Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Elections 2015 Operesheni Zinduka: Uamuzi Sahihi 2015

Inaelekea watu hawalali wanaumiza kichwa kisa jina Lowasa...kama hawaletei homa why mnapanic.lalen usingizi muone cha moto nyie majambazi sugu
 
Mzee Mwanakijiji hoja zako za kupingana na Lowassa kusimamishwa na chama / vyama ambavyo watanzania wanategemea kuwa ndio nguzo ya kubadili uongozi na think-tank ya uongozi ni nzuri na kiuhalisia binafsi najiuliza maswali kadhaa. Baadhi ni haya..

Kwa sasa naomba niishie hapo kwanza.

Maswali yako mazuri sana nitayajibu katika show mojawapo, nakuahidi.
 
Last edited by a moderator:
Sawa nmekuelewa sasa kwa kuwa umesema nisimpigie El sasa nikuulize nimpigie Nan? Na kwa nn... Mm ni mwelewa so ntakuelewa
 
Mzee Mwanakijiji[/JFMP3] , Mchungaji Mtikila alikuwa anaipenda Tanganyika, siyo Tanzania, sasa inakuwaje kwa heshima yake unaimba 'Tanzania Tanzania Nakupenda Kwa Moyo Wote'?
 
The most useless thing I know to date


Mwanakijiji nakuhakikishia, hata utushawishi vipi, ushawishi wako ni bure kabisa. Sisi tunaoelewa hila na janja zako tumeshazielewa na hatubabaishwi na harakati zako za kipuuzi. Mimi nimeamua kwamba Oktoba 25 2015, alfajiri na mapema kama ilivyokuwa mwaka 2010 nitakuwa wa kwanza kumpigia mgombea wa upinzani na safari hii ni Edward Lowassa. Hata upinzani ungekuwa umesimamisha JIWE BADO NINGECHAGUA JIWE.

Wewe unaishi Marekani lkn bado uelewa wako mdogo sana, hukuona katika chaguzi wa Marekani katika majimbo ya Blue (Democrats) na Nyekundu (Republicans) wanachagua chama tuuuuu hawachagui chama pinzani. Sasa unayetaka kutuhujumu sisi ukiwa ugaibuni unataka kutuambia nini?

Mwaka 2010, nilimchagua Dr Slaa, kwa dhati kabisa kwa sababu mimi ni mwana mageuzi na nilikuwa mtu wa kwanza kupiga kura ktk kituo changu. Na mwaka huu Mungu anipe nguvu na uhai bado nitajihimu asubuhi na mapema ili kumpigia Ndugu Edward Lowassa na madiwani na wabunge wa UKAWA (yaani CHADEMA, CUF NCCR na NLD).

Wewe huna maana ya kuwaghilibu watanzania kwa kununuliwa na CCM. Tuache sisi na Lowassa wetu na hata ukikazana sana bado hutamweza. Kumbuka Watanzania wa mabadiliko toka jana, leo na hata kesho watachagua mabadiiko tu. Si vinginevyo.

Tunataka tuachane na ghiliba za CCM kwa gharama yoyote na Lowassa ni njia tu ya kufika huko. Kwa hivyo hatudanganyiki. Kama wewe umenunulika basi lakini tunaoelewa maana ya siasa ya ushindani hatuwezi kudanganyika kirahisi kihivyo.

MIMI nilitegemea utatupa uzoefu na ujanja wa nchi za magharibi kama Marekani unayoishi kumbe lengo lako ni kutaka kutuhadaa Watanzania kutoka kwenye agenda ya uchaguzi na kutuletea maneno ya mtaani.

Kumbuka Watanzania hatuchagua MALAIKA awe rais wa Tanzania. Tunachagua binaamu awe rais wa Tanzania. Na binadamu huyo aweza kuwa Ndg. Lowassa au Magufuli. Hakuna katika hao au hata ningekuwa mimi atakayekosa dosari. Au chukulia uwe wewe ndio mgombea wetu bado ungekuwa na dosari nyingi tu. Kwa hiyo, suala la kutuambia kuwa eti Magufuli ni nafuu halina maana halina nafasi hapa.

Kama wewe umem-feel sana Magufuli mchague wewe na ukoo wako. Waache watanzania wachague Tanzania wanayotaka. Wewe umechagua Marekani lakini sisi tumechagua mama Tanzania. Tunaipenda sana kwa dhati kabisa.

Munu ibariki mama Tanzania na Mungu umtie nguvu na uwape mioyo wa ushindi Ndugu Edward Lowassa na Watanzania wote wa mabadiliko.
 
Hiki ni kituko. Hivi mtu ambaye hata hapigi kura eti anawaelekeza wapiga kura wasimchague kiongozi ambao wao wanaamini ndio anayewafaa
 
Hivi Mwanakijiji unajifanya unaakili sana kushinda sisi?

Unajiaminisha kabisa kwamba unaweza kubadili fikra za Maelfu na maelfu zinazomuunga mkono Lowassa? Umechelewa sana kaka, kazi hii uliyojitwisha sasa ni ngumu kama kujaza maji kwenye pakacha...... UTATOKA JASHO LA DAMU, MAJI HAYAJAI NG'OOOO!!

Nilijua umejifunza kitu kwa mada zako kinzani kwa wapenda Mabadiriko toka ulupoanza kuandika , kumbe sufuri kabisaaa.!!!

Jiandae kisaikolojia kaka, Lowassa hakwepeki pale Magogoni!!

BACK TANGANYIKA

Yote kwa yote huyo Mchumia tumbo Mwanakijiji hataweza chochote. Alishindwa Dr Slaa kwenye field sembuse maandiko haya mufilisi ndani ya Jamii Forums ambapo wengi wa Watumiaji wa JF ambao ni wapiga kura walishaamua nani wamchague. Wale wanaoamini Magufuli ambao ni JF Users na wale wa Lowassa katu huwez kuwabadilisha kwa porojo zako wewe uko kwenye Key board unafikir Watanzania wanadanganyika?
 
Hiki ni kituko. Hivi mtu ambaye hata hapigi kura eti anawaelekeza wapiga kura wasimchague kiongozi ambao wao wanaamini ndio anayewafaa

Mkuu thibitisha hili ili nisiwe kifuata upepo maana nahitaji mabadiliko
 
Sawa nmekuelewa sasa kwa kuwa umesema nisimpigie El sasa nikuulize nimpigie Nan? Na kwa nn... Mm ni mwelewa so ntakuelewa

Hili ndilo swali ambalo Mzee Mwanakijiji anapaswa alijibu badala ya kuzungukazunguka? Atueleze je tumpigie Mama wa ACT? Je, anakubaliana na waraka huo hapo unaosemekana ni wa ACT au bado anawaona hao ni wasaliti?

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimekuwa na mawasiliano na Dk. Wilbrod Peter Slaa, mwanasiasa nguli wa upinzani nchini, kuhusu uwezekano wa yeye kushiriki katika kampeni za Chama chetu kwa lengo la kuendeleza vita dhidi ya ufisadi nchini.

Tunamshukuru sana Dk. Slaa kwa imani aliyo nayo juu ya chama chetu na uamuzi wake wa kuikabidhi rasmi ACT-Wazalendo, mikoba yake ya vita dhidi ya ufisadi nchini.

Dk. Slaa anaamini kwamba chama chetu cha ACT-Wazalendo ndicho chama pekee chenye uhalali na uwezo wa kupambana na ufisadi baada ya chama chake cha zamani kuitelekeza vita hiyo. Dk. Slaa alikuwa ashiriki kikamilifu katika kampeni za uchaguzi zinazoendelea kupitia jukwaa la ACT-Wazalendo.

Alikuwa aanze na Mkutano wa hadhara Mjini Iringa siku ya Jumatano tarehe 7 Oktoba 2015, na baadaye angeendelea na mikutano mingine katika majimbo mbalimbali na kuhitimisha kampeni hizo katika Viwanja vya Mwembeyanga Jijini Dar es Salaam, ambao ndio uwanja ambapo vita dhidi ya ufisadi ilitangazwa rasmi mnamo tarehe 15 Septemba 2007.

Baada ya tathmini ya kina chama cha ACT-Wazalendo kimejiridhisha kwamba hali ya usalama wa Dkt Slaa ni ndogo sana kwa sasa kutokana na vitisho mbalimbali anavyovipata. Kutokana na hali hiyo ya vitisho dhidi ya usalama wake, chama chetu kimejiridhisha kuwa hakina uwezo wa kumhakikishia Dk. Slaa usalama wake atakapokuwa majukwaani.

Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, chama chetu kimefuta mikutano yote ambayo Dk. Slaa alikuwa aifanye kupitia jukwaa la ACT-Wazalendo. Chama kitaendelea kutambua mchango wake katika harakati za kukuza demokrasia na hasa bidii yake ya kujitoa katika kupambana na ufisadi nchini. Tunamuahidi kwamba chama chetu kitaendeleza vita hii kwa bidii kubwa na juhudi zake kamwe hazitapotea.

Tunamtakia Dk. Slaa na familia yake maisha mema.

Samson Mwigamba
KATIBU MKUU

Jumatatu Oktoba 5, 2015.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...brod-slaa-kwenye-chama-cha-act-wazalendo.html
 
Last edited by a moderator:
Liulize hili swali kivingine..nguvu kubwa ya kumsukumizabLowassabkwa Watanzania ya nini na kwanini? Ukipata jibu la swali hili utapata na jibu lako.

Kwani nani anamsukumiza Lowassa kwa watu? Ingekua ni suala la kusukumizwa leo hii Lowassa angekua na wafuasi kwa maneno na kashfa zote zile wanavyomchafua nazo? Nakubaliana na cabhatica upinzani mkubwa wa kumpa nafasi Lowassa kua rais ndio ulionifanya nione kuna kitu cha ziada ambacho wengi hatukielewi....dawa ni kumpigia kura Lowassa ili wengi tuweze kujua ni kitu gani haswa wakuu wanakiogopa na wameamua kwa wazi kutumia kila njia halali na ovu kuhakikisha Lowassa hapati nafasi.

Mwisho kabisa, tangu utoe taarifa za uongo kuhusu hali ya amani zanzibar wakati wa uamsho na wafanyakazi wa UN kwamba ulinzi ni mkali nikagundua kwamba habari zako zina walakini.
 
Last edited by a moderator:
Huyu mzee nilikuwa namuheshimu sana ila kwa sasa hapana aseeh nahisi huyu ni aina ya akina dr slaa kabisa hawa wazee wachumia tumbo ni mizigo kwa taifa alaf hivi wew upo nchi gani kwanza?
 
Mimi nilifikiri kuna kitu cha maana kwenye the so called VIDEO, lakini ndani yake nimegundua kutokujiamini kwa the so called Mzee Mwanakijiji.

Ukisikia mtu anasema 'TUTA.....' hii ni dalili ya kutojiamini. Umetutangazia operesheni ukianza na 'NITA......' huku mbele tena unaanza 'TUTA....'. Kwa kifupi sijaambua jambo zaidi ya ngonjera.

Unaposema SISI unamaanisha wewe na nani?
 
Last edited by a moderator:
Mpakwa mafuta Mzee Mwanakijiji,

Teh teh teh!

Leo upo "kigango" gani? Naona unaendelea na kazi yako ya "Mchumia dini"

Nisalimie Vatcan!
 
Last edited by a moderator:
Hata hao unaowaona kwenye mikutano ya Magufuli hawana muda wa kusikiliza mahubiri ya namna hii yako, sana sana wanapenda kumsikiliza Diamond na Ya Moto Band.

Ngonjera zako zimekosa vina
 
Mitaa inaendelea kuzinduka maelfu kwa maelfu. Wamemkataa lowassa na genge lake lote la mafisadi.
 
Back
Top Bottom