaja shule “Icole” katika dakika ya (3:57) kama moja ya nyenzo ya kubadilisha maisha na kuwa watu bora katika jamii, hivyo watoto (kizazi kipya) wafanye bidii katika elimu kwani ndo ukombozi halisi.MWISHO.
Mzee wetu Lowassa pia aliwahi kusisitiza “Elimu Elimu Elimu”😀