Kwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.
Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.
Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?
Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?
Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.
Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini
Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?
Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?
Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?