Pale mke anapofungwa miaka 30 jela na hurusiwi kuongeza mke, hii hali inatatuliwa vipi?

Pale mke anapofungwa miaka 30 jela na hurusiwi kuongeza mke, hii hali inatatuliwa vipi?

Si kweli unayoyasemea kwa Ukatoliki. Vigezo vitatu vinahitajika kwa ndoa kutambuliwa katika Kanisa Katoliki:
1. Ndoa iwe kati ya mwanamme na mwanamke.
2. Ndoa ifungwe (iwe 'solemnised') na mtu mwenye madaraka ya kufungisha ndoa.
3. Ndoa iwe 'consummated' yaani tendo la ndoa lifanyike kati ya maarusi.

Vigezo viwili vya kwanza vinaweza kutokea, lakini cha tatu kikakosekana. Hapo hakuna ndoa. Kwa mfano Padri ashuhudie arusi kanisani na kuwapa kabisa maarusi cheti cha ndoa. Usiku huo mme anaomba waahirishe unyumba kwa kuwa amechoka mno na pilka pilka za arusi. Kesho yake anaumwa tumbo. Siku inayofuata kuna sababu nyingine, mpaka mwezi unakatika bila unyumba kufanyika kati ya maarusi hawa. Baadaye inakuja kuthibitishwa kwamba mwanaume ni hanithi: hawezi kufanya tendo la ndoa. Kikanisa, kitakachofanyika ni 'annulment' ambayo ni kusema kwamba, japo Padri alifungisha 'ndoa' hiyo, ukweli ni kwamba hakukuwa na ndoa kwa kuwa kigezo cha tatu hakikutimizwa. Kwa hiyo, 'ndoa' hiyo itafutwa kwa 'annulment', yaani kwa kutamka kwamba hakukufungwa ndoa kati ya wahusika. Hapa hakuna talaka kwa kuwa hakuna ndoa iliyofungwa ili sasa ikomeshwe kwa talaka.

Mfano mwingine ambapo 'annulment' hufanyika ni pale mtu na dada yake waoane kanisani bila kujua kwamba wao ni ndugu wa damu. Wanaweza wakaishi katika 'ndoa' yao kwa miaka mingi wakazaa na watoto. Pindi ikijulikana kwamba wao ni ndugu wa damu, 'ndoa' hiyo itasitishwa kwa 'annulment' ambayo ni kusema kwamba ndoa ilikuwa batili japo ilifungishwa na Padri. It was nul and void. Hakuna talaka hapa kwa kuwa hakukuwa na ndoa.
Nimekuelewa vema na sidhani kama umenipinga bali umeeleza kwa protocol zaidi na duongeza mambo mengine nisiyoyajua. Huwenda mwenzangu ni mkatoliki muhusika zaidi(padre , katekista,mleyi,askofu,mzee wa kanisa au shemasi) kuliko mimi. Ingawa hata mimi sikuzungumzia talaka kwa maana ya karatasi kama wanayotumia waislamu ila nilimanisha sababu moja wapo inayotosha kuachanisha watu. Nadhani kutumia neno kuachanisha ndio palipoleta shida ulipenda nisitumie neno hilo kwakuaa ndo inavunjwa na kiwa kama haikiwepo .
Ila ahsante kwa ufafanuzi wa kiteolojia.
 
Inamaana ile mpk kifo,
Kinakua Ni kiapo batili au[emoji848]
Mkuu sana deep pond . Ndoa za kikatoloki zina vinisheria ambavyo hata kwenye biblia hazipo. Mfano biblia inasema unaruhusiwa kumwacha meanamke kwa kosa la "uzinzi" kufanya tendo la ngono na mtu mwingine asiye mwandoa wake. Lakini kiuhalisia sababu hiyo haijafanikiwa kuwatebganisha wanandoa wa kikatoliki .
Karibu Ng'wanamalundi kwa ufafanuzi
 
View attachment 2208333

Katika sheria za dini za kikiristo ni kwamba hurusiwi kuongeza mke na kifo pekee ndicho cha kuwatenganisha, kinyume na hapo ni nje ya sheria za ukristo.

Sasa inapotokea mfano mke wako anafungwa jela miak 30 ama hata kifungo cha maisha na bado hamna hata mtoto, ndoa bado ilikuwa mbichi, hapo hii hali inatatuliwa vipi?

Haiwezekani Mungu aweke sheria ya kukubana sehemu flani na asiweke mlango wa kutokea, hizi sheria za kuoa ni za viongozi wa makanisa na sio maandiko,

MUHIMU: Wanaokwenda jela sio wote wenye hatia, wengine wamebambikiwa
Daaaah aiseee.
 
Nimekuelewa vema na sidhani kama umenipinga bali umeeleza kwa protocol zaidi na duongeza mambo mengine nisiyoyajua. Huwenda mwenzangu ni mkatoliki muhusika zaidi(padre , katekista,mleyi,askofu,mzee wa kanisa au shemasi) kuliko mimi. Ingawa hata mimi sikuzungumzia talaka kwa maana ya karatasi kama wanayotumia waislamu ila nilimanisha sababu moja wapo inayotosha kuachanisha watu. Nadhani kutumia neno kuachanisha ndio palipoleta shida ulipenda nisitumie neno hilo kwakuaa ndo inavunjwa na kiwa kama haikiwepo .
Ila ahsante kwa ufafanuzi wa kiteolojia.
Mkuu, ni kweli sikuwa nakupinga. Nilijikita katika kufafanua mambo zaidi kwa kutumia uzi wako ulioanzisha hoja hiyo. Hoja zako ni sawasawa na zangu. Lakini niliona niende mbele kwa kuelezea mengi zaidi ya uliyoyasema.
Kwamba mwenzio ni Mkatoliki mhusika zaidi kuliko wewe, hilo siyo kweli. Nilibatizwa katika dini ya Katoliki, nikapata Komunio ya Kwanza na Kipaimara, na baadaye nikafunga ndoa, yote hayo chini ya Kanisa Katoliki. Sina cha ziada ya hapo.
 
Mkuu sana deep pond . Ndoa za kikatoloki zina vinisheria ambavyo hata kwenye biblia hazipo. Mfano biblia inasema unaruhusiwa kumwacha meanamke kwa kosa la "uzinzi" kufanya tendo la ngono na mtu mwingine asiye mwandoa wake. Lakini kiuhalisia sababu hiyo haijafanikiwa kuwatebganisha wanandoa wa kikatoliki .
Karibu Ng'wanamalundi kwa ufafanuzi
Mkuu, unayoyasema yalijibiwa na Yesu mwenyewe; angalia Mateo 19: 3-8.
'Some Pharises came to him and tried to trap him by asking, "Does our Law allow a man to divorce his wife for whatever reason he wishes?" Jesus answered, "Haven't you read the scripture that says that in the beginning the Creator made people male and female? And God said 'For this reason a man will leave his father and mother and unite with his wife, and the two will become one'. So they are no longer two, but one. No human being must separate, then, what God has joined together." The Pharisees asked him, "Why , then, did Moses give the law for a man to hand his wife a divorce notice and send her away?" Jesus answered, "Moses gave you permission to divorce your wives because you are so hard to teach. But it was not like that at the time of creation".
 
Dini iliweka wazi pia tuoe ili kuondokana na uzinzi, sasa katika hii hali mwanaume anaweza kukaa miaka 30 bila kupata unyumba ?
Ngumu sana. Nimefikiria hivi tuko tunaishi na wake zetu na bado haturidhiki tunachepuka, sasa uambiwe miaka 30? Achana na hilo, hata mwaka mmoja ni ngumu sana kuvumilia sema mwanamke akifungwa mwaka akitoka lazima atajua tu jamaa alikuwa anachepuka. ila atavumilia
 
Hakuna cha vatican wala cha marekani, sheria za ukristo ni kwamba huwezi kuongeza mke na kitu pekee cha kuwatenganisha ni kifo
Yapo mazingira ndoa hutenganishwa, mfano uzinzi lipo wazi.

Na hili pia nadhani wanatenganisha.
 
Yesu alipoletewa yule kahaba aliyehukumiwa kutupiwa mawe alisema asiye na dhambi awe wa kwanza kumrushia jiwe. Wote waliondoka. Kuna dhambi unatenda kutokana na mazingira unayoishi au uliyonayo..

Waislam wanaruhusiwa kula nyama ya pork kama hakuna chakula kingine.
Hapa ndugu unapotosha.

Ushauri wako wa kusema aende kuomba ushauri hapo ndio umekaa sawa, naamini kabisa katika hili ndoa inavunjwa tena na askofu wala si kwa papa.
 
Hakuna cha vatican wala cha marekani, sheria za ukristo ni kwamba huwezi kuongeza mke na kitu pekee cha kuwatenganisha ni kifo
Kwa hiyo mkristo mke wake akifungwa miaka 30 haoi tena wala kufanya ngono?tuache kujidanganya
 
Haina mjadala unaoa tu mwngne, wakati mwngne tujue kuwa hiz din n sheria na sheria zmewekwa ili zvunjwe teh teh teh!
Bora kuoa mwngne kuliko kuanza kudanga huku na kule, oa akitoka jela uje kuomba ushaur tena.
Watu wanafungwa miaka mitano tu wakitoka wanakuta mke kashaolewa au mume kaoa ndo iwe 30!!?unaoa tu
 
Siku hizi Maaskofu wa Majimbo wamepewa mamlaka ya kutengua ndoa. Haichukui tena muda mrefu kama kuna sababu ya msingi.

Nafahamu mifano miwili ya ndoa ambazo utenguzi haukuchukua zaidi ya mwaka mmoja.
Hakuna mamlaka zaidi ya mahakama kwenye kutengua ndoa
The rest ni ndoto za abunuasi
Hao maaskofu hawana locus stand
Pia hawa toi divorce certificate mkuu
 
Ni kuoa mke mwingine tu hakuna namna..mambo Kama hayo Mungu husamehe Jamani..
 
Si kweli unayoyasemea kwa Ukatoliki. Vigezo vitatu vinahitajika kwa ndoa kutambuliwa katika Kanisa Katoliki:
1. Ndoa iwe kati ya mwanamme na mwanamke.
2. Ndoa ifungwe (iwe 'solemnised') na mtu mwenye madaraka ya kufungisha ndoa.
3. Ndoa iwe 'consummated' yaani tendo la ndoa lifanyike kati ya maarusi.

Vigezo viwili vya kwanza vinaweza kutokea, lakini cha tatu kikakosekana. Hapo hakuna ndoa. Kwa mfano Padri ashuhudie arusi kanisani na kuwapa kabisa maarusi cheti cha ndoa. Usiku huo mme anaomba waahirishe unyumba kwa kuwa amechoka mno na pilka pilka za arusi. Kesho yake anaumwa tumbo. Siku inayofuata kuna sababu nyingine, mpaka mwezi unakatika bila unyumba kufanyika kati ya maarusi hawa. Baadaye inakuja kuthibitishwa kwamba mwanaume ni hanithi: hawezi kufanya tendo la ndoa. Kikanisa, kitakachofanyika ni 'annulment' ambayo ni kusema kwamba, japo Padri alifungisha 'ndoa' hiyo, ukweli ni kwamba hakukuwa na ndoa kwa kuwa kigezo cha tatu hakikutimizwa. Kwa hiyo, 'ndoa' hiyo itafutwa kwa 'annulment', yaani kwa kutamka kwamba hakukufungwa ndoa kati ya wahusika. Hapa hakuna talaka kwa kuwa hakuna ndoa iliyofungwa ili sasa ikomeshwe kwa talaka.

Mfano mwingine ambapo 'annulment' hufanyika ni pale mtu na dada yake waoane kanisani bila kujua kwamba wao ni ndugu wa damu. Wanaweza wakaishi katika 'ndoa' yao kwa miaka mingi wakazaa na watoto. Pindi ikijulikana kwamba wao ni ndugu wa damu, 'ndoa' hiyo itasitishwa kwa 'annulment' ambayo ni kusema kwamba ndoa ilikuwa batili japo ilifungishwa na Padri. It was nul and void. Hakuna talaka hapa kwa kuwa hakukuwa na ndoa.
Cha kuongezea,
Ndoa haitakiwa kufungwa kama kuna Chembe Chembe za Uongo,
Kwa maan hyo wew unaetak kufunga Ndoa wakati unajua ni hanithi inadhihilisha wazi kabisa kwamba ulikuwa Muongo Kwa Mwenzio
 
Kitu Ambacho kanisa limekaa kimya ni kuhusu Baadhi ya Watu kunyimwa Baadhi ya Sakrament za Either Ndoa au Update,
Mfano,
Mahanithi (either wa kusababishwa au wa kuzaliwa),watu wenye Jinsia mbili nk
 
View attachment 2208333

Katika sheria za dini za kikiristo ni kwamba hurusiwi kuongeza mke na kifo pekee ndicho cha kuwatenganisha, kinyume na hapo ni nje ya sheria za ukristo.

Sasa inapotokea mfano mke wako anafungwa jela miak 30 ama hata kifungo cha maisha na bado hamna hata mtoto, ndoa bado ilikuwa mbichi, hapo hii hali inatatuliwa vipi?

Haiwezekani Mungu aweke sheria ya kukubana sehemu flani na asiweke mlango wa kutokea, hizi sheria za kuoa ni za viongozi wa makanisa na sio maandiko,

MUHIMU: Wanaokwenda jela sio wote wenye hatia, wengine wamebambikiwa
Cha msingi wakat wa harusi mnakubaliana kipengele cha kula kiapo kisiwepo
 
Hakuna cha vatican wala cha marekani, sheria za ukristo ni kwamba huwezi kuongeza mke na kitu pekee cha kuwatenganisha ni kifo
Je technically unaweza kumuua, ukatubu halafu ukaoa mwingine ?
 
Back
Top Bottom