Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

Tetesi: P Diddy ahusishwa na kifo cha Notorious B.I.G

KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO ? (4)
_______________

Inaendelea......

Kutokana na Tupac kuhitaji bosi wa Death Row, Marion 'Suge' Knight apambane kumtoa ndani ili waweze kufanya biashara pamoja, Suge aliangaika huku na huko mpaka kufanikiwa kumchomoa Tupac jela.

Kiasi cha Dola Milioni 1.4 kilitolewa na Suge hivyo kufanikiwa kumtoa jela Tupac mwaka 1995, achilia mbali Dola 15,000 ambazo Suge alizitoa kumsaidia 'kishkaji' Tupac wakati akiwa jela.

Kimsingi Suge alikubali kujipukutisha fedha kwa sababu alijua kumwandika Tupac mkataba wa kumsimamia kupitia Death Row Records italipa. Knight alijua nini anafanya kwenye makubaliano hayo.

Makubaliano ya Tupac na Suge yakawa mazuri. Tupac akakubali kutengeneza albamu 3 chini ya Death Row Records lakini muda wote akihitaji Suge awe upande wake kwenye vita vyake dhidi ya Biggie.

Nyimbo ya kwanza ya Tupac kuitoa chini ya Death Row Records ikawa California Love. Kombinesheni ya Tupac, Dr Dre na Roger Troutman kwenye chorus ukawa unyama wa kufa mtu. Kwa hakika "The King was back from Jail''.

Ujio wa California love ulimtikisa kila mtu. Tupac alikuwa amejerea kuusimika upya ufalme wake uliotishiwa kuondoshwa kwa mtutu wa bunduki na vijana kutoka Pwani ya Mashariki (East Coast).

Marion Suge Knight na Tupac Shakur wakafanikiwa 'kuupika' mgogoro wa East Coast na West Coast ukapikika, mgogoro ambao chimbuko lake haswa ni chuki baina ya wasanii wawili, Notorious Big na Tupac Shakur.

Matatizo binafsi ya Biggie na Tupac yakajikuta yakirithiwa na hata wengine 'yasiyowahusu'. Wasanii wa East na West wakaonekana kuchukiana katika kiwango kilichotisha kabisa.

Wakati mgogoro huu ukikua na kuzidisha uhasama kwa wasanii, Serikali mwanzo ilionekana kama kupuuza, lakini kadiri hali ilivyozidi kuwa mbaya na viongozi walilazimika kusema chochote.

Lakini kabla ya kusema chochote, huko nyuma Tupac alikuwa ameshaingia kwenye mgogoro mara kadhaa na serikali kutokana na misimamo yake, harakati zake na maisha yake.

Nyimbo zake kupitia albamu yake ya 2Pacalypse ziliichefua sana serikali. Tupac alizungumzia zaidi Siasa, Ubaguzi na umasikini katika namna ambayo ilionekana kama kuchochea chuki kwa raia.

Mshtuko mkubwa ulitokea baada ya kijana mmoja mdogo kumpiga risasi polisi na kumuua kisha baada ya kukamatwa na kuhojiwa akathibitisha kufanya hivyo baada ya kusikiliza albamu ya Tupac iitwayo 2Pacalypse.

Tukio hilo lilikuwa gumzo nchini Marekani. Aliyekuwa Makamu wa Rais wakati huo, Bw Dan Quayle akatangaza kupigwa marufuku kwa nyimbo za Tupac kusikilizwa kwenye Jamii ya wamarekani.

Bw. Quayle alisema Tupac ni msanii asiyefaa kabisa kusikilizwa. Nyimbo zake zimejaa chuki na kuchochea uovu kwenye jamii. Akaanzisha kampeni za kuhakikisha jamii inamchukia na haipati nafasi ya kumsikiliza Tupac.

Masikini Quayle hakuwa amejua kuwa wakati anasema hayo, Tupac alikuwa ameshaiteka sehemu kubwa ya jamii ya wamarekani kuliko anavyodhani. Mahojiano yake na MTV ya mwaka 1993 yamlitosha kabisa kumfanya asimjibu lolote.

"Siwezi kuitawala dunia wala siwezi kuubadilisha ulimwengu, bali nichoweza kufanya ni kutema cheche zitakazofanya bongo za watu kuibadilisha dunia"..hii ndiyo kazi yetu tunayopaswa kufanya, kuamsha mtu mwingine anayetutazama".

Tupac alikiambia kituo cha televisheni cha MTV mwaka 1993 katika moja kati ya mahojiano yake yanayoendelea kukumbukwa mpaka leo. Quayle alishindwa vibaya katika kampeni ya kumaliza Tupac, lakini inaelezwa alichangia mno kupromoti mauzo ya kazi zake bila ya yeye kujua.

Watu mashuhuri mbalimbali waliyataja maneno hayo machache ya Tupac kama maneno bora zaidi kuwahi kutolewa na mtu "asiyetegemewa" na wengi kusema hivyo. Wengi waliyatumia kama rejea kwenye maeneo yao mbalimbali.

"Inawezekana baadhi yetu tusiwe watu wa kuibadilisha dunia, lakini tunapaswa kujaribu kila wakati kushawishi mtu mwingine kuchukua hatua zitakazoweza kuibadili dunia".

Maneno haya ya Tupac hata kwangu binafsi bado yanaishi sana.!

Itaendelea........[emoji3578]

#Balozi
Boss hapa ungekuwaa muungwana kama ungeongeleaaa kile kibao cha Pac na N.W.A cha "https://jamii.app/JFUserGuide the Police"
 
Yaani watu wanaongea pumba tupu humu. Eti Tupac aliuawa na Serikali. Really? Kwa impact gani aliyokuwa nayo kuitetemesha Serikali? You are giving him too much credit. Nataka mtu aniwekee kauli au lyrics au vitendo vya Tupac ambavyo viliitetemesha Serikali mpaka itake kumuua.
Boss lile Song https://jamii.app/JFUserGuide the Police lililetaa Uhasama mkubwaa Mno kati ya Serikali na Wahuni wa Compton
 
Natamani naninyi mlete stori habari za B.I.G ingependeza
Ukute hata habari za Big mwenyewe hawazijui, yan mpaka waende kuokota mawili matatu kwenye vijiwe vya kahawa ndo waje kujaribu kutulisha matango pori kwa habari sijui za kusimuliwa na mjomba wake muuwaji wa Big 😂😂😂😂
 
Wewe huenda unabisha tu bila kujua unachobishia, au unajua ila umeamua tu kuleta ubishi ili isionekane kuwa umeshindwa.

Kitendo cha 2pac kuzaliwa na mwanamke aliekuwa member wa black panther peke yake tayari lilikuwa tishio kwa mfumo wa kibaguzi wa enzi zile. Hapo sijazungumzia yale aliyokuwa anaaongea mara kwa mara kuhusu ubaguzi wa rangi waliokuwa wanafanyiwa watu weusi kitu ambacho mamlaka hawakukipenda maana ni kama kilikuwa kinawavua nguo duniani. Na ikizingatiwa kuwa taifa hilo lilikuwa linajinasibu kuwa ni la kidemokrasia na linalopambana na ubaguzi mbali mbali.

Chuki hiyo ndio iliyopelekea kifo chake. Na sio yeye tu. Hata wale ambao wewe unaona kuwa sio tishio pia waliuwawa au kuuliwa hovyo barabarani.

RIP George Floyd na wengine waliouwawa hovyo. Ingekuwa watu hawaku record au kufuatilia vifo vyao. Basi majumba mabovu wangeangushiwa kina Orlando wengine au yale magenge ya kihalifu kama ilivyokuwa desturi yao.

Yani ungetengenezwa uongo uliopangwa rangi vizuri na leo hii ingekuwa mmoja wa wanaoamini kuwa watu hao waliuwana wenyewe kwa wenyewe.
Ndio maana nikasema kwamba assumptions zako ni za kijinga. Eti kwa kuwa Tupac alizaliwa na Afeni Shakur basi tayari Serikali inamchukulia kuwa ni rebel. Halafu hayo maneno aliyosema Pac mpaka Serikali ikatetemeka ni yapi? Mbona hamuyaweki hapa?

Mnataka kumuweka Tupac kwenye level moja na MLK, Malcolm X na Fred Hamptons. Kamwe hakuwa kwenye level hiyo.

George Floyd alikuwa victim wa Police brutality. Sijui hata anahusiana kivipi na huu mjadala. Dude, you are all over the place, hata hujui unataka kuongea nini.
 
Ndio maana nikasema kwamba assumptions zako ni za kijinga. Eti kwa kuwa Tupac alizaliwa na Afeni Shakur basi tayari Serikali inamchukulia kuwa ni rebel. Halafu hayo maneno aliyosema Pac mpaka Serikali ikatetemeka ni yapi? Mbona hamuyaweki hapa?

Mnataka kumuweka Tupac kwenye level moja na MLK, Malcolm X na Fred Hamptons. Kamwe hakuwa kwenye level hiyo.

George Floyd alikuwa victim wa Police brutality. Sijui hata anahusiana kivipi na huu mjadala. Dude, you are all over the place, hata hujui unataka kuongea nini.
Umeshamezeshwa uongo na mjomba wake Orlando, so ni vigumu sana mtu kukuelewesha hadi ukaelewa tunachojadili.
 
Tupate hii series naamini kuna mapya tutayaona View attachment 2569031
20230328_200408.jpg
 
KWANINI TUPAC ALIMCHUKIA SANA BIGGIE MPAKA KIFO.? (5)
_______________

Inaendelea......

Pamoja na Tupac kuishi maisha yaliyoonekana kuwachukiza baadhi ya watu kutokana na kuwa na vitendo vya ukorofi uliopitiliza lakini alipendwa mno.

Ilistaajabisha watu. Kwanini mtu anayehubiriwa kuwa mbaya mbele ya jamii, jamii husika ilimpenda mno.? Maisha yake bado yanagusa hisia za wengi hata sasa.

Ukiachana na uhuni uliopitiliza, Tupac alipendwa mno na mademu. Historia inaonesha aliwahi kuwa na uhusiano na mademu wengi walioonekana kujigonga wenyewe kwake.

Katika orodha hiyo, mastaa kadhaa wa muziki hawakukosekana. Lady Madonna anafungua orodha hii kwa kuwahi kuwa na uhusiano na Tupac kwa muda wa miezi 18.

Uhusiano na Madonna na Tupac uliripotiwa sana lakini wawili hao wakamwagana kwa Tupac kuhisi kuwa taswira yake ya 'ki-gangsta' inapotezwa kwa kuwa na mahusiano na mzungu.

Staa mwingine aliyeudandia mtumbwi wa vibwengo wa Tupac alikuwa ni Whitney Houston. Wengi walishangaa kusikia mume wa Whitney, Bobby Brown akilithibitisha jambo hilo pasina shaka.

Katika Documentary ya kumbukumbu zake iitwayo "Every Little Step", Bobby anaelezea kuwa alifahamu uhusiano wa Tupac na Whitney lakini alipuuza kwa sababu hayo yalifanyika huko nyuma.

Mastaa wengine waliokuwa na mahusiano na Tupac kwa vipindi tofauti tofauti ni pamoja na Aaliyah, Yo-Yo, Faith Evans, Rosie, Jada Pinkett, Janet Jackson, Kidada Jones nk.

Hili la Jada na Janet limekuwa na ukakasi kipindi chote kutokana na wao wenyewe kukanusha vikali, japo watu waliokuwa karibu na Tupac huwezi kuwaambia hivyo wakakuelewa.

Hata kama Janet na Jada hawakuwahi 'kuliwa' na Tupac, hiyo haiondoi kuwa walimpenda mno muhuni huyo. Tupac alipendwa sana na wasichana, naye aliwapenda mno.

Maisha ya Tupac yalijaa visa na mikasa mingi. Hii ni kwa sababu dunia haipendi kuambiwa ukweli. Tupac aliishi maisha ya kuelezea hisia zake bila mipaka, jambo hili lilimgharimu.

Alivutiwa mno na maisha ya Uhuni na Ujambazi (Thug Life) na kuamua kujifaharisha kwa hilo. Tattoo yake maarufu aliyoichora tumboni kwake ya "Thug Life" ilizusha maswali mara kadhaa kwa waandishi aliyoamua kuyajibu 'kiaina'.

"Naona wengi mnahoji sana kuhusu "Thug Life". Mimi na 'wanangu' Syke Stretch, Mopreme Shakur, The Rated R, Macadoshis na Kato tumeanzisha kundi la Hip Hop lenye jina hilo".

"T.H.U.G. L.I.F.E. ni kifupi cha "The-Hate-U-Give-Little-Infants-Fucks-Every". Na hiki kama kundi ndicho tunachomaanisha" alieleza Tupac. Kundi hili pia lilitoa albamu moja iliyoitwa "Thug Life".

Mbali ya kurap, Tupac alijaaliwa kipaji kikubwa cha Uigizaji. Drama ya kihalifu ya "Juice" aliyeigiza mwaka 1992 kama Roland Bishop, kijana mwenye shida mtaani anayegeuka na kuwa muuaji ilimpa umaarufu mkubwa.

Miaka miwili baadae akaigiza filamu ya "Above The Rim" kabla ya kuigiza kwenye "Poetic Justice" sambamba na Bibie Janet Jackson. Filamu hizi zinadhihirisha kipaji alichojaaliwa Tupac katika sanaa ya muziki na Uigizaji.

Itaendelea........[emoji3578]

#Balozi
 
Tupac alikuwa na hasira baada ya kutokea ugomvi baina yake na BIG kuhusu utunzi wa wimbo fulani, alikwenda kwenye vyombo vya habari na kuanza kujisifu kuwa amelala na Faith Evans mke wa BIG.

BIG akaona isiwe shida ammalize tu. Kundi la Tupac likaamua nalo lilipize kisasi na vijana wawili wadogo wakaondoka kiurahisi sana.

Faith Evans akatoa wimbo mmoja mkali sana wa kumkumbuka BIG chini ya uongozi wa P Didy....
Umeandika nini hiki?
 
Ukisoma huu Uzi watu wanatoa detail utafikiri walikuwa wana hang na 2pac huko Marekani.

Kumbe ni washamba fulani wapo hapo Yombo hata ndege hawajawahi kupanda.
 
Big aligundua kwamba Diddy alikuwa anamnyonya sana, kwahiyo alikuwa amepanga akimaliza mkataba wao anaachana nae kitu ambacho Diddy hakupendezewa nacho na pengine kuamua kufanya kile anachohisi mama yake na Big.

Baada ya kifo cha Big Diddy umaarufu wake uliongezeka maradufu na pesa ikawa nyingi kutokana na kuuza nyimbo nyingi za Big ambazo bado zilikuwa studio kwake.

Pia akawahi fasta fasta kutoa ule wimbo wa 'I'll be missing you" akiwa amememshirikisha Faith Evans (ex wa Big) Nyimbo ile moja tu peke yake ilimpa pesa nyingi ambayo kama Big asingefariki basi angekaa zaidi ya miaka 5 bila kuishika.

So kifo cha Big kimemnufaisha zaidi Puff kuliko kilivyoinufaisha familia yake Big.
Diddy mjasiriamali sana.

So story ya kuondoka kwenye label baada ya mkataba ni the same na PAC na Suge/deathrow.
 
He (
Pddy hawezi kumuu BIGGIE nakataa,kwenye gari alipokuwepo BIGGIE Kulikua na ndugu yake wa damu..

Eugene deal ambae ni bondia wa pddy(Mtoto wa kaka yake)
Lil cease mjomba wa B.I.G na member wa JUNIOR M.A.F.I.A wote walifia humo..

Pddy ndio power control kwenye kesi ya SUGE Na anamchomekea kweli,halafu mwezi uliopita mama yake B.I.G Alikutana na SUGE mahakamani na wakati anarudishwa jela waliondoka pamoja..

BEEF YA SUGE KNIGHT NA P.DIDDY HAIWEZI KUISHA

Hamna lolote brother. Huyo mama anataka hela tuu hana lolote.

Puffy juzi kat8 hapa ameamua kuwamilikisha "master recording" wasanii wake wote including BIG mother ambae ni mrithi wa BIG na amekubali hilo deal kwa makubaliano toka Bad Boy records.

Pia Suge hana lolote he's in jail serving 23 years with possible parole in 2034. Na Death Row records ameshainunua Snoop akijua kwamba ubabe na umafia wa Suge uliisha mahakamani.
 
2pac aliwaibia sana ma nigger wa pandee zileee. Ila ki ukweli jamaa alikuwa miyeyushoo sana kama angekuwa kipindi Kuna social network asingeweza kuwashika masikio kiasi kilee.. Pac kengee sana

Yaan matatizo anatafuta mwenyewe alafu ananza kulaum watu wengine shida zikimkuta.
 
Back
Top Bottom