imagenyce4real
Member
- May 25, 2015
- 31
- 3
Ndiyo maana nikiwa kwenye mood ya kuangalia Comedy huwa naangalia Churchill ya Kenya yaani unajikuta unacheka na kutoa stress zote kabisa....Hata kama sintokuwa mzalendo lakin unakuta unaangalia Original Comedy unatafuta wapi utacheka mpaka show inaishia hakuna kichekesho hata kimoja.
Afya ni majaliwa ya Mungu,leo kundi la OK linasimama majukwaani kwenye kampeni za ccm hata kutoa post mitandaoni za kudhihaki afya ya Lowassa wamesahau yalimpata mwenzao Vengu? mwaka wa nne leo yuko kitandani.ikumbukwe huyu jamaa alikua ni bingwa wa kumuigiza Mrema na maradhi yake kwa bahati mbaya Mungu kampiga kofi leo hii yeye ndio yuko kitandani na Mrema huyoooo yuko mzima kabisa.
Tukumbuke tunayo yafanya Mungu anatuona.kuna Leo na kesho.
Hata CCM yenyewe haielewi damage inayopata kwa kubeza afya ya Lowasa na kufanya kama kitu cha kujivunia maana hata wapambe wao walio kwenye msafara wa Magufuli na Samia wanatumia maneno ya kejeli kuhusu Afya.
Namfahamu jamaa mmoja ambaye ilikuwa hata nimwambie nini kuhusu CCM na Magufuli alikuwa haelewi kitu, lakini nyumbani kwake ana Baba yake mzazi ni mgonjwa alipata stroke kama mwaka sasa na anaendelea na matibabu. Majuzi Lusinde sijui akiwa wapi akakebehi afya ya Lowasa na majigambo chungu nzima.
Toka maneno yale yule jamaa amekidharau hicho chama na wagombea wake kwa kukubali kupigiwa upatu kwa kukashifu afya za wengine. Jee ni wangapi wataidharau ccm kwa kauli za kuwadharau watu kwa afya zao?
Kwa upande wangu simfagilii kabisa Lowasa ....!
Mkuu hatudharau afya ya mtu.. Kumbuka hatuchagui rais pekee pia tunachagua amiri jeshi mkuu...... Afya ni kigezo ktk kazi yoyote na si urais pekee??
Ze comedy hawana mvuto na mda mrefu ka miaka miwili sijaangalia kipindi chao. Tatizo ubunifu zero sasa ukishamkashifu afya ya mtu ndo umeongeza kura za CCM mijitu mingine bwana. Wananchi wanawachora tu kuna watu wazima na wanakufa ghafla usingizi. Wanatukana wakunga na uzazi ungalipo.
Unamuulizia Gwajima mbona katoa tamko juzi tu hapa
salaaaaaaale!!!steve nyerere anaugua miwa.ya.
Na wala hatumbezi wala kumchukia.
Wema ana nundu kama la ngamia mgongoni, ni wakati tu utafika litakapo kuja kuwa malignant tumour.
Hiyo slogan nasikia imeongezwa ili msilaumiane baadae. #HAPA KAZI MDOMONI TUUKwa upande wangu simfagilii kabisa Lowasa kwani ni Fisadi na mlafi wa madaraka ndio maana atafanya lolote ili mradi tu aingie Ikulu maana nia yake ni kuingia Ikulu tu. Anapaswa kufanya nini Ikulu yeye anaona ataelewa akishafika Ikulu! Sasa kwanini tu-RISK? Hata hivyo sio hekima kabisa kutetea hoja kwa kuhusisha Ugonjwa wake na kumkebehi ! hapo ni kushindwa kujenga oa zenye mashie! Sijasikia Muhusika Mkuu Kumkbehi. Nami ninaiani nae kwani amejhiipambanua kutoka kwenye mabaya ya Chama Chaketangu kwenye utedaji wake. HAPA KAZI TU!
Hivi ze comedy bado ipo,?
Afya ni majaliwa ya Mungu,leo kundi la OK linasimama majukwaani kwenye kampeni za ccm hata kutoa post mitandaoni za kudhihaki afya ya Lowassa wamesahau yalimpata mwenzao Vengu? mwaka wa nne leo yuko kitandani.ikumbukwe huyu jamaa alikua ni bingwa wa kumuigiza Mrema na maradhi yake kwa bahati mbaya Mungu kampiga kofi leo hii yeye ndio yuko kitandani na Mrema huyoooo yuko mzima kabisa.
Tukumbuke tunayo yafanya Mungu anatuona.kuna Leo na kesho.
Pia kama miujiza ikitokea akawa Rais mda wake mwingi atakuwa anautumia kwenye matibabu India au US nk... Sasa Rais kama huyu wa nini? Mchagueni mtu mwenye siha yake bwana... #hapa kazi tu.
Kikwete alikuwa anashinda uko alikuwa mgonjwa? Je si amemaliza kuongoza?
Uzuri anaetamka kuwa hapa kazi tu amekwishaifanya tumeiona jamani hebu nielezeni alichofanya huyo mtu wenu. Hana ubavu wa kusema hapa kazi tu. Hana ubavu wa kusema atawashughulikia mafisadi hebu nieleze alichokifanya miaka 20 ya uwaziri na miaka 30 ya Ubunge. Mbona rahisi sana hebu nieleze na Vidhibiti!Hiyo slogan nasikia imeongezwa ili msilaumiane baadae. #HAPA KAZI MDOMONI TUU