Ongezeko la watu hifadhi ya Ngorongoro kuleta madhara makubwa kwa wakazi asilia na uhifadhi

Tokeni kwenye hifadhi mkapambane huko kama watu wengine...sio kutafuta huruma ya watu hapa
Hifadhi ilianzishwa Wamasai wakiwa pale pale Ngorongoro na wengine kuletwa kutoka Serengeti. Hapo ndipo eneo letu la kupambana. Tulipo hapo tunapambana kimaisha yani. Ni eneo letu la urithi. Hatuondoki.
 
Bora nibebe mizigo nilipwe dola lakin nisiombe. Wanaume wa kimasai wapo hovyo sana, maana wanajua kuzaa tu lakin hawatunzi wake zao wala watoto. Wanasababisha wake zao wanaliwa hovyo kwenye makambi,na watoto wao wanakuwa ombaomba
Ukawe kuli kwenye malori. Acha kubeba mizigo ya wanaume wenzako. Mna makasiriko ya njaa zenu lkn hatuondoki.
Mnataka mkoa mzima uwe mahifadhi tu? Vizazi vyetu viishi wapi wajinga nyie?
 
Sio Ngorongoro tu, Tanzania yote
 
Tokeni kwenye hifadhi mkapambane huko kama watu wengine...sio kutafuta huruma ya watu hapa
Hifadhi ilianzishwa Wamasai wakiwa pale pale Ngorongoro na wengine kuletwa kutoka Serengeti. Hapo ndipo eneo letu la kupambana. Tulipo hapo tunapambana kimaisha yani. Ni eneo letu la urithi. Hatuondoki.
Hata wakurya na waikoma walikuwa ndani ya Serengeti na wakatolewa. It's a matter of time..
 
Ukawe kuli kwenye malori. Acha kubeba mizigo ya wanaume wenzako. Mna makasiriko ya njaa zenu lkn hatuondoki.
Mnataka mkoa mzima uwe mahifadhi tu? Vizazi vyetu viishi wapi wajinga nyie?
Tanzania ni kubwa..kila mahali kuna mapori, acheni kung'ang'ania kuishi maisha ya kuomba omba na mahindi ya msaada. Ngorongoro ni kwaajili ya wanyama sio ombaomba wa kimasai
 
Ngorongoro ni kubwa sn na wala siyo kwamba imejaa mifungo ya wamasai siyo kweli hata kdg
 
Tanzania ni kubwa..kila mahali kuna mapori, acheni kung'ang'ania kuishi maisha ya kuomba omba na mahindi ya msaada. Ngorongoro ni kwaajili ya wanyama sio ombaomba wa kimasai
We kula hela ya watu uendelee kuropoka kama mashine. Njaa zako ndio zinakufanya uongee hivyo.
Sisi tunapambania eneo letu la urithi na sio matumbo kama wewe.
Mahindi ya msaada hatujawaomba.
Ulikuwa ni mpango wa kudiscourage kulima toka ilipokatazwa 2009.
Hujui lolote, unaropoka kama mashine baada ya kulipwa hela ya kula. Na wewe hauna tofauti na omba omba. In short ni omba omba wa rangi tofauti tu.
 
Na ukiona wivu watu wakiomba maanake na wewe ni omba omba.
 
Hii nchi imepata uhuru wakati kila jamii wakiwa katika eneo lao la asili. Hakuna jamii iliyopewa eneo na serikali. NCA imeanzishwa wamasai wakiwa ndani.
Babu zetu waliona pale ndio panawafaa kwa shughuli yao ya ufugaji.
Acheni kuleta mahindi yenu. Wa kufa wafe, wa kubaki wabaki lkn hatuondoki kwenye eneo letu la urithi.
 
Nyie ni wavamizi tu, asili ya masai ni huko Sudan kusini, sio ngorongoro. Acha kupotosha. Hamna urithi wowote pale. Wavamizi tu
 
Nyie ni wavamizi tu, asili ya masai ni huko Sudan kusini, sio ngorongoro. Acha kupotosha. Hamna urithi wowote pale. Wavamizi tu
Ndio akili yako ikipofikia. Hujui lolote. Nikuelelimishe kidogo tu kwamba utaifa unaanza siku taifa lilipopata uhuru na kudefine mipaka yake. Mjinga wewe. Ndivyo mnavyojidanganya?
 
Dah!... serikali zetu hizi huwa zinalal la mno....hivi mpaka watu wanavamia huko kinyemela wao walikuwa wapi?....mpaka wadau wapige kelele ndio wao washtuke tena huku wakichechemea.

Wa-Afrika bhana....
 
Hawa ndo wanyonge. Hiyo mbuga ina mchango mkubwa kwenye pato la taifa wanaiharibu na tozo hawatataka kulipa.

Tuwalinde sana wafanyabiashara na wawekezaji.
 
Gazeti limebainisha kuwa siku za nyuma zaidi kaya 110 ziliwahi kuhamishwa kwa hiyari kupelekwa katika kijiji kipya cha JEMA ambapo waliwekewa miundombinu yote muhimu.
Kama kuna ambao walishahamishwa hili ongezeko la Sasa la watu limetoka wapi?.....au hawa ni wavamizi?

...Au ukame pia umechangia hii kasi ya uvamizi?....kwani hakuna mapori mengine ya akiba yanayofaa kwa kuchunga?....hata kama yapo mbali na makazi yao bado hii sababu haitoshi kuhalalisha uvamizi.
 
basi wapelekee taarifa kwamba ardhi sio mali yao, nimali ya serikali and after all kwa ngorongoro, ile ngorongoro imekuwepo hata kabla ya uvamizi wa wamasai, wamezaliana wakaanza kuishi pamoja na wanyama tukaona vivutio, ndio maana wameachwa hadi leo ila walitakiwa wachapwe viboko vya kutosha kwa kuvamia mbuga. serikali iwafukuze kinguvu tuone wanaenda kudai haki hiyo wapi kwasababu mahakamani hawana sababu ya msingi ndo maana hawatashinda lolote. nilikuwa siamini kama baadhi ya watu hata ukiwasomesha bado akili zao zitabaki porini. hadi wasomi kabisa wanafanya kampeni ati aendelee kuishi kwenye mbuga?
 
Hao watu huko mbugani nani anawajengea barabara, umeme, zahanati, maji n.k.
Aliyewawekea hizo huduma ndio wakulaumiwa.
 
Taifa ni watu. Kuweni wabunifu. Achananeni na sisi. Sisi tunafurahia kukaa huko. Haiwahusu. Mkatafute hela kwingine.
 
Jaribuni kutufukuza muone kama tuna sababu ya msingi au hatuna.
Halafu mnaoshabikia sisi kuondolewa mtakuwa majangili.
 
Taifa ni watu. Kuweni wabunifu. Achananeni na sisi. Sisi tunafurahia kukaa huko. Haiwahusu. Mkatafute hela kwingine.
taifa ni watu na watu sio ninyi tu, watu wachache kama ninyi hamuwezi kufanya tulio wengi tupate hasara ya mbuga kwasababu ya mifugo yenu. kwanza elimikeni mfuge kisasa, mtaishi kiporipori hadi lini?dunia inabadilika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…