Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

CCM hata wangemsimamisha Amina Salum Ali wangetangazwa washindi tu.

Hivi watu wanadhani haya mabadiliko ya [uteuzi wa makamishna] ya tume ya uchaguzi yaliyofanywa na mwenyekiti wa CCM ni ya bure tu?

Huo uteuzi hata mimi ulinipa mashaka, kwanza aliyekua mkurugenzi alipelekwa kwa majaji, msaidizi wake akapandishwa juu. Nasikia kwenye IT nako yamefanyika mabadiliko, kana kwamba haitoshi mwenyekiti anaaminihsa watu wauamini mfumo wa uchaguzi kwamba utakua wa haki na huru kwa kuwaahidi kwamba matokeo yatabandikwa vituoni.

Nahisi kuna kitu kikubwa sana kipo nyuma ya huu mpango mzima, suala la ushindi ni zaidi ya kura zitakazopigwa na wananchi.
 
Kaka nipishane nawe kidogo...

kwa niyaonayo ndani ya mfumo Lowassa ni namba nyingine...

Tatizo wasilolijua watu ni kwamba CCM ya miaka yote siyo hii tuionayo leo...

So when you talk about CCM unatakiwa u specify...

kama issue ingekua simple hivyo wala isingetumika nguvu kubwa kuvuta upepo!!!

Hapashikiki..hapa kamatiki....

Watu wamejiandaa kwa mbinu na kwa mitaji...

Lowassa si sawa na akina Slaa na Lipumba!!!

Faza,

Mimi najihesabu kuwa ni mmoja wa anti-CCM wakubwa.

Na naombea washindwe vibaya mno hiyo tarehe 25, Oktoba.

Moyo wangu unataka CCM washindwe [na UKAWA washinde] lakini kichwa changu/ akili yangu inaniambia kwa jinsi mazingira ya sasa yalivyo, hilo tamanio langu kutimizika itakuwa vigumu sana.

Kwa hiyo natumaini unachokisema ni sahihi na kwamba CCM itabwagwa.

Lakini kila nikikishirikisha kichwa changu bado sioni hilo likitokea kwa sasa.

Sipendi kukosea ila kwenye hili nikikosea basi nitafurahi sana.

Yangu macho na subira tu kwa sasa.
 
Uchaguzi utakuwaje wa huru na haki wakati tume nzima imeundwa na mwenyekiti wa CCM ambaye chama chake pia kitashiriki huo uchaguzi?

Waache kutusi akili za watu.

Watu ndio kwanza ajira bado mpya na wanataka waonyeshe umashuhuri na nafasi yenyewe ndio hii kisha wapoteze? Huku wakijua kabisa hatma yao na bosi wao aliyewateua iko mikononi mwao?....hapo tuombee yatokee makosa ya kiufundi. Usijekushangaa tayari matokeo yapo mkononi watu wanafanya maandalizi ya namna ya kuyatangaza.
 
Waambie wana wa Israel wasonge mbele. Hayo ni maneno ya mungu kwa Musa. UKAWA tutasonga mbele na tutafika moja kwa moja. Eva ana taka kumpa Adam Tunda. Ushindwe.
 
Kaka yangu Mzee Mwanakijiji asante sana kwa moyo huu.Namshukuru Mungu kwa kukupa moyo wakuendelea kusimamia unachokiamini bila ksita japo umekua ukidharauliwa na kutukanwa na wanaodhani wana mapenzi na Tanzania zaidi yako.
Tuko pamoja na nina imani iko siku wanaokutusi iko siku watakuja kukuomba radhi.
Nazisubiri kwa hamu show zinazofuata nikiamini zitafungua macho ya walio wengi na kuiona picha halisi.

Lowassa ni balaa na Laana inayojaribu kuikumba Tanzania.
Roho inaniuma natamani hata kulia ninavyoona ndugu zetu wanavyokitamani kipande cha chupa wakidhani ni almasi.
Inauma kuona mtu aliye mchafu mbele ya Mungu na wanadamu akifikia hadi kupewa majina ya watakatifu na ya mitume watakatifu wa Mungu.
Uchaguzi wa mwaka huu shetani amejiinua na kuja kama malaika wa nuru na wengi wamevutiwa nae.
Eeh Mungu tunahitaji msaada wako tuepukane na hili balaa.
 
Last edited by a moderator:
Kadiri siku zinavyoenda mbele, Mwanakijiji ni kama anakuwa moko!
 
Hiki kizazi chenu ni cha ajabu sana. Mimi naita kizazi cha kula kulala na porojo. Mmeacha nchi nzuri ikichezewa na familia chache za watu wa ccm huku mnawapigia makofi miaka nenda rudi. Watu wanataka angalau wavuunje mfumo wa kutafuna nchi. Nyie mnaleta POROJO na UNAFKI ni ajabu, uoga na ujinga. Hiki kizazi chenu mtalaaniwa milele kwa kuonesha udhaifu na unafki.

Dr.Mo, dude got paid to start this thread. Very sad.
 
Faza,

Mimi najihesabu kuwa ni mmoja wa anti-CCM wakubwa.

Na naombea washindwe vibaya mno hiyo tarehe 25, Oktoba.

Moyo wangu unataka CCM washindwe [na UKAWA washinde] lakini kichwa changu/ akili yangu inaniambia kwa jinsi mazingira ya sasa yalivyo, hilo tamanio langu kutimizika itakuwa vigumu sana.

Kwa hiyo natumaini unachokisema ni sahihi na kwamba CCM itabwagwa.

Lakini kila nikikishirikisha kichwa changu bado sioni hilo likitokea kwa sasa.

Sipendi kukosea ila kwenye hili nikikosea basi nitafurahi sana.

Yangu macho na subira tu kwa sasa.


Vuta subira mkuu jambazi anaibiwa na jambazi mwaka huu...

Unaposikia habari za kulishana sumu usidhani mchezo...
 
Huo uteuzi hata mimi ulinipa mashaka, kwanza aliyekua mkurugenzi alipelekwa kwa majaji, msaidizi wake akapandishwa juu. Nasikia kwenye IT nako yamefanyika mabadiliko, kana kwamba haitoshi mwenyekiti anaaminihsa watu wauamini mfumo wa uchaguzi kwamba utakua wa haki na huru kwa kuwaahidi kwamba matokeo yatabandikwa vituoni.

Nahisi kuna kitu kikubwa sana kipo nyuma ya huu mpango mzima, suala la ushindi ni zaidi ya kura zitakazopigwa na wananchi.

Ndio maana waliyakataa mapendekeo ya katiba mpya.
 
Lowassa ni balaa na Laana inayojaribu kuikumba Tanzania.
Roho inaniuma natamani hata kulia ninavyoona ndugu zetu wanavyokitamani kipande cha chupa wakidhani ni almasi.
Inauma kuona mtu aliye mchafu mbele ya Mungu na wanadamu akifikia hadi kupewa majina ya watakatifu na ya mitume watakatifu wa Mungu.
Uchaguzi wa mwaka huu shetani amejiinua na kuja kama malaika wa nuru na wengi wamevutiwa nae.
Eeh Mungu tunahitaji msaada wako tuepukane na hili balaa.

Kama ni kweli una sali, huna haja ya kuwatahadharisha watu juu ya mgombea, Mungu anajua na atatupatia rais. Ntashangaa sana kama una uwezo wa kujua uchafu wa Lowassa bila kuomba Mungu na ukitaka watu wakubaliane na mawazo yako. kila mamlaka iliyopo huwekwa kutoka juu.
 
Mpaka sasa sijaona mchango wa Mag3 njoo huku
Nianze kwa kukushukuru mwanga lutila kwa kunikumbuka, kumbe kuna watu wanafuatilia michango yangu! Kwa kweli nimefarijika sana kwa hili.

mwanga lutila, mimi nilianza kuipinga CCM tangu mfumo wa chama kimoja kwa imani na sababu kuwa mchawi na adui nambari one wa taifa hili ni CCM na leo, miaka zaidi ya 20 baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, bado naipinga CCM kwa imani na sababu ziile zile. Ajabu ya maajabu ni dai la Mzee Mwanakijiji kwamba ni sisi tumebadilika kimsimamo na sababu pekee ya kudai hivyo ni kukubali kwetu kumpokea Lowassa kuungana nasi katika hayo mapambano dhidi ya CCM.

mwanga lutila, naomba nikupe tu kionjo kwa kurudi nyuma hadi 13th February 2009 mwaka moja baada ya Lowassa kuwajibika na kujiuzul Uwaziri Mkuu kufuatia kashfa ya Richmond...msome kwa makini Mzee Mwanakijiji, nanukuu;

Na. M. M. Mwanakijiji

Hatuendi mbele, wala hatutoki tuliko. Kama ni jeshini tunaweza kusema tuko kwenye marktime! Na kama ni lori basi tumekwama kwenye matope na magurumu yanazunguka kwa kasi na ngurumo ya gari inapasua anga huku harufu ya moshi wa matairi ikichafua pua zetu. Hata hivyo, hatuendi kokote. Tumebakia kama tumefungwa kamba karibu na vundo la uchafu, na kama tuliokaribishwa karamu kwenye shimo la uchafu, tumeketi, tunajaribu kuziba pua na huku tunajisikia kichefu chefu, lakini hatutoki.

Ni mfano mbaya ninaotumia, lakini inabidi.

Tumepiga kambi kwenye bonde la kashfa. Tulipoanza kujenga Taifa letu tulitaka tuendelee mbele, tulitaka tulete mabadiliko kwa watu wetu na siyo majengo yetu, tulitaka kuona katika Taifa letu watu wote wanakuwa sawa na wenye kufurahia haki zote za msingi za binadamu na huku wakifurahia pia haki zao kama raia. Na sisi tulitaka kujenga taifa la kisasa ambalo lina mazingira mazuri ya maisha na lenye kutoa nafasi sawa ya mafanikio. Bahati mbaya haya sasa yanaendelea kuwa ndoto inayofikiwa na wachache, huku wengi wetu kama taifa tumeendelea kukaa pembeni na kunung'unika kwenye bonde hili la kashfa.

Taifa letu kwa miaka karibu mitatu sasa limejikuta katika mijadala yake limekwama kwenye ile ya kashfa. Sipendi kuziorodhesha tena lakini wingi wake unajulikana na gharama yake inashtua mioyo. Na kama vile watu wasioona mbele tayari tumeshatengeneza kashfa zijazo kwa kuahirisha kushughulikia yanayowezekana sasa! Hatuwezi kuishi bila kashfa.

Tatizo kubwa nilionalo (na nimewahi kuandika huko nyuma) ni kutokuwa tayari kushughulikia jambo la kitaifa na kulimaliza na kufunga mjadala. Inashangaza mwaka mmoja baadaye suala la Richmond bado lipo, miaka nane baadaye suala la rada ndio hata halijaanza kushughulikiwa, miaka karibu kumi na kitu suala la IPTL bado linatoa harufu yake, na miaka karibu 20 uchafu wa BoT bado tunao! Hatuwezi kuendelea mbele kwa kadiri ya kwamba tunaendelea kuketi kwenye kambi hii ya kashfa za ufisadi.

Hatuwezi kwenda mbele kama katika mawazo na fikra zetu tunahangaika na mambo ambayo yangepaswa kushughulikiwa mara moja na daima. NI tabia hii ya kuvumilia uchafu na uovu ndiyo imetufanya tuuzoee kiasi kwamba usafi na wema vinaonekana kuwa ni tunu za "watakatifu" wachache na sehemu ya "waadilifu wateule".

Hatuwezi kwenda mbele na kujadali masuala ya mabadiliko ya taifa ambayo yatachochea kupiga hatua "ile kuu" ya maendeleo kwa kadiri ya kwamba tumeng'angania utamu wa kashfa mbalimbali tukikwepa kuzishughulikia mara moja. Tunaendelea kuchechema kama kulungu aliyenaswa mtegoni!

Tumefika mahali pa kuelezea na kusifia "hatua za maendeleo" ambayo yamo mawazoni mwetu. Tunapita kati ya watu wetu na kuwataka waimbe nyimbo za maendeleo ya kitu ambacho hawakuwa nacho. Unapojenga kisima mahali ambapo hakuna kisima ulichofanya siyo maendeleo bali kukutana na mahitaji ya watu. Maendeleo yatakuwa ni pale ambapo wakazi wa sehemu hiyo wanaweza kupata maji safi ya bomba kwenye nyumba zao!

Unapojenga kliniki mahali ambapo hapana kliniki ya msingi siyo umeendelea bali umekutana na mahitaji ya watu. Maendeleo hapo yatakuwa ni huduma ya kisasa, wataalamu wa kutosha na mchakato bora wa kupata tiba.

Unapojenga barabara ya lami unaweza kuona ni maendeleo. Hata hivyo hilo ni jambo la lazima katika ulimwengu wa leo. Maendeleo basi hapo yatakuwa ni kutengeneza mitaro ya maji machafu, taa zinazofanya kazi za kuongezea magari na zile za kumulika njia, alama nzuri za usalama wa barabarani n.k

Ndiyo maana wengine tulitakaa pale kina Lowassa walipotaka tuimbe wimbo wa kupaa ati kwa sababu tumejenga shule nyingi za msingi kupitia MMEM na miradi mingine. Tulikataa kwa sababu walikuwa wanatuonesha ongezeko la vitu. Walitaka tuone idadi ya wanaffunzi wanajiunga na sekondari na shule ya msingi. Lakini walikwepa kabisa kuangalia kufaulu kwa watoto hao.

Leo hii tulichokisema karibu miaka minne iliyopita kinaendelea kuwa kweli. Tumeongeza mashule, tumeongeza idadi ya wanafunzi wanaoingia shule lakini tumepunguza kiwango cha kufaulu, na kwenye masomo ya sayansi na kiingereza bado tuko nyuma sana. Siyo kwenye shule za awali bali hata kwenye vyuo! Tumepiga kambi kwenye kashfa nasi tumezizoa.

Naamini wakati upo, na haja ipo ya kubadili fikra zetu na kukataa kucheza mdumange wa kashfa huku tukipiga filimbi za ufisadi. Ni lazima tukatae kulazimishwa kucheza mganda wa sifa za uongo huku tukiruka ruka kamba za kudanganyana.

Kama taifa ni lazima tutoke kwenye kambi hii ya kashfa na kuingia katika uwanja wa ujenzi mpya wa taifa la kisasa. Tuweze kukusanya nguvu zetu za kifikra kujadiliana jinsi ya kuboresha vilivyopo na vipya. Tuweze kutoka katika kashfa za BoT, Bunge, n.k na kuanza kujadiliana jinsi ya kuiboresha BoT, Bunge, Mahakama n.k Tuweze na sisi kutumia uwezo wetu na vipaji vyetu tulivyopewa na Mungu bure kutatua matatizo yetu.

Vinginevyo, tutaendelea kukodoleana macho, kutukanana, kutafutana wachawi, kubezena, kupigana vijembe, huku tukicheka cheka, tukiremburiana macho na kukonyezana, katika bonde hili la kashfa na ufisadi, kiasi kwamba kizazi kijacho kitakapoamka kitatulaani kwa kupoteza muda katika shimo la takataka!

Tuamue kutoka, na wale ambao hawataki tuwafukie na takataka zao!

Mwenzenu,
Ndugu yenu,
Rafiki yenu,
Na kwa wengine....
Adui yenu


Na isimame kama ushahidi na mashtaka dhidi yetu!
M.M. Mwanakijiji
Feb 13, 2009
mwanga lutila, huu ndi ulikuwa ni mchango wangu kufuatia mada ya Mzee Mwanakijiji, nanukuu;
Tatizo watanzania wengi tunaanza kulizoea hili bonde na kuliona kama makao yetu ya kudumu. Ndiyo, na aliyetupeleka bondeni anajua fika kuwa nje ya bonde atapoteza nguvu kwa kuwa huko kuna hewa safi isiyoruhusu ustawi wa uvundo.

Bunge limegeuzwa kuwa baraza la kutunga sheria kudhibiti na kuzima mawazo yoyote ya kuhama bondeni. Serikali inalinda huu uvundo kwa nguvu zake zote kwa kisingizio cha amani na utulivu bila kujua inatafuna watu wake pole pole kama kansa.

Wengi baada ya kuathirika na uvundo wamepoteza kabisa uwezo wa kunusa, kusikia wala kuona na wanachapa usingizi bila wasiwasi. Wachache ambao hawajaathirika sana wamefungwa kamba miguuni na kuzibwa midomo wasije wakawakosesha wenzao usingizi
.
mwanga lutila, mwaka 2010 tulikuwa na uchaguzi mkuu na pamoja na kashfa zote na lawama zote kwa serikali ya chama tawala, CCM ilitangazwa kushinda uchaguzi na mgombea wake Jakaya Mrisho Kikwete kuongezewa awamu nyingine ya miaka mitano na leo tuko hapa tena. Mgombea wa Chadema mwaka huo alikuwa ni Dr. W. P. Slaa.

Swali la kujiuliza ni je hilo bonde la kashfa alilokuwa akiongelea Mzee Mwanakijiji bado lipo? Je anayeamua kutoka kwenye hilo bonde na kutafuta hewa safi huko nje ana kosa? Je kutoka kwa mtu moja ama wawili kunalitakasa hilo bonde? Je kwa nini kwa miaka minane baada ya Lowassa kujiuzulu tofauti lolote halikuweza kuonekana bondeni na badala yake kasi ya kashfa ndio ikaongezeka?

Mathalan, hivi kati yangu mimi, Mag3, na Mzee Mwanakijiji nani anaonekana amebadilika kimsimamo? Huyo Lowassa kama angeteuliwa kugombea Uraisi akiwa ndani ya hilo bonde ningempinga kama ninavyompinga Magufuli. Lowassa kaonesha ujasiri mkubwa kwa kulitosa hilo genge na kujiunga na sisi wana mabadiliko na tutamkaribisha mtu yeyote atakayeweza kuongeza nguvu katika hii vita; Tanzania bila CCM yawezekana.

Rejea: Taifa lililopiga kambi kwenye bonde la kashfa!
 
Kaka yangu Mzee Mwanakijiji asante sana kwa moyo huu.Namshukuru Mungu kwa kukupa moyo wakuendelea kusimamia unachokiamini bila ksita japo umekua ukidharauliwa na kutukanwa na wanaodhani wana mapenzi na Tanzania zaidi yako.
Tuko pamoja na nina imani iko siku wanaokutusi iko siku watakuja kukuomba radhi.
Nazisubiri kwa hamu show zinazofuata nikiamini zitafungua macho ya walio wengi na kuiona picha halisi.

Lowassa ni balaa na Laana inayojaribu kuikumba Tanzania.
Roho inaniuma natamani hata kulia ninavyoona ndugu zetu wanavyokitamani kipande cha chupa wakidhani ni almasi.
Inauma kuona mtu aliye mchafu mbele ya Mungu na wanadamu akifikia hadi kupewa majina ya watakatifu na ya mitume watakatifu wa Mungu.
Uchaguzi wa mwaka huu shetani amejiinua na kuja kama malaika wa nuru na wengi wamevutiwa nae.
Eeh Mungu tunahitaji msaada wako tuepukane na hili balaa.

Nyie watu acheni unafki nilini mlianza kujua kuwa Lowasa ni Fisadi mayowe haya mnayopiga Yanatudhihirishia bila shaka mmekwiba sana kwenye hii NCHI sasa mnaona huyo jamaa akiingia madarakani Atawafanya vibaya huyo MM yuko kzn so Lazima atimize wajibu wa waliomtuma lkn asidhani km kuna MTU asietumia Utumbo kufikiri ataweza kuMbadilisha kwa hizo Ngano....zake wengine tulishaikataa CCM tangu 1995 sasa kuja na blah blah kama hizi nikupoteza Muda wengine tunazipitia hizi thread kwaajili yakuona Watu wazima wanavyojitoa ufahamu sababu Njaa.......
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom