Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki ulioshamiri mijini

Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki ulioshamiri mijini

Zamani kwenye hii kazi ya Bodaboda risk kubwa ilikuwa ni muda wa usiku but siku hizi wezi nao wameendelea sana, kuna dogo moja akikuwa na pikipiki mpya akaja mtu aliyevaa kimasai ampeleke sehemu yenye umbali kidogo kama km 35, walipofika eneo lenye pori abiria aliomba kujisaidia aliposhuka tu alitoa sime na dogo akakabidhi Boda kiulaini.
 
Kuna jamaa wawili kutoka Dar walienda kuiba piki piki huko Bagamoyo na wakafanikiwa....kufika njiani Piki piki ikazima wakahisi ni mafuta...wakaingia chaka kidogo mmoja akaenda kutafuta mafuta...kumbe ile piki piki imefungwa kifaa cha Kui track popote iendapo na mwenyewe huweza kuizima muda wowote.

Basi baada ya muda yule mwizi akashangaa kundi la bodaboda likienda direct alipojificha....walichukua piki piki wakamuua kwani alikua amejificha juu ya mti...aliyeenda kununua mafuta alinusurika.

Fundisho:Kuna kampuni zinafunga vifaa hivi,kwa Piki piki haizidi 200k na chombo kinakua salama....kama unampa bodaboda Mkataba unaijumlisha kwenye mkataba kwani ukilipa umelipa...tujifunze kujiweka salama jamani...Sijazitaja kampuni makusudi ila zinajulikana sana tu.
Ni wazo zuri ila wezi nao huwa kidigitali wanaweza kuharibu hiyo security system kama wamegundua ipo ili lengo lao litimie.

Wahuni sio watu.
 
Kuna jamaa mmoja alienda sehemu kwenye kijiwe cha bodaboda akachukua bodaboda siku ya kwanza akaenda site jamaa akashuka akaenda ongea na wale mafundi then akarudi kwa bodaboda akarudi kituoni jamaa akapanda daladala akaondoka

Siku ya pili the same way

Siku ya tatu the same way

Siku ya nne jamaa alivyoshuka kwenye daladala alikuwa amebeba ndoo ya rangi mpyaaa

bodaboda akamkimbilia akamwambia kama kawaida jamaa akasema naaam jamaa akaenda site mshkaji akamwambia tushuke uone nyumba wakawa wanaelekea kwenye nyumba

Ile wanakaribia kufika kwenye nyumba this time jamaa kununua na rangi yaani ile wanakaribia jamaa akamwambia unajua nimesahau misumari hebu nishikie hii ndoo ya rangi nikakimbilie misumari pale road

Bodaboda likawa limebeba ndoo ya rangi akimsubiri jamaa dakika 5, 10, 20, 30 ikabidi awaulize mafundi kama ana namba ya mshkaji ili ampigie amuulize shida nini mbona kachelewa

Kuuliza washkaji wanamwambia Yule sio mwenye nyumba huwa anakuja pale kutafuta kibarua siku ya kwanza hakukutana na fundi mkuu siku ya pili hakukutana na fundi mkuu siku ya tatu hakukutana pia na fundi mkuu na wao walishangaa kumuona anakuja na rangi wakajua maybe wameshaonana na fundi mkuu

Yaani mwamba alikuwa anamdanganya bodaboda naenda site yangu nyumba yangu najenga, mwamba akifika kwa mafundi anafika kuulizia nafasi ya kibarua bodaboda anakaa mbali anajua mwenye nyumba anafanya ukaguzi wa nyumba yake

Jamaa bodaboda alivyoambiwa vile ushuzi ulimtoka bila yeye kujua
 
Ni wazo zuri ila wezi nao huwa kidigitali wanaweza kuharibu hiyo security system kama wamegundua ipo ili lengo lao litimie.

Wahuni sio watu.
Inapofungwa hats mwenye Piki piki hujui...unawakabidhi chombo inakuja imeshafungwa na haionekani...inapunguza risk kwa kiasi kikubwa sana.
 
Kuna jamaa mmoja alienda sehemu kwenye kijiwe cha bodaboda akachukua bodaboda siku ya kwanza akaenda site jamaa akashuka akaenda ongea na wale mafundi then akarudi kwa bodaboda akarudi kituoni jamaa akapanda daladala akaondoka

Siku ya pili the same way

Siku ya tatu the same way

Siku ya nne jamaa alivyoshuka kwenye daladala alikuwa amebeba ndoo ya rangi mpyaaa

bodaboda akamkimbilia akamwambia kama kawaida jamaa akasema naaam jamaa akaenda site mshkaji akamwambia tushuke uone nyumba wakawa wanaelekea kwenye nyumba

Ile wanakaribia kufika kwenye nyumba this time jamaa kununua na rangi yaani ile wanakaribia jamaa akamwambia unajua nimesahau misumari hebu nishikie hii ndoo ya rangi nikakimbilie misumari pale road

Bodaboda likawa limebeba ndoo ya rangi akimsubiri jamaa dakika 5, 10, 20, 30 ikabidi awaulize mafundi kama ana namba ya mshkaji ili ampigie amuulize shida nini mbona kachelewa

Kuuliza washkaji wanamwambia Yule sio mwenye nyumba huwa anakuja pale kutafuta kibarua siku ya kwanza hakukutana na fundi mkuu siku ya pili hakukutana na fundi mkuu siku ya tatu hakukutana pia na fundi mkuu na wao walishangaa kumuona anakuja na rangi wakajua maybe wameshaonana na fundi mkuu

Yaani mwamba alikuwa anamdanganya bodaboda naenda site yangu nyumba yangu najenga, mwamba akifika kwa mafundi anafika kuulizia nafasi ya kibarua bodaboda anakaa mbali anajua mwenye nyumba anafanya ukaguzi wa nyumba yake

Jamaa bodaboda alivyoambiwa vile ushuzi ulimtoka bila yeye kujua
Aisee hatari sana
 
Hapa Nchini kumekuwepo na wimbi kubwa la wizi wa pikipiki hasa pikipiki aina ya Boxer.

Tena baada ya uzuka kwa ugonjwa wa Kirona, ndo hali imekuwa mbaya. Watu (bodaboda) wengi wamekuwa wakilizwa mara kwa mara.

Kwa nini pikipiki aina za boxer ndo zimekuwa zikishambuliwa sana kuibiwa? Wengi wanasema kinachotafutwa pale ni injini yake tu. Inasemekana inatumika sana kama mita ya kuvutia na kumwagilizia maji kwenye visima au kilimo cha umwagiliaji. Ila kama ni kuuza kwa ajiri ya spea, wezi hao huziuza kwa bei ya kutupwa sana.

Siku hizi ukiwa na pikipiki mpyunaifanyia kazi basi inabidi uwe mwangalifu sana tena sana. Hasa uwe selective wa abiria wako.

Baada ya utangulizi huo sasa niende kwa maada husika :" Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki uloshamiri mijini" na hizo mbinu za wizi ni

1) Mhogo feki kwenye mguu.

Hapa inakuwa hivi. Jamaa anachukua mabox ama vitambaa na kujiviringishia pamba juu kwenye unyayo na vidole hadi usawa wa goti mithili ya mtu aliyevunjika mguu na kuwekewa mhogo.

Kisha anachukua gongo na kuzuga nalo mara nyingi wanategeshea maeneo ya hospitali. Anajifanya kama vile ameruhusiwa (discharge) kwenda nyumbani. Anaweza akawa na kijibegi mkononi au mgongoni.

Basi ana chunguza bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwita ampeleke mahali hasa hasa nyumbani. Basi kwa shida sana atapanda piki piki kisha anaondoka.

Trick ya wizi
Mkiwa njiani, tadondosha kwa makusudi lile ngongo kisha kukuomba msimame. Basi kwa vyovyote vile kwa huruma bodaboda atasimamisha pikipiki na kwenda kwa mguu harakaharaka kumchukulia lile gongo. Hapo hapo ndo penye mistake. (One mistake one goal) Bodaboda akiwa anaenda kuchukuwa hongo ndipo Mwizi huyo hudandia Pikipiki na kuondoka nayo Nduki. Watoto wa mjini wanasema anamwachia manyoya huku akijisemea kwa dharau :" Pumbavu Shenzi!"

2) Makazi feki kwenye nyumba ya heri.

Hii nayo inakuwa hivi:
Tofauti na ya kwanza ambapo anakuwa mtu mmoja, hapa hawa mabwana (wezi) wanakuwa kidogo a team. Wanaweza kuwasiliana watatu ama wanne.

Mchezo unakuwa hivi.
Hawa jamaa wanatafuta nyumba yenye geti iliyoko sehemu tulivu sana. Na wanakuwa wanakuwa kuwa wakazi wa nyumba hiyo si wengi na wako bize na mambo yao ( watu wa serikali au wafanyabishara) na once wametoka hawarudi mapema na endapo wamerudi hawatoki tena mpaka kesho.

Basi, hawa mabwana wanajipanga hivi. Wawili ama watatu wanabaki wamejificha maeneo ya getini la hiyo nyumba kisha mmoja wao anaenda kijiwe chochote cha pikipiki na kusellecki (kuchagua) bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwambia ampeleke nyumbani.

Basi bodaboda walivyo na haraka atakubali na kubagain naye bei na kumpakia na kwenda naye kama abiria. Wakiwa njiani, huyu bwana anakuwa anawasiliana na wenzake wale kuwa wanakuja nao wajiseti kisawasawa.

Kama tujuwavyo bodaboda huongozwa na abiria basi jamaa atampekeka mbaka getini kwenye ile nyumba ambayo wenzie wameshajipanga. Basi jamaa (wizi) atashuka na kumpa bodaboda hela kubwa inayohitaji Change let's say 10000 au 5000.

Basi huyu bodaboda akiwa kwenye harakati za kujisachi chenji mfukoni ndipo wale wezi wengine hujitokeza na kumkaba ama kumpiga sehemu mbaya mwilini (wao wanazijua) ambapo ukipigwa mara moja unalegea hata sauti haitoki. Basi wao hujisemea kwa zarau'' Bumbavu" na kuchukuwa pikipiki na kupakizana mshikaki na kuishia nayo.

Aina hii ya wizi hutokea muda wowote . Hasubuhi, mchana na hata jioni.

My take. Chonde chonde, madereva bodaboda kuweni makini sana. Yamkini wewe unaesoma post hii si bodaboda ila una ndugu au jamaa ambaye ni boda boda au kabisa wewe mwenyewe unamiliki Pikipiki na umemwajiri kijana anakuletea hesabu jioni, basi ni mwafaka wa kumpa semina ya wizi huu wa piki piki.
Hiyo style ya pili waliijaribu mtaani kwetu. Na mtaa ulivyo mtulivu walidhani hauna watu.

Hivi ninavyoongea jizi moja limeweka makazi ya kudumu ahera madukani.
 
Inapofungwa hats mwenye Piki piki hujui...unawakabidhi chombo inakuja imeshafungwa na haionekani...inapunguza risk kwa kiasi kikubwa sana.
Haionekani? unajua iyo ni wireless communication lazima kutakuwa na hardware kwenye pikipiki dereva hata asipojua hakuna shida lakini mwizi kama yupo makini anaweza akatafuta na kuharibu hiyo system maana inàmuhusu yeye sio dereva.
 
Dereva tu hajui ilipo,ndio aje kujua mwizi!
Udogo wa pikipiki unaashiria kuwepo na sehemu chache za kuweza kuficha hicho kifaa. Hivi wezi hawawezi kuwa na uzoefu wa kujua sehemu zote muhimu kwenye pikipiki ambazo wataalamu upendelea kufunga kifaa hicho ili mara tu wanapoiweka pikipiki mikononi kazi ya kwanza inakuwa ni kukagua hizo sehemu zote zenye uwezekano wa kuficha kifaa hicho na kukiondoa kwa haraka?
 
Hapa Nchini kumekuwepo na wimbi kubwa la wizi wa pikipiki hasa pikipiki aina ya Boxer.

Tena baada ya uzuka kwa ugonjwa wa Kirona, ndo hali imekuwa mbaya. Watu (bodaboda) wengi wamekuwa wakilizwa mara kwa mara.

Kwa nini pikipiki aina za boxer ndo zimekuwa zikishambuliwa sana kuibiwa? Wengi wanasema kinachotafutwa pale ni injini yake tu. Inasemekana inatumika sana kama mita ya kuvutia na kumwagilizia maji kwenye visima au kilimo cha umwagiliaji. Ila kama ni kuuza kwa ajiri ya spea, wezi hao huziuza kwa bei ya kutupwa sana.

Siku hizi ukiwa na pikipiki mpyunaifanyia kazi basi inabidi uwe mwangalifu sana tena sana. Hasa uwe selective wa abiria wako.

Baada ya utangulizi huo sasa niende kwa maada husika :" Ona hapa aina mbili mpya za wizi wa pikipiki uloshamiri mijini" na hizo mbinu za wizi ni

1) Mhogo feki kwenye mguu.

Hapa inakuwa hivi. Jamaa anachukua mabox ama vitambaa na kujiviringishia pamba juu kwenye unyayo na vidole hadi usawa wa goti mithili ya mtu aliyevunjika mguu na kuwekewa mhogo.

Kisha anachukua gongo na kuzuga nalo mara nyingi wanategeshea maeneo ya hospitali. Anajifanya kama vile ameruhusiwa (discharge) kwenda nyumbani. Anaweza akawa na kijibegi mkononi au mgongoni.

Basi ana chunguza bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwita ampeleke mahali hasa hasa nyumbani. Basi kwa shida sana atapanda piki piki kisha anaondoka.

Trick ya wizi
Mkiwa njiani, tadondosha kwa makusudi lile ngongo kisha kukuomba msimame. Basi kwa vyovyote vile kwa huruma bodaboda atasimamisha pikipiki na kwenda kwa mguu harakaharaka kumchukulia lile gongo. Hapo hapo ndo penye mistake. (One mistake one goal) Bodaboda akiwa anaenda kuchukuwa hongo ndipo Mwizi huyo hudandia Pikipiki na kuondoka nayo Nduki. Watoto wa mjini wanasema anamwachia manyoya huku akijisemea kwa dharau :" Pumbavu Shenzi!"

2) Makazi feki kwenye nyumba ya heri.

Hii nayo inakuwa hivi:
Tofauti na ya kwanza ambapo anakuwa mtu mmoja, hapa hawa mabwana (wezi) wanakuwa kidogo a team. Wanaweza kuwasiliana watatu ama wanne.

Mchezo unakuwa hivi.
Hawa jamaa wanatafuta nyumba yenye geti iliyoko sehemu tulivu sana. Na wanakuwa wanakuwa kuwa wakazi wa nyumba hiyo si wengi na wako bize na mambo yao ( watu wa serikali au wafanyabishara) na once wametoka hawarudi mapema na endapo wamerudi hawatoki tena mpaka kesho.

Basi, hawa mabwana wanajipanga hivi. Wawili ama watatu wanabaki wamejificha maeneo ya getini la hiyo nyumba kisha mmoja wao anaenda kijiwe chochote cha pikipiki na kusellecki (kuchagua) bodaboda mwenye pikipiki boxer mpya na kumwambia ampeleke nyumbani.

Basi bodaboda walivyo na haraka atakubali na kubagain naye bei na kumpakia na kwenda naye kama abiria. Wakiwa njiani, huyu bwana anakuwa anawasiliana na wenzake wale kuwa wanakuja nao wajiseti kisawasawa.

Kama tujuwavyo bodaboda huongozwa na abiria basi jamaa atampekeka mbaka getini kwenye ile nyumba ambayo wenzie wameshajipanga. Basi jamaa (wizi) atashuka na kumpa bodaboda hela kubwa inayohitaji Change let's say 10000 au 5000.

Basi huyu bodaboda akiwa kwenye harakati za kujisachi chenji mfukoni ndipo wale wezi wengine hujitokeza na kumkaba ama kumpiga sehemu mbaya mwilini (wao wanazijua) ambapo ukipigwa mara moja unalegea hata sauti haitoki. Basi wao hujisemea kwa zarau'' Bumbavu" na kuchukuwa pikipiki na kupakizana mshikaki na kuishia nayo.

Aina hii ya wizi hutokea muda wowote . Hasubuhi, mchana na hata jioni.

My take. Chonde chonde, madereva bodaboda kuweni makini sana. Yamkini wewe unaesoma post hii si bodaboda ila una ndugu au jamaa ambaye ni boda boda au kabisa wewe mwenyewe unamiliki Pikipiki na umemwajiri kijana anakuletea hesabu jioni, basi ni mwafaka wa kumpa semina ya wizi huu wa piki piki.
wamekusikia
 
Kuna jamaa mmoja alienda sehemu kwenye kijiwe cha bodaboda akachukua bodaboda siku ya kwanza akaenda site jamaa akashuka akaenda ongea na wale mafundi then akarudi kwa bodaboda akarudi kituoni jamaa akapanda daladala akaondoka

Siku ya pili the same way

Siku ya tatu the same way

Siku ya nne jamaa alivyoshuka kwenye daladala alikuwa amebeba ndoo ya rangi mpyaaa

bodaboda akamkimbilia akamwambia kama kawaida jamaa akasema naaam jamaa akaenda site mshkaji akamwambia tushuke uone nyumba wakawa wanaelekea kwenye nyumba

Ile wanakaribia kufika kwenye nyumba this time jamaa kununua na rangi yaani ile wanakaribia jamaa akamwambia unajua nimesahau misumari hebu nishikie hii ndoo ya rangi nikakimbilie misumari pale road

Bodaboda likawa limebeba ndoo ya rangi akimsubiri jamaa dakika 5, 10, 20, 30 ikabidi awaulize mafundi kama ana namba ya mshkaji ili ampigie amuulize shida nini mbona kachelewa

Kuuliza washkaji wanamwambia Yule sio mwenye nyumba huwa anakuja pale kutafuta kibarua siku ya kwanza hakukutana na fundi mkuu siku ya pili hakukutana na fundi mkuu siku ya tatu hakukutana pia na fundi mkuu na wao walishangaa kumuona anakuja na rangi wakajua maybe wameshaonana na fundi mkuu

Yaani mwamba alikuwa anamdanganya bodaboda naenda site yangu nyumba yangu najenga, mwamba akifika kwa mafundi anafika kuulizia nafasi ya kibarua bodaboda anakaa mbali anajua mwenye nyumba anafanya ukaguzi wa nyumba yake

Jamaa bodaboda alivyoambiwa vile ushuzi ulimtoka bila yeye kujua
Aisee
 
Back
Top Bottom