Orijino Komedi wanapokashifu afya ya Lowassa, wamesahau ya mwenzao VENGU?

Orijino Komedi wanapokashifu afya ya Lowassa, wamesahau ya mwenzao VENGU?

Afya ni majaliwa ya Mungu,leo kundi la OK linasimama majukwaani kwenye kampeni za ccm hata kutoa post mitandaoni za kudhihaki afya ya Lowassa wamesahau yalimpata mwenzao Vengu? mwaka wa nne leo yuko kitandani.ikumbukwe huyu jamaa alikua ni bingwa wa kumuigiza Mrema na maradhi yake kwa bahati mbaya Mungu kampiga kofi leo hii yeye ndio yuko kitandani na Mrema huyoooo yuko mzima kabisa.

Tukumbuke tunayo yafanya Mungu anatuona.kuna Leo na kesho.

Hooo mungu wangu!nimepata maumivu sana kwa hayo manenoyako,lakini wakumbuke kua LOWASA ajawahi hata kulazwa wuodini lakini mbona vengu yeye yukochini.bac umenitonesha kidonda maana nampenda sana jamaa kiukweli.
 
Nimeumia sana kama wasanii wa Tanzania wamekosa ujuz hadi kuanzia kubeza afya za watu nan anayejua hatma ya maisha yake . Wanawafundisha nn watoto wetu wanaoangalia . Mm huwaga siangaliii kabisa kipindi chao hicho wameishiwa Wameingia kwenye siasa Mwenyez mungu tunaomba impinge lowasa wetu
 
Mkuu hatudharau afya ya mtu.. Kumbuka hatuchagui rais pekee pia tunachagua amiri jeshi mkuu...... Afya ni kigezo ktk kazi yoyote na si urais pekee??
 
Ze comedy hawana mvuto na mda mrefu ka miaka miwili sijaangalia kipindi chao. Tatizo ubunifu zero sasa ukishamkashifu afya ya mtu ndo umeongeza kura za CCM mijitu mingine bwana. Wananchi wanawachora tu kuna watu wazima na wanakufa ghafla usingizi. Wanatukana wakunga na uzazi ungalipo.

Mami angu penda wew sana unanipaga raha sana na comments zako
 
Mkuu hatudharau afya ya mtu.. Kumbuka hatuchagui rais pekee pia tunachagua amiri jeshi mkuu...... Afya ni kigezo ktk kazi yoyote na si urais pekee??

Kwani raisi akiwa amiri jeshi afya yake inahusiana na nini?
Kwani ulishamwona kikwete anapiga push up?
Haiusiana hata kama raisi anatembelea wheelchair kama ana akili ya mabadiliko bado atafanya vyema
 
Mkuu hatudharau afya ya mtu.. Kumbuka hatuchagui rais pekee pia tunachagua amiri jeshi mkuu...... Afya ni kigezo ktk kazi yoyote na si urais pekee??

Kwa hiyo Amiri Jeshi hawatakiwi kuumwa? Mbona JK aliumwa tezi dume mpaka akafanyiwa operation?
 
Ni wanafiki sana hawa.
Kama huyo masanja ana laana maana amezoea kumkufuru Mungu na uchungaji hewa.
Eeeh Mungu wapige pigo kali ili wajue hata afya waliyo nao ni kwa huruma zako wala hawakustahili... sumbai umewaona og comedy?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu ungetuwekea hzo kashfa hapa.

haiitaji hata elimu ya ya darasa la saba kung'amua nani mlengwa kwenye hii tweet ya Orijino Komedi.
 

Attachments

  • 1441971889760.jpg
    1441971889760.jpg
    51.2 KB · Views: 1,051
Hakuna haijuaye kesho yake. Na hujafa hujaumbika. Kumbuka Mungu hadhihakiwi.
 
Hata Wema na Steve nao wamefanya upumbavu huo...hivi kweli Wema ni mzima? Hivi kweli Steve Nyerere ni mzima?

Steve nyerere si juzi tu alikuwa anaungua ugonjwa wa ajabu?
 
Hili jambo lilisababisha Majuzi nikaleftishwa kwenye group la whatsup. Yaani kuna ushabiki wa hatari sana, nilishangaa watu wazima wenzangu wakishabikia afya ya mzee wa watu! ! Nakumbuka nilikuwa mkali kama pilipili nawaambia hawaelewi nilijikuta nimewatukana matusi mazito watu wazima tena wengine zaidi yangu. Mi sio mshabiki wa EL lakini najua ninini Ugonjwa na kwetu kuna wakubwa!
 
Back
Top Bottom