Nimefurahi kwa sababu wakati watu wa kusini wakilia wako waliowabeza. Sasa hili limetokea kwenye ile Kanda Pendwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hata wale wa Mwanza waliojenga kwenye eneo la barabara?Kanda pendwa ni hisia tu, tingatinga halijabakiza sehemu yoyote. Kila mtu anakula jeuri ya chama kwa namna yake!
Habari wana JF
Nimeona taarifa zikimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Magu akiwanyang'anya wafanyabiashara shehena za choroko walizonunua kutoka kwa wakulima kwa madai ya kutotumia vyama vya ushirika kununua zao hilo.
Swali la kujiuliza, kwa nini serikali ya Rais Magufuli haitaki kujifunza kuwa Ushirika umeshindwa kufanya biashara na badala yake limekuwa genge la kudhulumu wananchi mali zao. Mfano ni mazao ya korosho na pamba ambayo mpaka sasa wakulima hawajalipwa malipo yao ya msimu uliopita.
Serikali ya CCM itambue kuwa kutaifisha/kunyang'anya mali za watu ni rahisi mno kuliko kufanya biashara yenyewe.
Toka kuwa Serikali ya wanyonge hadi kuwa genge la wanyang'anyi, CCM ni chama mufilisi hakiwezi kamwe kutupa uongozi wa kuendeleza taifa na watu wake.
Mi ni mwathirika wa ushirika nitakupa matukio kadhaa kwa upande wa kahawa.Kwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.
Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.
Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?
Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?
Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.
Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini
Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?
Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?
Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?
Wahusika ni washirika yaani wakulima na viongozi watakaowachagua, maafisa ushirika ambao ni serikali wanaowashauri na kuwaongoza viongozi, mrajisi wa mkoa ambaye ni serikali kazi yake ni kusimamia vyama vya mkoa wake na wakaguzi wa mahesabu ya vyama vya ushirika ambao ni taasisi ya serikali(coasco). Huo ndo muundo.Ndio maana nikaomba kuelimishwa mkuu wangu 'nyembela' juu ya uhusiano wa wakulima na hivi vyama vya ushirika, kwa sababu siujui.
Je, hivi vyama vya ushirika haviwezi kuwa mali ya wakulima wenyewe na wakajiamlia wao wenyewe wanataka vyama vyao vifanye nini na mambo mengine?
Hapa ndipo akili yangu ilipogotea. Je, ule ushirika uliokuwepo hapo zamani, kama kule Kilimanjaro, mbona ni kama walikuwa na mafanikio, au? Kwa nini tusirudishe muundo huo tena kama hakuna athari nisizozijua?
Hili jambo la mazao ya wananchi linatia hasira sanakwa kutoshughulikiwa ipasavyo na serikali. Pengine kutokuwa na ufahamu wa matatizo ndiko kunakotufanya sisi tukose subira!
Kifupi..hivyo vyama vya Ushirika ni uridhi wa wakoloni .Vyama hivi vingi vilianzishwa baada ya ww2 malengo yakiwa kuongeza tija ya uzarishaji,kusaidia wakulima kupata masomo pamoja na elimu.Ila lilijificha ilikua ni njia ya kuwezesha wakoloni kuwanyonya wakulima kwa wakati mmoja basi usishangae mpaka sasa huu mfumo upo na ndiyo mbaya zaidi.Ukienda kwa wakulima na kuwauliza kama wakati wanalima walipata msaada kutoka kwenye chama cha ushirika? Majibu tunayo....alafu mkija mnasema kua serikali ya wanyonge...Serikali ya wajamaa...kumbe uhalisia ni ubepari na ubeberu tu.Kalamu1,
Umehoji maswali mazuri, wajuvi wa namna vyama vya ushirika vinaanzishwa watuelimishe!
Lakini dosari kubwa ni kuonekana vyama vya ushirika vinalelewa na kudekezwa na serikali badala ya kushindana na wafanyabiashara wengine binafsi katika soko.
Kama serikali inaweza kutaifisha mali za wafanyabiashara na kuvipa vyama vya ushirika, watendaji wake hawawezi kuwa na akili na maarifa ya kuviendesha kibiashara! Kwa hiyo vitabaki kuwa pango la wanyang'anyi wamaosubiri vya bure kutoka kwa mjomba wao serikali.
Subiri Polepole akiishakagua utekelezaji wa ilani, wanajeshi lazima watatumwa kununua choroko virzuri kama walivyofanya kwenye korosho kule 'Ntwala'Hili haikubaliki nadhani kuna makosa sehemu fulani.
serikali kuu itaingilia kati nadhani. Mwananchi hawezi kudhurumiwa na serikali.
Huu ni unyonyajiWahusika ni washirika yaani wakulima na viongozi watakaowachagua, maafisa ushirika ambao ni serikali wanaowashauri na kuwaongoza viongozi, mrajisi wa mkoa ambaye ni serikali kazi yake ni kusimamia vyama vya mkoa wake na wakaguzi wa mahesabu ya vyama vya ushirika ambao ni taasisi ya serikali(coasco). Huo ndo muundo.
Mkuu mazao tu ni shida ambayo ishakuwa sugu miaka na miaka. Alafu utasikia walegeza pua tunapambana na BEBERU. Naishiaga kucheka tuKwenye mada kama hii, ndipo umma wa JF unapokosa fursa nzuri kabisa, ya kuwa chanzo cha elimu kwa wengi wetu.
Kwa mfano: mimi ningependa kujua muundo wa hivi vyama vya ushirika ukoje na sababu zinazofanya visiwe na ufanisi katika utendaji wake.
Hivi vyama vinaundwa na serikali, au wananchi wenyewe?
Wananchi wanayo mamlaka yoyote juu ya vyama hivi?
Ni nini wajibu wa serikali katika usimamizi wa hivi vyama.
Hizi taarifa za kuvuruga juhudi za wananchi ndizo zitakazoendelea kutufanya taifa zima kubaki maskini
Kwa nini hatuwezi kukopi tu walichofanya nchi zingine na kurekebisha kidogo kulingana na mazingira yetu, ili na sisi tupate mafanikio?
Ununuzi wa mazao ya mkulima, mbona linakuwa tatizo sugu kiasi hiki?
Miaka yote hii, tokea tupate uhuru wetu, tunashindwa nini kulishughulikia tatizo na kuliondoa kabisa?
Wezi wa choroko rudisheni choroko za watu wauni wakubwaWalanguzi fuateni sheria
Halafu cha ajabu Mkuu Vyama vyenyewe havina pesa za kununulia mazao. Yaani Mfanyabiashara unatakiwa ufanye makubaliano na Chama cha Ushirika unahitaji aina na kiasi gani ya mazao kisha unawapatia fedha wakununulie mazao toka kwa Wakulima. Kwa kifupi Vyama hivi vimekuwa ni madalali wa mazao ya Wakulima.Serikali iko busy kupambana na raia wake.
Suala la la kilimo serikali ya ccm ilishashindwa toka enzi za Nyerere ingewaacha wananchi wakajilimia tu wanavyotaka wenyewe.
Serikali yenyewe imejaa mbumbumbu tupu itaweza vipi kutatua changamoto lukuki za kilimo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli mkuu hao ni wezi zaidi ya mkoloniKifupi..hivyo vyama vya Ushirika ni uridhi wa wakoloni .Vyama hivi vingi vilianzishwa baada ya ww2 malengo yakiwa kuongeza tija ya uzarishaji,kusaidia wakulima kupata masomo pamoja na elimu.Ila lilijificha ilikua ni njia ya kuwezesha wakoloni kuwanyonya wakulima kwa wakati mmoja basi usishangae mpaka sasa huu mfumo upo na ndiyo mbaya zaidi.Ukienda kwa wakulima na kuwauliza kama wakati wanalima walipata msaada kutoka kwenye chama cha ushirika? Majibu tunayo....alafu mkija mnasema kua serikali ya wanyonge...Serikali ya wajamaa...kumbe uhalisia ni ubepari na ubeberu tu.
Nimekusoma vizuri sana, mkuu wangu 'Mbekenga', nimepata mwanzo wa somo mhimu toka kwako.Mi ni mwathirika wa ushirika nitakupa matukio kadhaa kwa upande wa kahawa.
Ngazi ya chini kabisa ni vyama vya msingi. Kuna ghala, m/kiti, karani, wajumbe, mlinzi. Wakulima huleta mazao (kahawa) kwenye ghala, hupima na kupewa stakabadhi ya kilo. Ghala likijaa karani anaita gari kutoka chama kikuu. Chama kikuu kinakoboa na kuunganisha uzito na vyama vikuu vingine wanaenda kwenye soko la dunia.
Madhara ya ushirika
1. Mizani ya mawe wazee hawajui kuisoma hivyo karani anaiba kilo na kujiwejekea kwa jina lake na wenzake ila wengi wamepatwa na mabalaa
2. Mkulima utakaa na shida zako labda chama kikuu kiwahurumie kiwalipe nusu ya malipo kwa kukisia bei. Baadae mnaweza kuambiwa soko la dunia limeshuka hakuna nyongeza na huna wa kumhoji kwa sababu hakuna mkulima wa kijijini aliyewahi kuona soko la dunia.
3. Mzigo wa mazao unaweza kupigwa ghalani au ukaharibika wakulima wakalazimishwa kukatwa.
4. Gharama zote za uendeshaji wa ofisi, za kusafiri kwenda soko la dunia, n.k zinalipwa na mkulima. Sijui anayepanga viwango vya mishahara na benefits.
Sasa kwa kuwa mkulima anakuwa ameshasubiri muda mrefu, hela anayopewa anashangilia ila swala la imechotwa kiasi gani na imechotwa na nani kwa matumizi gani hayo wanajua intelijensia.
Kinachoumiza ni kwamba anaweza kuja mnunuzi toka nchi jirani anatoa bei mara mbili ya bei ya ushirika na analipa cash lkn ataitwa mhujumu uchumi.
Hapa ni upande wa kahawa ila kila zao lina sarakasi zake.
Ahsante sana mkuu, kwa ufafanuzi huu.Wahusika ni washirika yaani wakulima na viongozi watakaowachagua, maafisa ushirika ambao ni serikali wanaowashauri na kuwaongoza viongozi, mrajisi wa mkoa ambaye ni serikali kazi yake ni kusimamia vyama vya mkoa wake na wakaguzi wa mahesabu ya vyama vya ushirika ambao ni taasisi ya serikali(coasco). Huo ndo muundo.
Mbaazi nazo waliziuwa halafu siku ya kura wanaenda na Mapolisi kuwatisha Wakulima
Hali ni MBAYA SANA kila mahali na kwa kila zao la biashara. Ushirika kumejaa urasimu na WIZI, WIZI, WIZI.Habari wana JF
Nimeona taarifa zikimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Magu akiwanyang'anya wafanyabiashara shehena za choroko walizonunua kutoka kwa wakulima kwa madai ya kutotumia vyama vya ushirika kununua zao hilo.
Swali la kujiuliza, kwa nini serikali ya Rais Magufuli haitaki kujifunza kuwa Ushirika umeshindwa kufanya biashara na badala yake limekuwa genge la kudhulumu wananchi mali zao. Mfano ni mazao ya korosho na pamba ambayo mpaka sasa wakulima hawajalipwa malipo yao ya msimu uliopita.
Serikali ya CCM itambue kuwa kutaifisha/kunyang'anya mali za watu ni rahisi mno kuliko kufanya biashara yenyewe.
Toka kuwa Serikali ya wanyonge hadi kuwa genge la wanyang'anyi, CCM ni chama mufilisi hakiwezi kamwe kutupa uongozi wa kuendeleza taifa na watu wake.
Hili haikubaliki nadhani kuna makosa sehemu fulani.
serikali kuu itaingilia kati nadhani. Mwananchi hawezi kudhurumiwa na serikali.