Oliver N’Goma: Muziki Burudani na Elimu (Ujumbe)

Mkuu isidingo55 Baada ya Uzi wako huu wa nguli wa ZOUK Africa, nimefurahi sana ulivyomtaja producer Manu Lima, kwa sababu nilikua natamani kwa muda mrefu kujua nani alikua mitamboni kupika instrumentals kali sana za zouk ambazo mkali Oliver Ngoma alikua akijinafasi. Leo nimepata muda wa kumfuatilia Manu Lima kwa kina, aisee huyu Manu Lima alikua ana balaa sana, ni jamaa mzaliwa wa senegal ila mwenye asili ya cape verde, ni mtaalam haswa katika maswala ya production kwenye miondoko ya Zouk, cabo-zouk, funana, cabo love, cola-dance, afrozouk and kizomba music. Pia jamaa ni mtunzi, mtafsiri, na mwanamuziki. Ni mbobezi mkubwa katika ZOUK. Ndio maana midundo aliyokua akimsukia Oliver Ngoma na wasanii wengine Africa kama Madilu System ule wimbo Ya Jean n.k ilikua mikali mnoo.


Manu Lima
 
Ndio mkuu binafsi kwangu ndo producer bora wa miondoko ya zouk!!alimjulia sana Oliver
 
kumbe mpaka ile ya jean alisuka huyu mwamba
Inaonekana alikuwa mtaalam wa kinanda sana
 
Ingia youtube andika Manu Lima, zitakuja baadhi ya nyimbo alizoimba pia na live show akipiga vyombo piano n.k, kuna wimbo utauona Manu Lima Falal nha amigo kizomba bonge ya wimbo humo manu lima kaimba mnoooo. Alafu bonge moja la beat kalitengeneza, nikawaza kama hilo beat angepita nalo Oliver Ngoma ingekua balaaa. Nimeweka picha ya screenshot ya huo wimbo.

 
Thanks kuna nyingne anaimba ndani ya gari...jina limenitoka 😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…