Pamba, Korosho Mmeshindwa kununua sasa mnanyang'anya Watu Choroko zao

Pamba, Korosho Mmeshindwa kununua sasa mnanyang'anya Watu Choroko zao

Kwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.

Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.

Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?

Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?

Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.

Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini

Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?

Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?

Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?
 
Na kahawa Mambo ndo hata hata, lakini ngoja wakulima waipate fresh maana huwa hawasikii Wala kuelewa somo
 
Kalamu1,
Umehoji maswali mazuri, wajuvi wa namna vyama vya ushirika vinaanzishwa watuelimishe!
Lakini dosari kubwa ni kuonekana vyama vya ushirika vinalelewa na kudekezwa na serikali badala ya kushindana na wafanyabiashara wengine binafsi katika soko.

Kama serikali inaweza kutaifisha mali za wafanyabiashara na kuvipa vyama vya ushirika, watendaji wake hawawezi kuwa na akili na maarifa ya kuviendesha kibiashara! Kwa hiyo vitabaki kuwa pango la wanyang'anyi wamaosubiri vya bure kutoka kwa mjomba wao serikali.
 
Kalamu1, Huwenda Kuna Siri kubwa kwenye hivi vyama, tuitazame serikali ipo upande upi wawakulima au vyama? Hivi vyama nimtaji wanani? Wakulima wanakopwa hawalipwi namazao yao yanakuwa yashauzwa au wanalipwa kidogo, kwanini wanunuzi binafsi wanapendwa nawakulima?

Nani anasema wanunuzi binafsi wanawapunja wakulima au wenyewe wauzaji au serikali au vyama vya ushirika? Je hivi vyama vinaushirika nawakulima? Kama wakulima wanalima wenyewe kwanini walazimishwe pakuuza? Mbona hatusikii Bei elekezi kwenye mabati,saruji,nabidhaa nyingi zaviwandani?

kwani mkulima anatatizo gani? Mwisho nashauri hivyo vyama vyaushirika vipewe mitaji na serikali vilime vyenyewe mazao husika watauza watavyo ardhi yakilimo nikubwa Sana ili wananchi binafsi waamue wenyewe pakuuza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo hasara ya kuwa mshamba. Kwenye vyama vya ushirika ni rahisi kwa serikali kuchota hela kama inavyotaka maana wakulima huwa wanakopesha bidhaa zao.

Hili swala linafanywa ili kumzuia mkulima asije akapanda hata siku moja. Ni hatari maana mkulima anakopesha ushirika analipwa baada ya miezi mingi tena hela pungufu. Nimeona kwenye kahawa namna watu wanavyokopesha mazao yao.
 
Ripoti ya Bank of Tanzania ya October 2019 imeonesha kwamba, mapato ya agricultural export ya mwaka ulioishia Agosti 2019 yaliporomika kwa asilimia 60.

Kwa kiasi kikubwa hili lilitokana na serikali kuingilia bei ya korosho.

Naona hatujaelewa somo bado.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Kulikoni soko la "dhahabu ya kijani" Tanzania - JamiiForums
Kwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.

Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.

Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?

Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?

Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.

Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini

Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?

Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?

Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wakulima wanalima wenyewe kwanini walazimishwe pakuuza? Mbona hatusikii Bei elekezi kwenye mabati,saruji,nabidhaa nyingi zaviwandani?
Ndio maana nikaomba kuelimishwa mkuu wangu 'nyembela' juu ya uhusiano wa wakulima na hivi vyama vya ushirika, kwa sababu siujui.

Je, hivi vyama vya ushirika haviwezi kuwa mali ya wakulima wenyewe na wakajiamlia wao wenyewe wanataka vyama vyao vifanye nini na mambo mengine?
Hapa ndipo akili yangu ilipogotea. Je, ule ushirika uliokuwepo hapo zamani, kama kule Kilimanjaro, mbona ni kama walikuwa na mafanikio, au? Kwa nini tusirudishe muundo huo tena kama hakuna athari nisizozijua?

Hili jambo la mazao ya wananchi linatia hasira sanakwa kutoshughulikiwa ipasavyo na serikali. Pengine kutokuwa na ufahamu wa matatizo ndiko kunakotufanya sisi tukose subira!
 
Ripoti ya Bank of Tanzania ya October 2019 imeonesha kwamba, mapato ya agricultural export ya mwaka ulioishia Agosti 2019 yaliporomika kwa asilimia 60.

Kwa kiasi kikubwa hili lilitokana na serikali kuingilia bei ya korosho.

Naona hatujaelewa somo bado.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Kama hatuelewi somo rahisi kama hili, sisi tunavyo vichwa vya aina gani!
 
Huyo jamaa aliyenyaganywa nakaa naye nyumba ya tatu kutoka kwangu ....na aliweka bond mkopo nyumba yake wife kaanguka na preasure yupo hospital na alikuwa kapata soko la kupeleka indian

........hiii ni biahsara huria na ninasikia mwaka huu wanampango hata mpunga vyama vya ushirika vinunue kwa kanda ya ziwa ...kwa mkopo huku si kurudishana nyuma

sent from HUAWEI
Hili haikubaliki nadhani kuna makosa sehemu fulani.
serikali kuu itaingilia kati nadhani. Mwananchi hawezi kudhurumiwa na serikali.
 
Back
Top Bottom