Paji la uso na siri ya jicho la tatu

Paji la uso na siri ya jicho la tatu

Kuna kitu nimeanza kukielewa hapo hasa nilivyosoma hicho kitabu cha KUTOKA 13:16 kwenye Biblia.

Ngoja tuanze sasa kufukunyua nondo za huu uzi taratibu.

Ipi ni athari ya kulala chali, na kwa nini watawala wengi wa zamani walikuwa hawalali kifudi fudi??

Ukiangaliakumbu kumbu za mafarao wa misri walikuwa wanawekewa kabisa mto wa kulaliaambao ulikuwa hauwaruhusu kugeuza vichwa wakati wa kulala, na wote walikuwa wanalala chali.

Kuna siri gani hapa.??
Na hata mtu akifa kwenye jeneza kuzikwa ni chali
 
[emoji120][emoji120][emoji120]

Jr[emoji769]
Mkuu hv inakuaje 'mm hua na mazoea ya kulala na ubavu, lakini nkiota ndoto hususan naotaga ndoto za kukimbizwa, nikishtuka najikuta nimelala chali alafu nmekunja miguu'
Ebu nsaidie ktk hilo kwa niaba ya wote ambao hii hali inawakumba wao au watu wao wa karibu
Ahsante
 
Mkuu hv inakuaje 'mm hua na mazoea ya kulala na ubavu, lakini nkiota ndoto hususan naotaga ndoto za kukimbizwa, nikishtuka najikuta nimelala chali alafu nmekunja miguu'
Ebu nsaidie ktk hilo kwa niaba ya wote ambao hii hali inawakumba wao au watu wao wa karibu
Ahsante
Isome tena mada kule juu nimelijibu hili
 
f6e63668ac1c4a88887ca94b0bd11c01.jpg


Hutaamini utakachogundua hapa kuhusu paji lako la uso...hapa ndio asili ya neno kipaji ilipatikana..hapa napo ni lango hapa ndio penye njia ya kuingilia mlango wa sita baada ya ile mitano. Hili ni jicho la ndani jicho lisioonekana.lango kuu la kiroho.

Tutaenda kwa mitazamo yote ya kidini na kiimani, kisayansi, kihisia na hata kwenye nguvu za giza.

1. Third Eye - Thalamus - Eye of Horus
c028b8f6365bdd2fb44aaf6796fdf17f.jpg


Hapa ni kwa mtazamo wa kisayansi nafikiri ni kwenye somo la anatomy kuhusu ubongo, jicho la tatu linaonekana katikati ya ubongo (zingatia katikati) vertebrate brain hapo ndio zinapozalishwa homoni za kulaza au kuamsha hisia maono usingizi nk.

2. Mathematics
22f4856d4325c03356542c3c19a96824.jpg


Katika ulimwengu wa mahesabu na hesabu, wanamahesabu kwenye ishu za ratio cos na tan watatusaidia hapa.

3. Tahjud (Meditation)
1a3f1076a0eecca2d21fb8771039a216.gif


Kwenye tahajudi wale waliosoma chakra na habari za milango nane, ukiangalia vizuri huo mchoro chakra ya sita ndio ya kuingilia mlango wa sita wa fahamu.

4. Baptism & Sijda
b23bbe047b4fed53bc8acd968bfbde9f.jpg
7581aaa5dd84dc3d74104360bf95c259.jpg


Kiimani katika ukristo, kwenye ubatizo alama ya msalaba kwenye paji la uso ndio hukamilisha tendo na kuwa Mkristo kamili sasa.. Lakini pia ukisoma kitabu cha ufunuo na habari za kutiwa Muhuri katika paji la uso utafahamu zaidi..

Kwenye Uislam tunajua nini maana na umuhimu wa swala tano na kuthibitisha uchaji wako katika swala tano ni sigida kwenye paji la uso.

5. A kiss on the Forehead
95e4888b95b1f04ef937618e752fd13d.jpg


Kwenye mahusiano busu kwenye paji la uso ni tofauti kabisa na mabusu ya sehemu nyingine yoyote.

6. FREEMASONRY
2eaa591e515e975051f9640238953750.jpg

Kwenye imani za mpinga Kristo freemason satanism nk alama yao kubwa ni jicho la tatu

7. SEVERE PUNISHMENTS (WATERBOARD)
8654ca9f3d106b3012aa7228ab664632.jpg


Kwenye adhabu na mateso mbalimbali paji la uso hutumika kuleta adha ya ajabu mwilini... Mateso ya water board ni mfano mmojawapo. Unalazwa chini unafunikwa kitambaa usoni kisha unamwagiwa maji.. Ni aina ya adhabu isiyoumiza mwili bali inayoumiza hisia.

8. Michezoni:
Kwenye mchezo wa ngumi alama za juu ni zile ambazo zinaangukia kwenye paji la uso.

Nimejaribu kwenda na picha kuokoa ufafanuzi wa maneno mengi... Tunaishi kwenye ulimwengu wa ajabu mno.. Tunashiriki kitu hicho hicho lakini kwa maana matumizi na mitizamo tofauti. Tunafundishwa kutolala chali kuepuka ndoto za mauzauza na majinamizi kumbe siri ni jicho la tatu jicho la maono.

Manabii na watenda miujiza hupenda kuwapuliza ama kuwashika watu penye paji la uso na kifuatacho hapo ni mzinga kama si kupiga kelele... Baadhi ya tiba mbadala hutumia paji la uso kama lango la uponyaji.

Wahindi na wahindu kwenye imani zao hujipaka rangi katikati ya macho kama sehemu ya ibada nk.

Jaribu kutafakari kwa hatua hiki kinachoitwa jicho la tatu, paji la uso, imani yako na maisha yako ya kila siku... Mwishowe tunaweza kujikuta tunaabudu paji la uso kwa muktadha tusiojua.

Mkuu naomba kuuliza

Nivibaya kutumia hilo jicho la tatu??

Je? Kuna madhara yoyote ukitumia jicho la tatu?

Je? Kunafaida gani ukitumia jicho la tatu??

👀👁
 
Mkuu naomba kuuliza

Nivibaya kutumia hilo jicho la tatu??

Je? Kuna madhara yoyote ukitumia jicho la tatu?

Je? Kunafaida gani ukitumia jicho la tatu??

[emoji102][emoji872]
Ni vizuri kulitumia hasa positively... Hawa wanaojiita waganga na manabii wengi wana posess half of it
 
Back
Top Bottom