Orodha ya Miji yenye hadhi isiyostahili

Orodha ya Miji yenye hadhi isiyostahili

Upo sahihi sana,inabidi irudishwe kama zamani iwe Tarafa ya Same.Mzee Msuya inawezekana kuna rafu ya ushawishi aliifanya enzi zake
Kama mzee Pinda alivoshawishi Mpanda kuwa manispaa, na mzee Brigedia jeneral Hassan Ngwilizi alivomshawishi mzee wa msoga akamuingiza chaka eti Tanga iwe jiji.
 
Kwakweli Shinyanga kwa sasa imefunguka imeamka, kasi ya maendeleo nikubwa mno. Kwa waliotembelea Shy kuanzia 2020 kurudi nyuma na sasa nadhani wameona mabadiliko makubwa sana. Mji umefunguka umeanza kuchangamka. Pia wengi wanapita barabara kuu wanajua ndio mjini kati hapo ila hapo wanapopita ni pembeni, mji umefunguka sasa CBD inakimbilia lubaga na mpaka bushushu uelekeo wa oldshy,mahotel yanajengwa kwa kasi na biashara zinafunguliwa kwa kasi. Pongezi za dhati kwa mkurugenzi aliepita bwana jomari satura hakika alikua na juhudi za dhati kuubadilisha mji walau sasa mji unaonekana.
 
Kumekuwepo na mjadala kuhusu Majiji.

Ukweli ni kwamba sio Majiji tu ambapo yapo yenye hadhi hiyo ilihali kiuhalisia ilipaswa yawe manispaa Tu.

Leo nakupa orodha ya manispaa zisizostahili hadhi hiyo.

1. Lindi
2. Shinyanga
3. Tabora
3. Singida
5. Kigoma
6. Songea
7. Musoma
8. Bukoba

Manispaa hizo kimiundombinu na maendeleo ya mtu mmoja mmoja bado Sana. Mfano Shinyanga nilipofika nilibak mdomo wazi.

Taja manispaa zingine
Tanga.
 
Mbeya ina sifa ya ukubwa,idadi ya watu na shughuli za kiuchumi kuwa nyingi.ukianzia uyole mpaka mwanjelwa pameunganika wakati zamani ilikuwa mashamba tu.Tatizo la mbeya ni city centre ni ndogo na haieleweki.Hadhi ya jiji ni msukumo wa kisiasa na jiji kukosa miundo mbinu bora nazo ni hujuma za kisiasa.Kiukweli ni juhudi za wana mbeya wenyewe kufika hapo ilipo.Watawala wamefanikiwa kuihujumu ķimuonekano lakini kiuchumi nafsi zao zinawasuta!
 
Back
Top Bottom