Ombi kwa Utumishi: Mwenzi huu tunaingia mwezi mtukufu wa mfungo

Ombi kwa Utumishi: Mwenzi huu tunaingia mwezi mtukufu wa mfungo

Hili ni ombi kwa wanao husika tarehe mosi mwenzi wa tatu mwezi mtukufu wa ramadhani unaweza kuanza rasmi.

1. Mishahara ya watumishi itoke mapema ili waweze kupangilia bajeti ya mwezi mzima kununua bidhaa ya mwezi mtukufu mapema.

2. Kuongeza bei ya vitu muhimu ni Dhambi kwahiyo acheni tabia ya kupaishwa bei ya viazi miongo sukali tende nk.

3. Waajiliwa peeni watumishi wenu muda wa kufanya ibaada nakutoka kazini mapema kwa kuzingatia utukufu wa mwezi huu.

4. Nyie msiofunga acheni kula chakula hadharani tuvumiliane kipindi hiki sie sote ni jamii moja kwa imani tofauti.

Ahsanteni.
Serikali ya tanzania haina dini hivyo kuruhusiwa kutoka kazini mapema ni kuvunja kanuni za kazi
 
Kiukweli Kuna mda mnafanya waislam waonekane sio watu wa maana
Inawezekana hata mwenyezi Mungu anatushangaa namna tulivo wapumbavu
Tujifunze kuheshimiana na wengine amri kuu Kwa Mungu ni upendo hata mtume Muhammad saw hakuwa hivi tulivo waislam wa sasa
 
Kiukweli Kuna mda mnafanya waislam waonekane sio watu wa maana
Inawezekana hata mwenyezi Mungu anatushangaa namna tulivo wapumbavu
Tujifunze kuheshimiana na wengine amri kuu Kwa Mungu ni upendo hata mtume Muhammad saw hakuwa hivi tulivo waislam wa sasa
Mkuu la ajabu ni lipi hapo?
 
Kwenu jirani yako akiwa na sherehe au msiba hutowi ushirkiano kwasbb sherehe inamhusu yeye tu?
Uliwahi kushirikiana na wakristu kwenye funga yao?
Au walishawahi kukuomba ushirikiano wowote?
 
Hili ni ombi kwa wanao husika tarehe mosi mwenzi wa tatu mwezi mtukufu wa ramadhani unaweza kuanza rasmi.

1. Mishahara ya watumishi itoke mapema ili waweze kupangilia bajeti ya mwezi mzima kununua bidhaa ya mwezi mtukufu mapema.

2. Kuongeza bei ya vitu muhimu ni Dhambi kwahiyo acheni tabia ya kupaishwa bei ya viazi miongo sukali tende nk.

3. Waajiliwa peeni watumishi wenu muda wa kufanya ibaada nakutoka kazini mapema kwa kuzingatia utukufu wa mwezi huu.

4. Nyie msiofunga acheni kula chakula hadharani tuvumiliane kipindi hiki sie sote ni jamii moja kwa imani tofauti.

Ahsanteni.
Usilazimishe watu wasioamini dini yako kuifuata.

Huo ni ujinga.
 
Uliwahi kushirikiana na wakristu kwenye funga yao?
Au walishawahi kukuomba ushirikiano wowote?
Mkuu sio kushirikiana tuna saidiana kwa kila kitu mpaka kwenye sherehe za ubatizo wao, sio ni wastaarabu sanaa.
 
Linabadilika kua zito kwasababu mada ilikua "ombi" sio agizo.
Ombi lina vipengele vyenye ujinga wa kufikiri kwamba watu wasioiamini dini fulani wanapaswa kuifuatilia na kutekeleza imani zake.

Mimi nisiyeamini Uislamu nikiwa nakula mchana wazi wakati wa Ramadhani hilo linakuzuiaje wewe Muislamu kufunga?

Hapo mnaoweka hizi habari za watu wasile wazi mchana mwezi wa Ramadahni kama hamtaki kutu control na kutupangia maisha mnataka nini?

Sitaki ujinga.
 
Back
Top Bottom