Huyu dogo kaja kutafuta attention tu huku, anataka aonekane uzi wake una pages nyingi jinga sana.Utoto mwingi sana huu uzi
Baadhi ya mistariSaleh Jabir kutokana na uzi huu nadhani sio huyo unayemsema wewe,hapa amezungumziwa Saleh Jabir anayetambulika kama mwanzilishi wa kuimba wimbo wa kwanza au chache za mwanzoni za mtindo wa rap ambapo aliutohoa wimbo wa ice ice baby kwa kuchukua midundo (beat) naye kuweka maneno ya kiswahili,wakati huo huyo mtangazaji unayemsema alikuwa "mama nnya"
Bilnas anaimba mziki gan?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Sasa hilo ni tatizo la waandaji tuzo
Lakini nakwambia ukweli hata SUGU angekua kwenye hiyo category bado ningeona ni upuuzi tuu kama ww unavyo shangaa Bilnass kuingia kwenye tuzo hizo wakati hafanyi HIPHOP
Nembo ya taifa bongo records ingetumika,Kama ninge ..kama ningekuwa mimi star[emoji445]
Nahisi jina langu kila mtaa lingezagaa[emoji445]
Anzia ngazi Taifa, mpaka mkoa[emoji445]
Vibanda vya mamc katuni vyote ningebomoa[emoji445]
Jamaa alikuwa ananata na beats kali za majani pale bongo records
Huyu mwamba alikuwa na hits
Kama
Mnyalu
Nampenda ft nature
N.k
Huyu aliyetoa mada afungwe pingu apelekwe selo
Hivi hiii Style ya Jabali la Kampala. Jose inaitwajeeeMchizi Mox anasema kuwa Majani hakupenda vile jamaa anavyoimba kwa kukoroma, akamshauri abadili na kuimba kwa sauti ya kawaida, Mchizi Mox akakataa. Majani akafanikiwa kumbadilisha Jay Moe, huyu ndio akaanza kuimba hivi tulimvyomsikia katika nyimbo zake, ila nae awali alikuwa akitoa sauti ya kukoroma kama Mox.
Hata hivyo Majani hakuwahi kusema kuwa Mox hana kipaji, ila aliona kibiashara atazingua. Mtazamo aliokuwa nao Majani hata mimi nilikuwa nao wakati naanza kumsikia Jose Chameleon na ngoma yake Mama Mia. Niliona ni msanii mwenye sauti mbovu na hawezi kutoboa kumbe sikuwa sawa. Ilikuwa ni mtazamo wangu tu na sio kuwa jamaa hakua na kipaji, sasa the same goes kwa Mox et al
I need a doctor. Song langu la hip hop la muda woteeeeStill D.R.E ?. Ile ngoma yote iliandikwa na Jay Z. Ila biti lake ni next level.
Sugu moto chini ni bonge la dude hata likipigwa leoLakini nyimbo zake zinatoka Kama Sugu Moto chini..zilivuma kiasi chake
Huyu jamaa ni tahira wala usibishane nae yeye kambatiza 2 proud kua too proudNimeanza kumfatilia Sugu kabla hujazaliwa, na ushahidi nimekuwekea Sasa wewe leta ushahidi popote pale palipoandikwa TOO PROUD
JcB namuelewaga sana [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kuna hizi ngoma zake nazipendaKwenye list muongeze JCB wa watengwa na Joh Makini. Jcb bwana sijui kama alichokuwa anaimba ye mwenyewe anakijua au kama unaweza okota karatasi ya wimbo alioandika ukajua kama ni wimbo
Yaani La Moto Haswaaa [emoji95][emoji95]Sugu moto chini ni bonge la dude hata likipigwa leo
Sugu Moto Chini Ile Ngoma ni balaa na ni Alama ya hip-hop ya BongoYaani La Moto Haswaaa [emoji95][emoji95]
We hujui mziki aisee.Kalapina,
Huyu jamaa mbali na kuwa na harakati nyingi akiwa pamoja na kundi lake la Kikosi cha mizinga .ukweli ni kwamba hana kipaji cha music. Alipata umaarufu coz ametoka kipindi wasanii ni wachache
Sugu
Huyu jamaa ana majina kibao kama Mr two, jongwe, too proud na sasa anajiita Taita licha ya kuwa na heshima kama moja ya waasisi wa music wa hiphop tanzania , ukweli ni kwamba hana kipaji cha music
Jaffarai
Huyu ni moja ya member wa wateule alitamba na wimbo wa niko bize .lakini hakuweza kudumu kwenye game kwa muda mrefu kutokana ukweli hana kipaji
Mchizi mox
Huyu pia ni member mwingine wa wateule ngoma zake zilizowahi kupata airtime ni mambo vp na chupa nyingine . lakini uwezo wake ni wa kawaida sana
Mike tee mnyalu
Huyu jamaa alipata airtime miaka ya zamani kwa ngoma zake lakini ukimskiliza ni wazi hana uwezo kabisa. Ni moja kati ya wasanii ambao huwa wanaandikiwa
Soggydog hunter
Huyu jamaa bora angebaki kwenye u presenter tuu huku kwenye music aliforce tuu hana uwezo kabisa ana ngoma nyingi ila iliyopenya ni kibanda cha simu pekee yake
Bou nako
Huyu alikua member wa N2N lakini tangu hakua na uwezo kabisa .nafkir wana walimbeba tuu kutokana na love .ila kwenye music jamaa hana kipaji
Fido vato
Huyu member wa vatokoko soldiers ni empy kabisa , analazimisha fan tuu ila ukweli anaujua kuwa hana uwezo wowote ule zaidi ya kujikuta gangstar
Kr mulah
Huyu ndio founder wa style ya kucheza Mapanga . ameanza sanaa muda mrefu sana lakini ukimskiliza utagundua jamaa hana uwezo wowote kwenye music kwa kifupi hana kipaji
Mh temba
Huyu ni member wa TMK wanaume family mwanzoni alibahatisha ngoma kama tatu zikaenda mjini, baadaye akaja kuungana na chege wakatoa hadi album..ila ukimfuatilia vizur jamaa hana
uwezo kabisa
Rich one
Huyu pia ni member wa TMK alitamba na ngoma moja aliyomshirikisha Juma nature inaitwa hatuna kitu.baada ya hapo hajawai kutoa hitsong tena, Jamaa anasifika kwa utapeli wa kuandaa show na wasanii fake huko mkoani afu anapiga hela
Dudu baya
Huyu jamaa aliotea ngoma kama tatu tuu ambazo zilimtambulisha vyema kwenye game .lakini alipata jina kwakua kipindi anatoka hapakua na upinzani mkali kama ilivyo sasa
Dark master
Huyu ndo muhasisi wa Chamber squard Nampa heshima kubwa sana kwa kuweza kuiweka dodoma kwenye ramani ya muziki , Lakini tukiongelea uwezo binafsi .jamaa anauwezo wa kawaida sana
John mjema,
The late John mjema alitamba na wimbo wa wachumba 30. Na ngoma zingine alizofanya kwenye kundi lao aliokua na kina the late steve 2k na buibui .lakini tukimzungumzia binafsi kimuziki jamaa hana kipaji cha muziki
Maujanja suppliers
Hawa jamaa nawakubali kwa harakati zao za street lakini kwenye music watupishe hawana vipaji .lakini wao wamekua wanalalamika wanabaniwa kitu ambacho sio ukweli
Kama unafuatilia music wa bongo fleva utakua unakubaliana na mimi hawa jamaa hawana talent za music kabisa
JcB namuelewaga sana [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] kuna hizi ngoma zake nazipenda
Ukiskia Paah Orijino na Remix
Machochoro zote [emoji3][emoji3] ft Chaka
Bongo Fleva
Wanashangaa ft Jay Moe, Nakaaya (hii ngoma kali sana)
Halafu Kuna Zile Watengwa wote, Mashairi yake nayaelewa kwenye nyimbo kama
Africa
1 2 3 4
Rap si mchezo
Sio lazima
Tabia mbaya
Tunafanya
Tathmini ft Kikosi cha Mizinga
Narizika
Full iwe laana
Toka TZ A, TZ B mpaka C, sina hata TAXI.Kwenye list muongeze JCB wa watengwa na Joh Makini. Jcb bwana sijui kama alichokuwa anaimba ye mwenyewe anakijua au kama unaweza okota karatasi ya wimbo alioandika ukajua kama ni wimbo
Mwamba anachoangalia ni kutengeneza vina tu hata kama anachoimba hakieleweki😀😀Toka TZ A, TZ B mpaka C, sina hana TAXI.