Pamba, Korosho Mmeshindwa kununua sasa mnanyang'anya Watu Choroko zao

Pamba, Korosho Mmeshindwa kununua sasa mnanyang'anya Watu Choroko zao

Title ya thread ni ya kishabiki, inaonyesha thread hii siyo objective. Badala ya kuandika "Serikali imeshindwa..." iimeandikwa kwa maana kuwa sisi tutaosoma thread ndiyo tumeshindwa. Ninajua mwandishi alikuwa na maana gani lakini matumizi ya hiyo lugha ya kejeli ndiyo inakoseasha thamani thread nzima.
 
Vyama vyote vilishakufa na vina madeni yasiyolipika leo nani Aende kufanya biashara na bankrupt entities?
Halafu cha ajabu Mkuu Vyama vyenyewe havina pesa za kununulia mazao. Yaani Mfanyabiashara unatakiwa ufanye makubaliano na Chama cha Ushirika unahitaji aina na kiasi gani ya mazao kisha unawapatia fedha wakununulie mazao toka kwa Wakulima. Kwa kifupi Vyama hivi vimekuwa ni madalali wa mazao ya Wakulima.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kanda pendwa ni hisia tu, tingatinga halijabakiza sehemu yoyote. Kila mtu anakula jeuri ya chama kwa namna yake!
Huyu Mzee analazimisha vitu vya kipumbavu sana, yule mfanyabiashara kasema.kabisa kwamba amelipa ushuru kwa mtendaji wa Kata na risiti anazo za serikali lakini mkuu wa wilaya anatumia mabavu kunyang'anya mzigo! Nitamkumbuka sana Mzee Mwamwindi!
 
Habari wana JF

Nimeona taarifa zikimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Magu akiwanyang'anya wafanyabiashara shehena za choroko walizonunua kutoka kwa wakulima kwa madai ya kutotumia vyama vya ushirika kununua zao hilo.

Swali la kujiuliza, kwa nini serikali ya Rais Magufuli haitaki kujifunza kuwa Ushirika umeshindwa kufanya biashara na badala yake limekuwa genge la kudhulumu wananchi mali zao. Mfano ni mazao ya korosho na pamba ambayo mpaka sasa wakulima hawajalipwa malipo yao ya msimu uliopita.

Serikali ya CCM itambue kuwa kutaifisha/kunyang'anya mali za watu ni rahisi mno kuliko kufanya biashara yenyewe.

Toka kuwa Serikali ya wanyonge hadi kuwa genge la wanyang'anyi, CCM ni chama mufilisi hakiwezi kamwe kutupa uongozi wa kuendeleza taifa na watu wake.
akimaliza kwetu atakuja na kwenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali inahofia madalali kutumia huo mwanya kuwakandamiza wakulima.
Mkuu nikuulize swali la kizushi, kwa mfano hapa kuna wanunuzi wawili: mnunuzi wa kwanza ananunua kwa cash lakini pungufu ya shilngi 200 ya mnunuzi wa pili ambaye ananunua kwa mkopo ambaye hajulikani atalipa lini. Mkuu utaenda kwa mnunuzi yupi?
 
Vyama vya ushirika kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya ushirika ya mwaka 2013 vimeundwa katika 3 tier system.

1 chini kuna kuwa na vyama vya msingi au PCS ambavyo vinaundwa na wakulima wenyewe.

2 Kati kuna chama kikuu ambacho majukumu au Union ambacho wanachama wake ni hao PCS.

3 Mwisho ni Federation ambayo wanachama wake ni vyama vikuu japo PCS pia wanaweza kuwa wanachama wa shirikisho.

Hii ndiyo structure iliyopo kwe Agricultural Marketing Corperative Socities (AMCOSs)

Sasa ili serikali uweze kumonitor ushirika sheria imeanzisha chombo kinachoutwa REGISTRAR wa vyama vya ushirika ambaye ana watu wake mpaka huko wilayani ambao wengi ni mchwa wa kutafuna pesa za ushirika kwa kushirikiana na viongozi wa ushirika hasa vyama vikuu na vyama vya msingi.

Sheria ya mwaka 2003 ilikuwa na 4 tier structure ambapo kulikuwa na chama kilele au APEX ambacho kiliondolewa baada ya kuwa chanzo cha migogoro na upigaji tu.


Sasa kuhusu changamoto zilizochangia kulala kwa vyama vya ushirika na uwezo wake wa sasa kuhudumia wakulima hii ni mada ndefu kwa sababu umeomba muundo niishie hapa kwanza.
Kwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.

Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.

Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?

Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?

Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.

Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini

Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?

Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?

Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali inahofia madalali kutumia huo mwanya kuwakandamiza wakulima.
Wazo swafi kabisa na tunaliunga mkono 100%. Lakini, kuwakopa wakulima halafu uyachukue mazao yao ndio ukatembeze kutafuta soko. Hivi hilo ndo wazo safi??
Mkulima amewekeza kwenye jembe lake, akisali kila siku kuwa mvua inyeshe ya kiasi isijezidi mazao yakazolewa na maji kwa sababu ya miundo mbinu hovyo.
Sasa kavuna, unasema kumlinda ni kungoja aje mnunuzi aliyelipa cash akamuokoa huyu mkulima weye umnyang'anye bila hata kumrudishia kile alichotoa. Useme; Sitaifishi gari kwa kuwa lilikodishwa kuubeba mzigo tu. Aliyenunua mzigo unamwambia; Kimbia tena usiangalie nyuma au nikufunge kwa uhujumu uchumi.
We waona; Hallal?? Nadhani we au miye mmojapo ni chizi. Onesha muunganiko wa utaifishaji wa kilichonunuliwa bila refund na ukandamizaji wa madalali kwa mkulima.
 
Vyama vya ushirika kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya ushirika ya mwaka 2013 vimeundwa katika 3 tier system.

1 chini kuna kuwa na vyama vya msingi au PCS ambavyo vinaundwa na wakulima wenyewe.

2 Kati kuna chama kikuu ambacho majukumu au Union ambacho wanachama wake ni hao PCS.

3 Mwisho ni Federation ambayo wanachama wake ni vyama vikuu japo PCS pia wanaweza kuwa wanachama wa shirikisho.

Hii ndiyo structure iliyopo kwe Agricultural Marketing Corperative Socities (AMCOSs)

Sasa ili serikali uweze kumonitor ushirika sheria imeanzisha chombo kinachoutwa REGISTRAR wa vyama vya ushirika ambaye ana watu wake mpaka huko wilayani ambao wengi ni mchwa wa kutafuna pesa za ushirika kwa kushirikiana na viongozi wa ushirika hasa vyama vikuu na vyama vya msingi.

Sheria ya mwaka 2003 ilikuwa na 4 tier structure ambapo kulikuwa na chama kilele au APEX ambacho kiliondolewa baada ya kuwa chanzo cha migogoro na upigaji tu.


Sasa kuhusu changamoto zilizochangia kulala kwa vyama vya ushirika na uwezo wake wa sasa kuhudumia wakulima hii ni mada ndefu kwa sababu umeomba muundo niishie hapa kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu 'PTER', ahsante kwa somo zuri.

Kumbe 'gut feeling' yangu tokea mwanzo ilikuwa ni sahihi.

Tatizo ni bayana kabisa, lipo serikalini.

Sheria zilizopo kusimamia ushirika hazitekelezwi ipasavyo, na watendaji katika ngazi zote za ushirika hawawajibishwi kusimamia kazi zao ipasavyo.

Tatizo la wakulima ni serikali.
 
Yule mfanyabiashara ni kama anaonewa, kwanin asipewe mlolongo wa kufuata ili arejeshewe mali yake. Nimejikuta namuonea huruma kwa jinsi alivyojitetea, sasa endapo kakopa Benki ndio baaasi mnada wa nyumba yake unamhusu. Hurumaaa
Toka lini wakawa na huruma hawa,we check bandarini tu wanavopiga minada gari za watu bila huruma hawana uwezo wa kufikiri zaidi ya kukariri kumbe zipo njia mbadala tu wangetumia wakapata kodi zao bila kumpora MTU gari lake
 
Serikali inahofia madalali kutumia huo mwanya kuwakandamiza wakulima.
Wakulima sio malofa kama unavyofikiri, eti kuwakandamiza, sijui nini kwanini serikali inapenda kuingilia biashara na wakulima, usikute huyo DC mkulima akikosa kulipwa kwenye ushirika hajui hata namna ya kumsaidia, ni rahisi tu kufanya uhalifu wa kutaifisha mali za watu ili mkubwa aone anafanya kazi!
 
Huyo jamaa aliyenyaganywa nakaa naye nyumba ya tatu kutoka kwangu ....na aliweka bond mkopo nyumba yake wife kaanguka na preasure yupo hospital na alikuwa kapata soko la kupeleka indian

........hiii ni biahsara huria na ninasikia mwaka huu wanampango hata mpunga vyama vya ushirika vinunue kwa kanda ya ziwa ...kwa mkopo huku si kurudishana nyuma

sent from HUAWEI
What? Mpunga wangu nikauzie wapi? Mpunga si pamba, nitautunza ndani nile na familia yangu kidogo kidogo hata kwa miaka 4 hadi uishe. Sipend
 
Back
Top Bottom