Ongezeko la watu ambao hawana tabia ya utu ya kusalimia au kuitikia salamu

Ongezeko la watu ambao hawana tabia ya utu ya kusalimia au kuitikia salamu

Hello!!

Anaandika Wadiz a.k.a Baharia

Moja ya sifa na upekee wa binadamu ni utashi wa kusalimiana na kuitikia salamu.

Kumekuwapo ongezeko kubwa la ujeuri, dharau, kibri, vijana wa kiume, wa kike, baadhi yao wakubwa tu hawatoi salamu au kuitikia salamu iwe mnapishana njiani, akukute sehemu labda bar, dukani, kwenye bus, kwenye daladala.etc. Angalizo simaanishi kusalimia hovyo hovyo.

Dadadadeki kuna mfano videmu ukimsalimia haitikii salamu na hata hana tabia ya kusalimia, hakika salamu yangu isipoitikiwa natema mate na nihakikisha huyo mtu aone nikitema mate.

Ingalikuwa watu wanatilia maanani umuhimu wa salamu kama sehemu mojawapo kuu ya utashi wetu sisi binadamu maisha yangalikuwa yenye ubuheri sana.

Mungu wenu wa kanisani na misikitini ni yupi?, malezi na makuzi bora ya jamii ni yanapotea.[emoji849][emoji849]

Je, tunaenda wapi kama jamii?

Wadiz.
Safi uzi nimeupenda huu.Mimi huwa napenda sana kusalimia na huwa sijisikii vizuri kuwapita watu/mtu bila kumsalimia,lkn kuna watu wanakera sana unawasalimia lkn wao hawajibu salamu au wanakupita tu km kisiki.Tabia mbaya sana hiyo.
 
Mjini utasalimia wangapi, utachoka bure. Nina uhakika hata wewe uliyeandika hufanyi hicho kitu otherwise unaishi kijijini au pembezoni mwa mji au Jiji ulilopo. Lakini chukulia sehemu Kama Dar kusalimia Kila unayepishana nae. Huwezi hicho kitu.
 
Hello!!

Anaandika Wadiz a.k.a Baharia

Moja ya sifa na upekee wa binadamu ni utashi wa kusalimiana na kuitikia salamu.

Kumekuwapo ongezeko kubwa la ujeuri, dharau, kibri, vijana wa kiume, wa kike, baadhi yao wakubwa tu hawatoi salamu au kuitikia salamu iwe mnapishana njiani, akukute sehemu labda bar, dukani, kwenye bus, kwenye daladala.etc. Angalizo simaanishi kusalimia hovyo hovyo.

Dadadadeki kuna mfano videmu ukimsalimia haitikii salamu na hata hana tabia ya kusalimia, hakika salamu yangu isipoitikiwa natema mate na nihakikisha huyo mtu aone nikitema mate.

Ingalikuwa watu wanatilia maanani umuhimu wa salamu kama sehemu mojawapo kuu ya utashi wetu sisi binadamu maisha yangalikuwa yenye ubuheri sana.

Mungu wenu wa kanisani na misikitini ni yupi?, malezi na makuzi bora ya jamii ni yanapotea.[emoji849][emoji849]

Je, tunaenda wapi kama jamii?

Wadiz.
Tatizo unataka kuishi maisha ya kijijini kwenu mjini. Mjini wanasalimiana watu wanaofahamiana tu.
 
Kuna jamaa aliagizwa kuja ofisini kwangu sababu ya tatizo alilokuwa nalo ambalo ningeweza kumsaidia.
Jamaa alipofika eneo la ofisi alikuta watu kadhaa nikiwemo na mimi. Alipita bila kusalimia yeyote na kwenda sehemu ilipokuwa amekaa dada wa reception.
Alipofika akaulizia jina langu ndio dada kumjibu mbona umempita hapo nje.

Kimbembe ikawa kuja tena hapo nje na kuniulizia tena ikizingatiwa hakuwa ametoa salamu na alipita katikati yetu maana ilikuwa kama tumekaa kwa mistari 2 na kuacha uwazi katikati.

Mshkaji alirudi nje kinyonge sana na kuuliza mwenye jina langu ni nani hapo. Watu wote wakauchuna kama hawamsikii na hii ilichangiwa na kutosalimia hata aliporudi mara ya pili japo aliuliza kiupole.
Nilikuja kumjibu baadae baada ya kupiga simu kwa aliemulekeza ambae alinipigia na mimi.

Kabla ya kumshughulikia tatizo lake nilimchana kwanza ajifundishe ustaarabu.
Hiyo ni ofisi au kijiwe mnakaa nje kupiga hadithi
 
Mpaka nikasema hii Dar, kusalimia watu njiani ni kusumbua akili yako tu, unakuta kundi la watu unawasalimia hawaitkii, ukiwa na bahati anaitika mmoja tu.

Wakupishana nao ndiyo kabisa, Mpaka unajiuliza kwani una shida gani lwao, unaamia kupishana bila kusalimiana nao, hapa naongelea maeneo yasiyo na pilika, maana kwenye pilika utasalimia wangapi.
 
Mimi sema ukweli salamu hua sipendi, kwanza ni kupoteza muda tu
Wabongo wengi wana tabia za kuweka vipaumbele kwenye mambo yasiyo na umuhimu, wakati mambo ya muhimu hawaweki vipaumbele.

Kwa mfano, unaweza kuwa jambazi unayevaa suti, ukawaibia vizuri sana wabongo, kwa sababu wana tabia ya kuheshimu watu wanaovaa suti. Na unaweza kuwa mtu safi kabisa wa msaada sana, lakini ukapingwa sana hata kuingia ofisini, kwa sababu umevaa jeans iliyochanikachanika.

Watu wengi ni very shallow katika kuangalia mambo ya msingi. Wanafuata formula za kizamanizamani katika dunia inayobadilika kwa kasi sana.

Hapo ndipo unapata hizi habari za kulazimishana kusalimiana na watu ambao huwajui na wao hawakujui mmekutana barabarani tu.

Mtu anaweka msisitizo kwenye kusalimiana na watu asiowajua, ukimuuliza kama anaelewa soko la hisa linavyofanya kazi na "angel investors" ni kitu gani, jibu mara nyingi ni mgogoro.

Atapata wapi muda wa kufuatilia soko la hisa wakati muda wote anataka kusalimiana na watu asiowajua?
 
Kuna jamaa aliagizwa kuja ofisini kwangu sababu ya tatizo alilokuwa nalo ambalo ningeweza kumsaidia.
Jamaa alipofika eneo la ofisi alikuta watu kadhaa nikiwemo na mimi. Alipita bila kusalimia yeyote na kwenda sehemu ilipokuwa amekaa dada wa reception.
Alipofika akaulizia jina langu ndio dada kumjibu mbona umempita hapo nje.

Kimbembe ikawa kuja tena hapo nje na kuniulizia tena ikizingatiwa hakuwa ametoa salamu na alipita katikati yetu maana ilikuwa kama tumekaa kwa mistari 2 na kuacha uwazi katikati.

Mshkaji alirudi nje kinyonge sana na kuuliza mwenye jina langu ni nani hapo. Watu wote wakauchuna kama hawamsikii na hii ilichangiwa na kutosalimia hata aliporudi mara ya pili japo aliuliza kiupole.
Nilikuja kumjibu baadae baada ya kupiga simu kwa aliemulekeza ambae alinipigia na mimi.

Kabla ya kumshughulikia tatizo lake nilimchana kwanza ajifundishe ustaarabu.
Huyo alikuwa hamnazo kabisa. Suala la kusema tu HABARI ZENU JAMANI wakati anapita alionao gumu. Hakukuwa na haja ya kuvaa miwani ya mbao Ilhali anahitaji msaada kwenye ofisi za watu
 
Mimi nikisalimia kikundi Cha watu huwa nafanya marking.. usipoitikia sahau kukusalimia tena. Kuna wamama niliwahi kuwasalimu, ni rafiki zake mama.. walikuwa watu, wawili waliitikia mmoja hakurespond na nilisalimu kwa sauti ya kusikika kabisa.. Hadi Leo, hata kesho na hata milele, sijawahi, sitowahi na haitokaa itokee nikamsalimia hata tukikutana face to face, hata niende home nimkute..
 
Back
Top Bottom