Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Tuna chini ya siku 150 kuelekea uchaguzi mkuu.
Huu utakuwa uchaguzi mkuu tofauti kabisa na chaguzi nyingine zote zilizopita
Hakuna amsha amsha hakuna shamra shamra
Hakuna kimbiza kimbiza... Kumetulia sana na kwa sehemu kuna wasiwasi, woga na sononi kwa wananchi... Lakini pia wana tashwishwi ya kutaka kuona maajabu yakitendeka.
Muda uliobaki ni mchache sana lakini ni muhimu sana kwa kila dakika inayo tiktok.. Kuna mambo yanaendelea kimyakimya... Chinichini lakini kwa haraka na wepesi wa ajabu
The race against time...! Kama kutakuwa na huo uchaguzi (achana na neno HURU na HAKI) Tanganyika inaweza kuishangaza dunia.. Kila zama huwa na kurasa zake... Na unapofika wakati wa kufunua ukurasa husika huna budi.. huna jinsi.. Huna namna.. Huna hiari... Inabidi kuufunua...!!!
Kila jambo huwa na kikomo cha kuwa... Kikomo cha zama.. Kikomo cha nyakati... MWANADAMU ni mtumwa wa muda... Achana na maneno HURU na HAKI kuna watu walivikwa ukuu wakiwa hawapo... Kuna watu walikabidhiwa majukumu makubwa wakiwa mbali uhamishoni..
Kuna baadhi ya imani ukitaka kuoa mke si lazima uwepo eneo la tukio... Ndugu yako anaweza kukuolea kwa maneno halafu vitendo ukaja kufanya mwenyewe
Hili ni pambazuko la kipenga cha mwisho.. Kila alfajiri ipitayo haitarudi tena... Nje upepo unavuma lakini unavuma na mengi... Ni alfajiri nyingine tena...
Natambua wazi jana ulilala fofofo baada ya uchovu wa kazi na mihangaiko ya siku nzima... Juma zima... Lakini wapo ambao hawalali... Hawakulala na hawatalala mpaka kipenga cha mwisho kitakapodhihiri mwangwi wake na kupotelea kwenye kadamnasi ya hadhira yenye tashwishwi kubwa ya mabadiliko
Ni alfajiri nyingine tena.. Wanaume hawajalala ni mwendo wa kuandaa mazingira ili timu pinzani isiliguse dimba.. Kisha tutangaziane ushindi mnono wa kishindo!!
Kwenye kila andishi kuna TAMATI... Kama tamati ya andiko lako imetimia funika buku lako ulirudishe kabatini kwakuwa hakuna kurasa zaidi... Huhitaji kufanya marudio ya kurasa
Kuna kitabu kipya na wasomaji wapya.. Wape nafasi kwa upendo na bila ghiliba wasome kwa utulivu na amani kurasa zao... Nao kuna siku watafikia TAMATI... Usilazimishe makhaba kama hisia zumeshakufa
Kumbuka ni wafu pekee ndio wasiokula wala kunywa... Chumvi ikiisha ladha haifai tena kwakuwa hakuna cha kuipa ladha tena..
Ni alfajiri ya kipenga cha mwisho. Pambazuko lenye tumaini jipya. Achana na maneno HURU NA HAKI.. Uchaguzi utafanyika.. Maajabu yatatokea na dunia itashangaa
Jr[emoji769]
Huu utakuwa uchaguzi mkuu tofauti kabisa na chaguzi nyingine zote zilizopita
Hakuna amsha amsha hakuna shamra shamra
Hakuna kimbiza kimbiza... Kumetulia sana na kwa sehemu kuna wasiwasi, woga na sononi kwa wananchi... Lakini pia wana tashwishwi ya kutaka kuona maajabu yakitendeka.
Muda uliobaki ni mchache sana lakini ni muhimu sana kwa kila dakika inayo tiktok.. Kuna mambo yanaendelea kimyakimya... Chinichini lakini kwa haraka na wepesi wa ajabu
The race against time...! Kama kutakuwa na huo uchaguzi (achana na neno HURU na HAKI) Tanganyika inaweza kuishangaza dunia.. Kila zama huwa na kurasa zake... Na unapofika wakati wa kufunua ukurasa husika huna budi.. huna jinsi.. Huna namna.. Huna hiari... Inabidi kuufunua...!!!
Kila jambo huwa na kikomo cha kuwa... Kikomo cha zama.. Kikomo cha nyakati... MWANADAMU ni mtumwa wa muda... Achana na maneno HURU na HAKI kuna watu walivikwa ukuu wakiwa hawapo... Kuna watu walikabidhiwa majukumu makubwa wakiwa mbali uhamishoni..
Kuna baadhi ya imani ukitaka kuoa mke si lazima uwepo eneo la tukio... Ndugu yako anaweza kukuolea kwa maneno halafu vitendo ukaja kufanya mwenyewe
Hili ni pambazuko la kipenga cha mwisho.. Kila alfajiri ipitayo haitarudi tena... Nje upepo unavuma lakini unavuma na mengi... Ni alfajiri nyingine tena...
Natambua wazi jana ulilala fofofo baada ya uchovu wa kazi na mihangaiko ya siku nzima... Juma zima... Lakini wapo ambao hawalali... Hawakulala na hawatalala mpaka kipenga cha mwisho kitakapodhihiri mwangwi wake na kupotelea kwenye kadamnasi ya hadhira yenye tashwishwi kubwa ya mabadiliko
Ni alfajiri nyingine tena.. Wanaume hawajalala ni mwendo wa kuandaa mazingira ili timu pinzani isiliguse dimba.. Kisha tutangaziane ushindi mnono wa kishindo!!
Kwenye kila andishi kuna TAMATI... Kama tamati ya andiko lako imetimia funika buku lako ulirudishe kabatini kwakuwa hakuna kurasa zaidi... Huhitaji kufanya marudio ya kurasa
Kuna kitabu kipya na wasomaji wapya.. Wape nafasi kwa upendo na bila ghiliba wasome kwa utulivu na amani kurasa zao... Nao kuna siku watafikia TAMATI... Usilazimishe makhaba kama hisia zumeshakufa
Kumbuka ni wafu pekee ndio wasiokula wala kunywa... Chumvi ikiisha ladha haifai tena kwakuwa hakuna cha kuipa ladha tena..
Ni alfajiri ya kipenga cha mwisho. Pambazuko lenye tumaini jipya. Achana na maneno HURU NA HAKI.. Uchaguzi utafanyika.. Maajabu yatatokea na dunia itashangaa
Jr[emoji769]