Padri wa Kanisa Katoliki aliyefukuzwa afunguka

Padri wa Kanisa Katoliki aliyefukuzwa afunguka

Wakati Padre Christopher Fosudo aliyefukuzwa na Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam akitarajia kuondoka nchini hivi karibuni, Jeshi la Uhamiaji limesema halina tatizo naye.

Agosti 17, 2022, Katibu wa Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Vicent Mpwaji alituma barua kwa mapadri wote jimboni humo akiwataarifu kufukuzwa kwa Padre Fosudo.

Padri huyo alikuwa paroko msaidizi wa Parokia ya Watakatifu Mashahidi wa Uganda, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kwenye barua hiyo, Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi hakueleza sababu za uamuzi huo wa kufukuza.

“Askofu mkuu wa Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi OFMCap anatoa taarifa kwamba Padre Christopher Fosudo kutoka Nigeria ambaye alikuwa anahudumu hapa jimboni kama paroko msaidizi wa Parokia ya Magomeni hatakiwi tena kuwepo jimboni Dar es Salaam. Hivyo, askofu mkuu amemuagiza Padre Fosudo arudi nchini kwake Nigeria,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Taarifa za kufukuzwa kwa padre huyo aliyewahi kuhudumu Jimbo Kuu la Dodoma, Kanisa Kuu la Mtatifu Paulo wa Msalaba na parokia tofauti za Jimbo Kuu la Dar es Salaam ikiwamo ya Mtakatifu Padre Pio ya Tabata Kisiniwa, zilisambaa mitandaoni na kuibua mijadala miongoni mwa waumini.

Kati ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa ni kwa nini amefukuzwa na kwa sasa yupo wapi hivyo gazeti hili jana lilizungunza na Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Dar es Saalaam, Peter Mwita na Padri Fosudo na kuhusu suala suala hilo.

Mwita ambaye ni kamisha msaidizi mwandamizi wa Uhamiaji alisema baada ya taarifa za kufukuzwa kusambaa mitandaoni walimtafuta ili wamjue ni mtu huyo.

Baada ya kuzungumza naye, alisema “Tulibaini yupo nchini kihalali na hana kosa lolote wala taarifa yoyote ya uvunjifu wa usalama na kwa sababu hiyo, sisi kama Jeshi la Uhamiaji hatujaona sababu za kushiriki kumfukuza.”

Akifafanua kilichowashawishi kumtafuta, Mwita alisema walitaka kujua kama yupo nchini kihalali na walipojiridhisha walimwacha aendelee na shughuli zake kwani hakuna aliyetoa taarifa mbaya kumhusu.

Alisema padri huyo aliwaeleza kilichotokea kuwa ni masuala ya ndani ya kanisa hilo: “na si uvunjifu wa amani. Tumewaachia wenyewe kama kanisa kuona watafanya nini.”

Aidha, alisema padri huyo “anasoma PhD katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na alifuata taratibu zote za kisheria na kupewa kibali cha ‘student visa.’ Ili upewe kuna taratibu ambazo alizifuata na kupewa na masomo yake bado hajamaliza.”

Mwananchi pia ilizungumza na Padri Fosudo aliyesema alipoiona taarifa ya kutotakiwa jimboni alishituka na alipohojiwa na Uhamiaji aliambiwa aendelee na shughuli zake.

Alipoulizwa ataendelea na masomo au ataondoka, padri huyo alisema “nimeamua nitakwenda nyumbani, kuna mazungumzo na Baba Askofu nyumbani (Nigeria). Katika mazingira haya siwezi kubaki. Nitakwenda kuzungumza na Baba Askofu yeye ndiye ataamua nirudi au niende wapi.”

Akijibu anatarajia kuondoka lini, alisema: “siku chache zijazo kwa sababu katika mazingira haya, si vizuri kuendelea kukaa bila amani. Nitakata tiketi ya kurudi nyumbani.”

Katika mazungumzo yake na gazeti hili, padri huyo hakutaka kuweka wazi sababu za yeye kufukuzwa akisema: “Si vizuri kuyaweka kwenye magazeti yaliyotokea. Lakini, Watanzania ni watu wema sana.”

Padri huyo alikuja nchini kwa mara ya kwanza mwaka 2014 na kufundisha Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordan kilichopo mkoani Morogoro hadi mwaka 2016 aliporudi Nigeria kisha akaja tena kwa masomo mwaka 2017/18 anayoendelea nayo mpaka sasa.

Padre huyo alisema atakapozungumza askofu wa jimbo lake ataamua ama kurejea nchini kuendelea na masomo au kusoma kwa njia ya mtandao.

Agosti 18 ikiwa siku moja tangu barua itoke na kusambaa, gazeti hili lilizungumza na Askofu Mkuu Ruwai’chi kutaka kujua sababu za kumfukuza padri huyo ambapo alisema haawezi. “Mimi nimepeleka ujumbe kwa mapadre,” alisema.

Utaratibu wa kisheria
Kwa mujibu wa Sheria za Kanisa Katoliki (Canon Law), kuna makundi tofauti ya mapadre kulingana na karama zao. Wengine ni wa jimbo, watawa wa ndani au wengine ni wamisionarii wanaoishi katika jumuiya za kitawa.

Chini ya sheria hizo, padre anaweza kufanya kazi katika jimbo au eneo lingine kwa mkataba maalumu. Muda wote mapadre huongozwa na nadhiri za utii, useja na ufukara (wale walio watawa), huku wa jimbo wakiongozwa na utii kwa askofu na useja.

Sheria za Kanisa Na. 1341-1356 zinaainisha adhabu zinazoweza kutolewa kwa waumini wote wakiwamo mapadre na walei pindi wakikosea.

Waziri wa Sheria na Katiba amepewa mamlaka kupitia Kifungu cha 14(1) cha Sheria ya Uhamiaji ya mwaka 1995, kumwondoa nchini mtu yeyote ambaye si Mtanzania baada ya kuthibitika kutenda kosa linalovunja sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kuwa Padre Fosudo hana hatia yoyote ya kisheria, wataalamu wa masuala ya sheria wanasema hawezi kuondolewa nchini (deportation) kwani ametofautiana tu na mwajiri wake.

Source: MWANANCHI
ni wivu tu....
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa

All animals are equal, but some animals are more equal than others.​

 
Ninyi mmeshindwa kuchunguza hicho kisa mkatuletea hiyo habari hapa?
 
Romani Catholic imejengwa katika misingi ya utii wa hali ya juu. Kamwe, si padri Fosudo au askofu atakayefunguka kuhusu sababu za kufukuzwa.

Ila assumptions za kuadhibiwa mapadri wa Roman Catholic huwa ni uzinzi wa wazi wazi, na wizi wa fedha za kanisa uliopindukia. Padri akiwa anachukua fedha kidogo kujihudumia yeye anavumiliwa tu.

Pia, kosa lingine kubwa kabisa ambalo padri wa roman catholic atafukuzwa kutoka kanisani, ni pale atakapoanza kuombea waumini mapepo na kuanguka kama wanavyofanya kina Mwamposa. Sijajua kwa nini roman catholic hawataki kibisa mapadri kuombea watu mapepo.
Wapo mapadre na waumini wengi tu ambao wanaombea na kutoa pepo,ila mpaka kanisa lijiridhishe kuwa unafanya kwa nguvu za kiMungu na sio utapeli.
 
Mpaka ukiona Askofu ametoa huo waraka, basi ujue huyo Padre amefanya kosa ambalo halivumiliki kwa mujibu wa sheria na taratibu za Kanisa.

Hivyo arudi tu nchini kwao. Maana hakuna namna. Sisi wengine tuliona bora tuondoke huko mapema. Maisha ya kuishi kama mseja, fukara, mtii kwa Askofu! Nani angeyaweza. Bora nibakie tu kuwa Mlei muaninifu kwa Kanisa.
Mkuu mimi huwa najiuliza mapadre wanalipwa mshahara ? na pia kuna hawa wengine mtu unakuta ni padre bado pia anafanya kazi serikalini madaktari, walimu na Fani mbalimbali malipo yao yanakuaje ? Analipwa mara mbili ?
 
Wakati Padre Christopher Fosudo aliyefukuzwa na Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam akitarajia kuondoka nchini hivi karibuni, Jeshi la Uhamiaji limesema halina tatizo naye.

Agosti 17, 2022, Katibu wa Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Padri Vicent Mpwaji alituma barua kwa mapadri wote jimboni humo akiwataarifu kufukuzwa kwa Padre Fosudo.

Padri huyo alikuwa paroko msaidizi wa Parokia ya Watakatifu Mashahidi wa Uganda, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kwenye barua hiyo, Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi hakueleza sababu za uamuzi huo wa kufukuza.

“Askofu mkuu wa Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi OFMCap anatoa taarifa kwamba Padre Christopher Fosudo kutoka Nigeria ambaye alikuwa anahudumu hapa jimboni kama paroko msaidizi wa Parokia ya Magomeni hatakiwi tena kuwepo jimboni Dar es Salaam. Hivyo, askofu mkuu amemuagiza Padre Fosudo arudi nchini kwake Nigeria,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Taarifa za kufukuzwa kwa padre huyo aliyewahi kuhudumu Jimbo Kuu la Dodoma, Kanisa Kuu la Mtatifu Paulo wa Msalaba na parokia tofauti za Jimbo Kuu la Dar es Salaam ikiwamo ya Mtakatifu Padre Pio ya Tabata Kisiniwa, zilisambaa mitandaoni na kuibua mijadala miongoni mwa waumini.

Kati ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa ni kwa nini amefukuzwa na kwa sasa yupo wapi hivyo gazeti hili jana lilizungunza na Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Dar es Saalaam, Peter Mwita na Padri Fosudo na kuhusu suala suala hilo.

Mwita ambaye ni kamisha msaidizi mwandamizi wa Uhamiaji alisema baada ya taarifa za kufukuzwa kusambaa mitandaoni walimtafuta ili wamjue ni mtu huyo.

Baada ya kuzungumza naye, alisema “Tulibaini yupo nchini kihalali na hana kosa lolote wala taarifa yoyote ya uvunjifu wa usalama na kwa sababu hiyo, sisi kama Jeshi la Uhamiaji hatujaona sababu za kushiriki kumfukuza.”

Akifafanua kilichowashawishi kumtafuta, Mwita alisema walitaka kujua kama yupo nchini kihalali na walipojiridhisha walimwacha aendelee na shughuli zake kwani hakuna aliyetoa taarifa mbaya kumhusu.

Alisema padri huyo aliwaeleza kilichotokea kuwa ni masuala ya ndani ya kanisa hilo: “na si uvunjifu wa amani. Tumewaachia wenyewe kama kanisa kuona watafanya nini.”

Aidha, alisema padri huyo “anasoma PhD katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na alifuata taratibu zote za kisheria na kupewa kibali cha ‘student visa.’ Ili upewe kuna taratibu ambazo alizifuata na kupewa na masomo yake bado hajamaliza.”

Mwananchi pia ilizungumza na Padri Fosudo aliyesema alipoiona taarifa ya kutotakiwa jimboni alishituka na alipohojiwa na Uhamiaji aliambiwa aendelee na shughuli zake.

Alipoulizwa ataendelea na masomo au ataondoka, padri huyo alisema “nimeamua nitakwenda nyumbani, kuna mazungumzo na Baba Askofu nyumbani (Nigeria). Katika mazingira haya siwezi kubaki. Nitakwenda kuzungumza na Baba Askofu yeye ndiye ataamua nirudi au niende wapi.”

Akijibu anatarajia kuondoka lini, alisema: “siku chache zijazo kwa sababu katika mazingira haya, si vizuri kuendelea kukaa bila amani. Nitakata tiketi ya kurudi nyumbani.”

Katika mazungumzo yake na gazeti hili, padri huyo hakutaka kuweka wazi sababu za yeye kufukuzwa akisema: “Si vizuri kuyaweka kwenye magazeti yaliyotokea. Lakini, Watanzania ni watu wema sana.”

Padri huyo alikuja nchini kwa mara ya kwanza mwaka 2014 na kufundisha Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordan kilichopo mkoani Morogoro hadi mwaka 2016 aliporudi Nigeria kisha akaja tena kwa masomo mwaka 2017/18 anayoendelea nayo mpaka sasa.

Padre huyo alisema atakapozungumza askofu wa jimbo lake ataamua ama kurejea nchini kuendelea na masomo au kusoma kwa njia ya mtandao.

Agosti 18 ikiwa siku moja tangu barua itoke na kusambaa, gazeti hili lilizungumza na Askofu Mkuu Ruwai’chi kutaka kujua sababu za kumfukuza padri huyo ambapo alisema haawezi. “Mimi nimepeleka ujumbe kwa mapadre,” alisema.

Utaratibu wa kisheria
Kwa mujibu wa Sheria za Kanisa Katoliki (Canon Law), kuna makundi tofauti ya mapadre kulingana na karama zao. Wengine ni wa jimbo, watawa wa ndani au wengine ni wamisionarii wanaoishi katika jumuiya za kitawa.

Chini ya sheria hizo, padre anaweza kufanya kazi katika jimbo au eneo lingine kwa mkataba maalumu. Muda wote mapadre huongozwa na nadhiri za utii, useja na ufukara (wale walio watawa), huku wa jimbo wakiongozwa na utii kwa askofu na useja.

Sheria za Kanisa Na. 1341-1356 zinaainisha adhabu zinazoweza kutolewa kwa waumini wote wakiwamo mapadre na walei pindi wakikosea.

Waziri wa Sheria na Katiba amepewa mamlaka kupitia Kifungu cha 14(1) cha Sheria ya Uhamiaji ya mwaka 1995, kumwondoa nchini mtu yeyote ambaye si Mtanzania baada ya kuthibitika kutenda kosa linalovunja sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kuwa Padre Fosudo hana hatia yoyote ya kisheria, wataalamu wa masuala ya sheria wanasema hawezi kuondolewa nchini (deportation) kwani ametofautiana tu na mwajiri wake.

Source: MWANANCHI
Hakuna cha ajabu hapo. Kufanya kazi kwa Padre nchini kunahitaji vitu viwili: Mwajiri (yaani Kanisa) aseme anamhitaji na aridhike na sifa zake; na Uhamiaji waridhike kwamba mhusika hana tatizo la kiusalama nchini. Kwa Padre huyu, mwajiri ameona kasoro zimejitokeza za kiutendaji, ambazo hana ridhaa za kuutangazia umma, mbali na kumwambia mhusika. Hivyo, mwajiri ameamua aachane naye. Kwa upande mwingine, Uhamiaji hawajaona dosari za kiusalama za mhusika. Hivyo, hawana sababu za kumuondoa nchini.

Kanisa linaweza kuridhika na Padre mmoja lakini Uhamiaji wakagundua huyo ni CIA, kwa mfano, wakamnyima kibali cha kufanya kazi nchini. Padre huyo atafukuzwa nchini. Ni pale tu vyombo vyote viwili vinaporidhika kwa pamoja ndipo Padre atafanya kazi nchini.
 
Rc mmetisha,mpaka sasa wabongo hatujajua kosa lake? Nyie ndo mnapaswa kuwa usalama wa taifa.
Kwani mtumishi wa umma akifukuzwa kazi na mwajiri wake Taifa hutangaziwa kwamba amefanya kosa kadhaa? Kwa nini ulidai Kanisa litangaze kosa la Padre huyu? Kwanza, hiyo itakuwa kukiuka haki zake, na anaweza hata kwenda mahakamani kwa kudhalilishwa.
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa
Nimeshasikia sn hii kitu mkuu!! Ni yule binti mwenye pacha wake ambaye alimuweka maabara pale dispensary kwake epiphany au huyo unae mzungumzia ni mwingin?
 
Mkuu mimi huwa najiuliza mapadre wanalipwa mshahara ? na pia kuna hawa wengine mtu unakuta ni padre bado pia anafanya kazi serikalini madaktari, walimu na Fani mbalimbali malipo yao yanakuaje ? Analipwa mara mbili ?
Huwa wanapewa posho ya mwaka mzima. Miaka ya 1990's wakati nasoma kwenye shule zao, walikua wanapewa posho ya Tsh. Milioni 1.5 hivi kwa mwaka. Na kwa kipindi kile, ilikuwa si haba. Sijui kwa sasa wanapewa kiasi gani.

Kuhusu hao Mapadre/Watawa Madaktari, walimu na wale wenye fani mbalimbali; utaratibu ulivyo ni kwamba mali zote wanazomiliki ni za Kanisa! Hivyo hata hiyo mishahara yao inatakiwa iingie kwenye mfuko wa Kanisa!

Ingawa kuna baadhi yao huwa wanajiongeza kwa kuanzisha miradi mbalimbali. Maana baadhi wana familia zinazo wategemea.
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa
Ndugu, acha majungu. Kama una ushahidi, uliufikisha kwenye Baraza la Parokia; au kwa Paroko; au kwa Askofu? Njia zote hizo ziko wazi kusikiliza tuhuma hizo. Ninaongea hivyo kwa kufahamu mambo yaendavyo kikanisa kwa kuwa nimefanya kwenye mabaraza ya Parokia nchi tatu tofauti.
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa
Wewe umepuyanga kwenye hiki ulichoandika. Unaonekana una matatizo makubwa sana, jitathmini ndugu
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa
Hebu utoe huo ushahidi unaousema hapa jukwaani
 
K

Ila hawa Roma huwa siwaelewi kuna mapadri wanao adhiniwa kwa makosa ambayo wengine hawaadhiniwi mfano Padri Bayo wa Jimbo la Pwani Bagamoyo ushahidi wa wazi kabisa upo amezaa na mfanyakazi wake watoto 2 lakini anasalisha na hakuna hatua yoyote alichukuliwa
Jimbo la Pwani linapatikana nchi gani
 
Ndugu, acha majungu. Kama una ushahidi, uliufikisha kwenye Baraza la Parokia; au kwa Paroko; au kwa Askofu? Njia zote hizo ziko wazi kusikiliza tuhuma hizo. Ninaongea hivyo kwa kufahamu mambo yaendavyo kikanisa kwa kuwa nimefanya kwenye mabaraza ya Parokia nchi tatu tofauti.
Ila hili suala la baadhi ya Mapadre/Maaskofu wa Kanisa Katoliki kuwa na watoto, aisee siyo majungu! Hili jambo lipo!

Mimi nimeishi kwa miaka mingi Wilaya ya Kilombero na Ulanga! Kule Majimbo Katoliki mawili ya Mahenge na Ifakara! Kiukweli kuna idadi kubwa sana ya Mapadre wenye watoto! Kuna Pandre mmoja alikuwa na watoto wawili aliozaa na mwalimu wa sekondari! Kuna mwingine alikuwa na watoto 4!

Na wanatumia jina la ukoo wake, na la mdogo wake! Lakini wananchi/waumini wanaona kila kinacho endelea! Amemjengea huyo mwanamke nyumba, na kumfungulia biashara!

Kwangu mimi kama Mkatoliki, natamani kuona Mapadre/Watawa wakipewa uhuru wa kuoa/kuolewa! Ili kupunguza haya mateso ya useja kwa binadamu walio kamilika.
 
Mkuu mimi huwa najiuliza mapadre wanalipwa mshahara ? na pia kuna hawa wengine mtu unakuta ni padre bado pia anafanya kazi serikalini madaktari, walimu na Fani mbalimbali malipo yao yanakuaje ? Analipwa mara mbili ?
Hapokei mshahara,mshahara wake unaingia shirikani kwake au jimboni kwake .Yeye anapewa na shirika hela ya matumizi.Nyingine zinatumika shirikani kwa shughuli za shirika kama matumizi kwa wote na miradi mbalimbali kama mashule hospitali na kusaidia wahitaji

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom