On Ndulu: The "Guardian" must be kidding me!


Si jukumu la serikali kuwajengea raia wake makazi bora. Jukumu la serikali ni kuweka mazingira ambayo yatawawezesha raia wake kupata( Kujenga au kupanga) makazi bora. Dhana ya kuwapatia wafanyakazi au raia wake makazi ndiyo iliyotufikisha hapa.

Amandla.......
 
.
jmushi, asante sana kwa maoni yako, ninaposema sifagilii lavish spending, ninamaanisha kuna matumizi ya mabilioni na mabiliona yanakuwa spent na serikali yetu for nothing, or not accounted for. Hii ndio naita lavish spending.

Nimesema we deserve the best money can buy not the luxury. Mimi ni mtu wa Nyerere time, ile miezi 18 ya kujifunga mikanda ndio nilikuwa primary na foleni nimepanga mpaka zile za kupanga mawe nimeshiriki kupata kilo ya unga wa yanga!. Uniform tumevaa 'madurufu'. Kipindi hicho Nyerere alituaminisha personal car ni laxury, tv ni luxury etc. Nyerere ndie alitembelea benzi, mawaziri peogeot 504. Hivyo hata gari la kutembelea na tv kwa wakati huo ilikuwa lavish spending.

Leo gari tv, dish ni ordinary emenities sio laxury tena. Hivyo hiyo nyumba ya gavana, japo kwa sasa itaonekana lavish na laxury, imejengwa idumu miaka 100. Ile swimming pool ambayo leo inaonekana ni laxury, kwa wengine ni exericise ground for tension releave na relaxation, labda Balali angekuwa na swimming pool home na gym, asingekufa mapema vile, angekuwako on the dock na kutegua vitendawili kibao kikiwepo cha Kagoda.

Kwa vile hatuna detailed value for money ya hiyo nyumba na ina nini, then to me spending 1.4 billion kwa nyumba ya hadhi ya gavana itakayoishi for 100 years is not a big deal despite all our povert stinking nation kama hiyo ni fedha ya kununua only a single mobile phone ya Goldvish "Le million".

Rev. Kishoka amekuwa objective kuhoji hivi hiyo nyumba ina nini?. ukishajua what it takes to swallow hiyo bilioni, then tunajustify lawama. J.Mushi huwezi amini, taasisi kama TACAIDS inatumia mara kumi ya kiwango kama hicho kwenye warsha, semina na makongamano kuhusu Ukimwi, huku waathirika wakiuliwa na retroviral kufuatia mlo mmoja kwa siku!.

Bilioni 1.4 is a lot of money in a small picture, but in a bigger picture, its nothing!. We are spending like hell for nothing, tunahaki ya kupiga kelele, ila pia sometime kelele zinazidi hata kama we are spending for something.
 
Usimuonee yeye ameandika kama alivyoona na sio mtaalam. Ameona granite tiles zimetumika, akaambiwa madirisha ni bullet proof na vikolombwezo kibao alipouliza wakamwambia hiyo ndio Japanese technology etc etc. Ujumbe umefika.
 

Tatizo sio nyumba kugharimu kiasi hicho. Tatizo ni kutumia pesa za umma kujenga nyumba ya gharama hiyo. Kama ingekuwa kajijengea binafsi wengi tusingemchachamalia. kama Yona ana uwezo wa kujijengea nyumba ya mabilioni, hilo si shauri letu ili mradi akituhakikishia kuwa pesa zilizotumika hazikutoka serikalini. Pasco kuwa na simu ya $milioni moja haituhusu. Ni pale Pasco atakaponunuliwa na shirika la serikali simu ya $milioni ndipo panapotokea tatizo. Upuuzi fanyia pesa yako mwenyewe lakini si ya umma! Hakuna justification kwenye hilo.

Amandla........
 

Kuweka mazingira na kujenga kuna tofauti gani? Au unaongelea mazingira ya rushwa?
 
Usimuonee yeye ameandika kama alivyoona na sio mtaalam. Ameona granite tiles zimetumika, akaambiwa madirisha ni bullet proof na vikolombwezo kibao alipouliza wakamwambia hiyo ndio Japanese technology etc etc. Ujumbe umefika.

Hapana, simuonei. Hii inaweza kuwa walikuwa wanajaribu kuona kama wataweza kutumia upuuzi huo ku-justify matumizi yao ya ovyo! Si unaona wanavyotapa tapa kwenye haka kajumba? Watu hawana aibu hawa.

Amandla......
 



Very true, tatizo hapa naona jazba ndio zinatawala. Nyumba ni kweli inaweza kugharimu bilioni 1.4 kutegemea na material yalitumika, security systems nk.

Ningekuwa mimi ningeuliza mchanganuo wa gharama kwanza kabla sijaita watu wajinga( MMK anasema Guardian are stupid).

Pia umefafanua vizuri kuwa ni nyumba ya Gavana wa benki kuu sio ya Beno Ndulu.

MMK sometimes naona kama sifa zimezidi na kudhani wate ambao hawafikiri kama yeye ni wajinga. NA mara nyinyine anapinga kila kitu.

Hasa siku hizi unaonyesha kama umeshuka kidog.. u complain on everything , ooh sijui Haiti hutujasaidia yani sijui vipi .. unaboa at times ile mbaya.
 
Kuweka mazingira na kujenga kuna tofauti gani? Au unaongelea mazingira ya rushwa?

Mazingira ni pamoja na kumwezesha mwananchi kupata mahali pa kujengea, kuweza kupata pesa ( kipato kizuri au uwezo wa kukopa) au malighafi ya kujenga kama anataka. Ni mwananchi ndiye anayejenga sio serikali. Unaposema jukumu la serikali ni kujenga ina maana serikali inajenga na kumkabidhi nyumba mwananchi! Na kuwa na makazi mazuri si lazima yawe yako. Panatakiwa pawe na makazi mazuri yanayoweza kupangwa kwa bei inayomudika.

Si kila kitu ni rushwa.

Amandla........
 

Asante Fundi Mchundo,
Nilitembezwa katika hili hili la kutaka kujua, masikini mimi, sina hili wala lile, nilidanganywa kama walivyodanganywa wenye jengo, limejengwa kama oval office, eti safe and secure.

Tena ili kuwalinda watumishi wa BOT eti nao wanakinga ya kutoshitakiwa popote kutokana na utekelezaji wa maukumu yao, kama ile ya rais!.

Nakubaliana na wewe, kama ni mtu hujua titanium ni nini, utakubali unachoambiwa. Tena electical ya jengo line ni supper conductors!. Inawezekana wameyasema yote hayo ili kuhalalisha ulaji tuu, justification inapatikana kwenu wenye uzoefu wa nini haswa kimefanyika, kimegharimu nini na tunaambiwa nini sie tusiojua.
Thanks.
 


Kabla ya kutoa shutuma na kuleta Jazba kama ulivyosema, thamani ya nyumba iliyojengwa haizidi 500 million kuna jamaa walileta data kwenye thread ya ile nyumba.

Vile vile kuna consultants ambao wametoa vidokezo na ushahidi kusema haiwezekani pesa nyingi kiasi kile kwa kale kajumba. Sasa wewe kama una Bill of quantity ya hiyo nyumba iweke hapa ili tuweze kuchambua mchele na pumba.
 
We say the said expenditure was a pretext because available evidence indicates that, based on the annual rent of 113 million/- BoT had been paying for the governor’s accommodation in rented premises

Hiyo nyumba walipanga kutoka kwa nani? Na ilikuwa wapi? Na ikoje?

Amandla........
 


Nikupe mfano wa UK. Serikali ina jukumu la kuwapatia makazi raia wake. Kama hawana nyumba inawapatia mahali pa kuishi na kuna system ya kuweza kuona uwezo wa kila raia wake. Ukiweza kulipa kodi kwa miaka kadhaa wanakuuzia kwa bei poa nk. Na hii ni kwa sababu ya kukusanya kodi na kuweka vitu muhimu kama makazi nk.

Unachosema wewe ni kwamba wale waliopata ndio basi wengine walie tu. Yaani waliowahi kuingia NHC warithishane hadi kiama. Je kulikuwa na muongozo gani hadi hawa wakodishwe na wengine wasiweze kukodishwa kwenye nyumba za NHC?

Je katiba ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema nini kuhusu hili?

Ukipitia yote hayo utarudi hapa na kuniambia jukumu ni la serikali na hapo ndipo utakata mzizi wa Wizi ambao umekubuhu na hauna tija kwa taifa. Pesa ambazo serikali inakusanya kwenye kodi nk ni tosha kabisa kufanya mambo makubwa ambayo wengine wanaona ni miujiza.
 
It’s such a shame, it’s such a shame, (Ndulu)
Don’t walk away, don’t walk away(Ndulu)

yana mwisho haya.
 

This is what is referred as "the crux of the matter". Watu wanafikiria tunagombana kuwa Gavana anaishi kwenye nyumba iliyogharimu bilioni 1.4.. kama ingekuwa ni ya kwake na kutokana na mapato yake halali hakuna ambaye angehoji.. sisi ni mabepari bwana! Kwani kuna mtu kalalamikia nyumba anayoishi Rostam au Mengi?
 
Mzee Mwanakijiji

Usiue inzi kwa nyundo. khe khe khe khe
 
Hivi hadhi ya Ndullu ni kubwa kuliko Wakazi wa Kagera ambao hawana reliable airport? au Lindi Au Tabora au Sumbawanga etc etc? na kati ya Nyumba ya Ndullu na maendeleo mengine mfano kuwa na Scanner Hospitali ya Bombo etc lipi linalo faa ?
 
Hiyo nyumba si itatumiwa na Ndulu, na Gavana wa BOT atakayefuata baada ya Ndulu?
 

I choose my words very careful; and I mean them!

kusema kuwa "nyumba ni ya Gavana na siyo ya Ndulu" ni kuchezea maneno!
 
Hiyo nyumba si itatumiwa na Ndulu, na Gavana wa BOT atakayefuata baada ya Ndulu?

Hivi unakumbuka Nyumba ya NHC aliyokuwa anakaa BWM ilikarabatiwa kiroho mbaya wakati yeye ni rais na baadaye aliuziwa kwa bei ya peremende.

Ndulu naye atapewa mkono wakati anastaafu kwa bei ile ile ya pipi. Hiyo ndio Tanzania ya leo, ile katiba inasema makazi bora kwa .... .... lakini Serikali ya Chama Cha Majambazi inaigeuza kama kinyonga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…