Ontario una kipaji sana, ushawishi wako ni kama mganga wa kienyeji au wachungaji feki

Ontario una kipaji sana, ushawishi wako ni kama mganga wa kienyeji au wachungaji feki

Status
Not open for further replies.
Kuna kitabu kinamwelezea tapeli wa Marekani anaitwa Yellow Kid.

Sababu ya kufanikiwa kutapeli watu wengi bila kufikishwa kwenye vyombo vya usalama ni sheria ya miaka hiyo ambayo ilikua ikisema kua kila biashara itataka makubaliano ya pande mbili.

Yakifikiwa askari hawatakua na cha kufanya kwa kua mtu atakua ameingia makubaliano akiwa timamu bila kushinikizwa.
 
kama kwa siku unapata 290,000 kutoka forex so kwa mwezi utakuwa na 8,700,000 ambayo ni mara 16 ya take home ambayo unalipwa na serikali Je umisha acha hiyo kazi ya take home 560K???

Ukawaambie kwanza ma lectures kule vyuoni waache kazi zao za nje au wengine wakafanye biashara wanazofanya

biashara ni part ya maisha kama zingine ndio maana husomei miaka mingi kama profession yangu

cha pili, napenda SANA SANA SANA SANA kazi yangu sijapoteza miaka yote nisije kuifanya ko nafanya vyote
 
kama kwa siku unapata 290,000 kutoka forex so kwa mwezi utakuwa na 8,700,000 ambayo ni mara 16 ya take home ambayo unalipwa na serikali Je umisha acha hiyo kazi ya take home 560K???

sipati kwa siku ni kwa masaa, usiilazimishe data zako
 
Baada ya Nyerere kusema maadui wetu wakuu ni magonjwa, ujinga na umasikini

sasa hivi maadui wetu wakuu ni

1. Chuki

2. Wivu usio na tija

3. Ubinafsi na visasi!

Na hawa maadui wanawaandama mpaka viongozi wetu wa juu wa hili taifa!


watu wana chuki sanaaaa
 
habari wadau

nimegundua kuna watu wana vipaji vya kupiga watu hela... mfano huyu dogo ontario

maana nimesoma thread ambayo dhumuni lake kuu ni kuitangaza bit coin na wenzake apige hela.. ila kaanzia mbali... kamix ma treni humo ya umeme.. kamix ma google map na magari yasiyo na madereva.. ili achanganye watu tu wasielewe kama wanategwa wapigwe hela zao....


nimekumbuka mbali sana....kwenye thread ya kwanza ya forex

mwanzo alianza hivi.. hii ni aya kwenye thread ya kwanza ya forex ya smart mind wetu ontario

Mimi nikikwambia nimelipa Rand 14,000 (ni kama mil 2.5) kwaajili ya 1 to 1 mentorship huwezi kuamini. But wanaoelewa forex wanajua nini namaanisha. Vijana makini sana ambao pia nina malengo ya kumeet nao mwakani wanaitwa AstroFX wana charge $7500 kwaajili ya 1 week training na 6 months guidance ktk forex.

Mimi nimekaa na kuwaza sana, nimefikiria nitoe offer ya watu wa mwanzo kabisa kutoka JF. It's gonna be FREE! namaanisha 100% FREE. Watu 300 wa mwanzo nitakaoanza nao hii safari nitatoa learning materials, trainings, mentorship, na 3 months guidance for free. I am blessed to bless others - Don't misquote me.

Kwanini nafanya free?! Bado forex haijulikani TZ, na ni ngumu sana kubadili mind set ya watanzania wengi - ambao mara nyingi hua hawapendi kujifunza. So, natoa hii kitu for free kwa watu wa mwanzo, ili wapige pesa na wabadili financial status zao. Then hawa watu watakua ambassadors wangu, namaanisha hawa ndio watatutangaza pande zote za TZ. Watu wakimake consistent profits, wakaelewa how it works basi kama watu hawa si wachoyo wa mafanikio wataenda kuwashtua wenzao - ndugu, jamaa na marafiki. Hapo tutaanza na reasonable fees mpk tutakapoona ni muda sasa wa sisi nasi kula jasho letu, ndio tutaanza kuweka bei za faida.

Again I salute all you bosses

ONTARIO.



mwisho wa siku jiulize kama hao watu 300 walipata hiyo huduma free kama alivyoahidi... hii ni njia nzuri ya kumvuta mtu unamwambia huduma free kabla hajakaa sawa unampiga hela zake
hiyo thread ya bitcoin iko wapi sijaiona bado
 
kama kwa siku unapata 290,000 kutoka forex so kwa mwezi utakuwa na 8,700,000 ambayo ni mara 16 ya take home ambayo unalipwa na serikali Je umisha acha hiyo kazi ya take home 560K???


Screenshot_2018-01-09-13-29-03[1].png


bado naendelea kuzichuma taratibu
 
View attachment 671630

bado naendelea kuzichuma taratibu
Hapa ndipo wewe bwana forex unaposhindwa kuelewa.

Watu hawana shida sana juu ya hizo takwimu za transactions.

Kinacholeta ukakasi ni tozo ya darasa la forex.

You do not want to be honest, and that is what rises doubts about you.

Kubali kwanza darasa la forex linatumika kama fursa ya kuchuma fedha, wala sio dhambi.

Kwanini hutaki ku admit hilo?
 
Ukawaambie kwanza ma lectures kule vyuoni waache kazi zao za nje au wengine wakafanye biashara wanazofanya

biashara ni part ya maisha kama zingine ndio maana husomei miaka mingi kama profession yangu

cha pili, napenda SANA SANA SANA SANA kazi yangu sijapoteza miaka yote nisije kuifanya ko nafanya vyote
mkuu nimekuuliza hivyo kutokana nna sentensi yako pale juu unasema ni bora magufuli aongeze kodi ili watu wapanue akili kutafuta njia zingine za kuongeza kipato!
pia kama ktk hiyo forex kwa siku unaingiza hiyo 260K maana yake ukiacha kazi unayoifanya ukawekeza huko kwenye forex naamini baada ya wiki uta double hayo mapato utakuwa unapata 520K,ndio maana nashangaa ni mtu gani duniania ambaye hupo optimistic anaingiza kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa siku kwa nini asiwekeze huko nguvu na maarifa yake bado anangangania mshahara wa 560K-unapendaje kazi amabyo haina tija kwako kimasilahi ??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom