Pale Bungeni simuoni Mbunge wa kuichambua ripoti ya CAG baada ya kukosekana Zitto Kabwe na wabunge wa CHADEMA

Ripoti yenyewe bado imefichwa, Prof. ASAD pekee ndo aliyeonyesha ethics za auditing procedures based on independent basis, kazi ya ukaguzi haitakiwi kuingiliwa ata kidogoo
 
Tukiweka itikadi pembeni, kiukweli pale bungeni simuoni mtu mwenye uwezo wa kuichambua ripoti ya CAG kama walivyokuwa Zitto Kabwe, J J Mnyika, James Mbatia na Tundu Lissu...
Leo ndo mmejua haya jamani?

Duh
 
Kwenye post zako huwa nikiingia na hasa pale unaponicot hupenda kuniita "Bwashee" ila sikuzote huwa nakupotezea sababu nakuona mnaa kama wengine...
Johnthebaptist ni mzima hasa ila wakati fulani huwa anaamua kujitia wazimu ili kunogesha baraza.

Siyo vizuri kumsema marehemu, lakini kwa kweli huwa siamini kama alikuwa mzalendo wa kweli. Mzalendo wa kweli kabisa hawezi kudharau maamuzi ua wananchi halafu akajipachikia wawakilishi wa kwake, halafu akawaita ni wawakilishi wa wananchi. Tena wengi aliowapachika na hamnazo, ni watupu vichwani kuanzia akili mpaka maarifa.

Amlaze pema peponi. Uovu aliolitendea Taifa tunausamehe, mazuri aliyoyatenda tutaendelea kuyaenzi.

Mheshima Rais Samia, tunaomba hekima ya Mungu itembee nawe, safisha uchafu mwingi uliomo ndani ya nyumba Tanzania. Kuna takataka nyingi. Kuna takataka za ukabila, ukanda, uchama, undugu, na ufisadi kwa waliokuwa wameruhusiwa. Nyumba imejaa nyufa na matindu mengi. Kuna kuta itabidi matundu yake uyazibe, lakini kuna kuta nyingine za kubomoa na kujenga upya.
 
Huyu muda mwingine akili zinakua sawa tofauti na yule Wakudadavuwa na jingalao
Johnthebaptist hastahili hata kulinganishwa na jingalao, wakudadavua, bia yetu na USSR. John hata akiamua kuandika ujinga, unaona kabisa kaamua kujifanya mjinga. Lakini hao wengine unaona kabisa kuwa ni wajinga na wanafiki.
 
Gwajiboy na Ripoti ya CAG wapi na wapi, nayeye amezoea kukariri vifungu vyamathayo ili ale kondoo kwa wepesi
 
Bwashee acha dharau; Babu Tale yupo, Kibajaji yupo, FA yupo, Msukuma ypo, Deo sanga ypo...hao wote watalisaidia Taifa kuichambua report.
 
mungu mtu wenu sindio alivyokuwa anataka kila ujinga atakaopeleka kule ukubalike

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Yaani Wote waliopelekwa kwa Mbelekeko....hawaamini Mbelekeko imekatika. Naamini hata Mjengoni watakua wanatetemeka sana...!!
 
Ukweli mchungu, kibajaji atakwambia anaweza kwani anauzoefu wa kumsikiliza zito kwa miaka kadhaa, vipi wale kovid 19 nao hawawezi?
 
Ukweli mchungu, kibajaji atakwambia anaweza kwani anauzoefu wa kumsikiliza zito kwa miaka kadhaa, vipi wale kovid 19 nao hawawezi?
Halafu CAG baada ya hayo akiwaita dhaifu watakimbilia kumuita kamati ya maadili na biti kali toka kwa spika kuwa asipofika atafuatwa kwa pingu.
Yaani Prof Assad hadi kesho inaniuma jamaa alikuwa jembe na hapepesi macho, alivyotolewa nikaanza kupata mashaka na uzalendo marehemu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…