Orodha ya Wakurugenzi Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) tangu Uhuru

Orodha ya Wakurugenzi Wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) tangu Uhuru

True

Kwa wakati mmoja Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa na CDF walikuwa Viongozi wa Kanisa!
CDF kaandika mpka kitabu cha dini, kina uzwa huko kwa wakatoliki na pesa zote zinazo patikana ni kwa ajiri ya kanisa, hachukui hata sent

 
ORODHA YA WAKURUGENZI WAKUU WA 'TISS' TANGU UHURU.

Idara ya usalama wa Taifa (TISS) imeundwa kwa sheria ya bunge namba 15 ya mwaka 1996 (Tanzania Intelligence and Security Service act No. 15 of 1996) iliyosainiwa na Rais Benjamin Mkapa tarehe 20 mwezi Januari mwaka 1997. Sheria hiyo ndio inayoipa mamlaka Idara hiyo kufanya kazi zake ndani na nje ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Pamoja na idara hii kusajiliwa kisheria mwaka 1996, lakini ilkuwepo tangu wakati wa utawala wa kikoloni chini ya ofisi ya Gavana wa Tanganyika. Baada ya Uhuru mwaka 1961 ilihamishiwa ofisi ya Rais.

Tangu idara hii kuanzishwa hadi sasa imeongozwa na Wakurugenzi 9 akiwemo Diwani Athumani Msuya aliyepo kwa sasa

Wa kwanza ni mzee Emilio Mzena, huyu aliongoza mwaka 1961 hadi mwaka 1975. Ndiye Mkurugenzi wa TISS aliyeongoza idara hii kwa miaka mingi zaidi kuliko wengine (miaka 14). Aliaminiwa na Mwalimu Nyerere baada ya idara yake kuzima majaribio kadhaa ya kumpindua.

Wa pili ni Dr. Lawrence Gama (PhD). Huyu alipokea kijiti kutoka kwa Mzena. Aliongoza kwa miaka mitatu tangu mwaka 1975 hadi mwaka 1978, kabla ya Mwalimu Nyerere kumuondoa katika nafasi hiyo na kumteua kuwa mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Wa tatu ni Dr. Hassy Kitine (PhD) ambaye aliongoza idara hii kwa miaka miwili toka mwaka 1978 hadi 1980. Kitine alichaguliwa kuongoza idara hiyo nyeti akiwa kijana wa miaka 36 tu. Anakumbukwa kwa jinsi alivyoiwezesha TISS kushirikiana na Idara ya Usalama na Utambuzi Jeshini (MI) Chini ya Meja Jenerali Tumainieli Kiwelu, kuiteka nyara ndege ya makomandoo kutoka Libya iliyokuja kumsaidia Idd Amin katika vita ya Kagera.

Mwaka 1980 Mwalimu Nyerere alimteua kijana mwingine mwenye miaka 35 Dr. Agustine Mahiga (PhD) - (Marehemu) ambaye alikuja kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na baadaye Waziri wa Sheria chini ya Hayati Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli - kuwa Kaimu Mkurugenzi mkuu wa TISS. Alikaimu nafasi hiyo hadi mwaka 1983, Nyerere alipomuondoa na kumteua Kaimu Balozi wa Tanzania (Minister Plenipotentiary) nchini Canada.

Baada ya Mahiga kwenda Canada, Mwalimu Nyerere alimteua Luteni Jenerali Imrani Kombe kuwa Mkurugenzi mkuu wa 5 wa TISS mwaka 1983. Nyerere alipong'atuka alimuacha Kombe kwenye idara hiyo na alidumu hadi mwaka 1995.

June 30 mwaka 1996 Jenerali Kombe aliuawa na Jeshi la polisi kwa madai kuwa walifananisha gari lake (Nissan Patrol) na gari iliyokua imeibiwa na mtuhumiwa Ernest Mushi maarufu kama "White".

Alimininiwa risasi 4 kifuani licha ya kushuka kwenye gari na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kusurrender. Askari waliohusika na mauaji hayo walihukumiwa kunyongwa lakini Rais Kikwete aliwapunguzia adhabu mwaka 2011. Bado kifo cha Jenerali Kombe kina maswali mengi kuliko majibu.

Baada ya Kombe kuuawa alifuata Kanali Apson Mwang'onda. Huyu aliteuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa 6 wa TISS ambaye aliongoza Idara hiyo hadi mwaka 2005 alipostaafu. Kanali Mwang'onda anasifiwa kwa kuifanyia marekebisho makubwa idara ya TISS ya kimfumo na kiutendaji. Ndiye aliyewezesha muswada uliounda sheria ya TISS mwaka 1996.

Mwaka 1980 Mwalimu Nyerere alifanyiwa jaribio kubwa la kutaka kupinduliwa na baadhi askari wa JWTZ (akina Tamin, McGhee na Kepteni Maganga) . Hili lilikua jaribio la 3 kubwa la kumpindua Nyerere, lakini ni jaribio la 7 katika orodha ukijumlisha na mengine madogo. Kanali Apson Mwang'onda akiwa Mkurugenzi wa ndani wa TISS (DOI) alifanikiwa kuzima jaribio hilo. Historia hii ilimuongezea sifa ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa TISS mwaka 1995.

Mwaka 2005 Rais Jakaya Kikwete alimteua Othman Rashid kuongoza Idara hiyo hadi mwaka 2016 alipostaafu. Othmna Rashid alikuwa Mkurugenzi wa 7 wa idara hiyo.

August 24 mwaka 2016 Rais John Magufuli alimteua Mchungaji Dr. Modestus Kipilimba (PhD) wa Kanisa la City Harvest Church la jijini Dar es Salaam kuwa Mkurugenzi Mkuu wa 8 wa TISS. Kabla ya uteuzi huo Kipilimba alikua Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya taifa (NIDA).

Mchungaji Dr. Kipilimba amedumu katika nafasi hiyo hadi September 12 mwaka 2019 alipotenguliwa uteuzi wake na nafasi yake kuchukuliwa na Kamishna wa Polisi CP Diwani Athumani Msuya.
Polen sana kwa kuwa na ubongo unaotafsir mada zao ni za kidin.


Siye wengine tunajifunza jambo kupitia wao.

DINI YAO WATAJUA WAO.
 
Kwa miaka 35 tangu uhuru hadi mwaka 1996 hakukuwa na sheria ya TISS?
Kwenye nchi zetu za Commonwealth Ilikuwa ni "Special Branch", chombo cha Ikulu. Pengine walikuwa na sheria zao huko ndani, lakini formally hakuna kokote ilikuwa inajulikana.
 
DSTV kuna mpaka Majambazi wa Silaha ambao huo ujambazi ni sehenu ya Kasi zao

Umewahi kupata kuelezwa namna Hayati Prof Nikas Mahinda aliekuwa Mbunge wa Morogoro alivyovamiwa na kuuawa nyumbani kwake?
Umenikumbusha hili tukio wakati limetokea lilizizima Morogoro ila sikuwa na utambuzi mkubwa. Naomba nikumbushe mkuu kama hutajali.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
CP Msuya amekuwa The worst DG to be, With all resources ila still Ameruhusu Amiri jeshi Mkuu kuondoka mikononi mwake, Ila pia interesting ni kuwa Vijana wa Zamani walikuwa so ambitious imagine Mahiga amekaimu Ukuu wa idara nyeti kabisa at 35 Age, Njoo kwa Kitine nae at 36, Ila kwa sasa kijana wa miaka 35 kumuamini ni Ngumu sana mana Mzee alijaribu kuwaamini watu kama Makonda,Sabaya na Hapi ila matokeo yake wote tumeyashuhudia
 
CP Msuya amekuwa The worst DG to be, With all resources ila still Ameruhusu amiri jeshi Mkuu kuondoka mikononi mwake, Ila pia interesting ni kuwa Vijana wa Zamani walikuwa so ambitious imagine Mahige amekaimu Ukuu wa idara nyeti kabisa at 35 Age, Njoo kwa Kitine nae at 36, Ila kwa sasa kijana wa miaka 35 kumuamini ni Ngumu sana mana Mzee alijaribu kuwaamini watu kama Makonda,Sabaya na Hapi ila matokeo yake wote tumeyashuhudia
Una uhakika? 😡😡🙄
 
CP Msuya amekuwa The worst DG to be, With all resources ila still Ameruhusu Amiri jeshi Mkuu kuondoka mikononi mwake, Ila pia interesting ni kuwa Vijana wa Zamani walikuwa so ambitious imagine Mahiga amekaimu Ukuu wa idara nyeti kabisa at 35 Age, Njoo kwa Kitine nae at 36, Ila kwa sasa kijana wa miaka 35 kumuamini ni Ngumu sana mana Mzee alijaribu kuwaamini watu kama Makonda,Sabaya na Hapi ila matokeo yake wote tumeyashuhudia
Kwa maneno mengine Msuya ndiye aliyemwua rais. Amefeli majukumu yake.
 
Ni hospitali iliyo chini ya idara ya usalama wa taifa, kama ilivyo Hospitali ya Lugalo kwa JWTZ na hospitali ya Kurasini Baracks kwa jeshi la polisi.

Imepewa jina la mzena kumuenzi mkurugenzi wake wa kwanza wa idara aliyeitwa Emilio Mzena
Hospital hiyo ipo wapi??
 
Kwa miaka 35 tangu uhuru hadi mwaka 1996 hakukuwa na sheria ya TISS?
Kimsingi TISS imeanzishwa wakati wa Mkapa.

Kabla ya hapo kulikuwa na "Kitengo Maalum" cha watu wasiojulikana kilichofanya kazi nje ya sheria kama sehemu ya Ikulu.

Nakumbuka kwa sababu hawa wengine ndugu zetu tulivyokuwa wadogo tulijua wanafanya kazi Ikulu tu.
 
Kwa maneno mengine Msuya ndiye aliyemwua rais. Amefeli majukumu yake.
Rais hataki kuvaa barakoa in the middle of a pandemic wakati ana matatizo ya moyo na mpaka wasaidizi wake wa karibu wanafariki kwa Covid-19.

Anawashushua wanaovaa barakoa, mpaka kanisani, hataki chanjo, hataki watu wapimwe. Hataki isolation.

Kapigwa daflao unamlaumu Msuya?

Hapa ni case ya "Mwana kulitafuta, mwana kulipata" tu.

Msuya anaweza kuwa na matatizo mengi, lakini kifo cha rais Magufuli alijitakia Magufuli mwenyewe kwa uzembe wake na ubishi wake wa kukataa sayansi, licha ya kuwa na Ph.D ya Chemistry, na kuendekeza propaganda za siasa.

Kwa kweli ukiangalia matatizo yake ya moyo, Magufuli hakutakiwa hata kugombea kazi yenye mikiki kama urais, kagombea urais kwa sababu ya uroho wake wa madaraka tu.

Sasa mtu kama huyo ambaye hashauriki wala hapangiwi, akifa, utamlaumu vipi Msuya?
 
Rais hataki kuvaa barakoa in the middle of a pandemic wakati ana matatizo ya moyo na mpaka wasaidizi wake wa kqribu wanafariki kwa Covid-19.

Anawashushua wanaovaa barakoa, mpaka kanisani, hataki chanjo, hataki watu wapimwe. Hataki isolation.

Kapigwa daflao unamlaumu Msuya?

Hapa ni case ya "Mwana kulitafuta, mwana kulipata" tu.

Msuya anaweza kuwa na matatizo mengi, lakini kifo cha rais Magufuli alijitakia Magufuli mwenyewe kwa uzembe wake na ubishi wake wa kukataa sayansi, licha ya kuwa na Ph.D ya Chemistry, na kuendekeza propaganda za siasa.

Kwa kweli ukiangalia matatizo yake ya moyo, Magufuli hakutakiwa hata kugombea kazi yenye mikiki kama urais, kagombea urais kwa sababu ya uroho wake wa madaraka tu.

Sasa mtu kama huyo ambaye hashauriki wala hapangiwi, akifa, utamlaumu vipi Msuya?
Yaani
 
Back
Top Bottom