Pamoja na Katiba Mpya Kenya, Polisi wapiga marufuku Maandamano. CHADEMA jifunzeni kitu Hapo!

KATIBA mpya tunayodai TANZANIA Si waliyonayo Kenya.
 
Haya yote ni mafunzo muhimu tutengeneze katiba bora kabisa kama ile ya Marekani ambayo mwendawazimu Trump alishindwa kuichezea.
Hakuna Cha tofauti Mzee, principal ni zile zile na wanaosimamia utekelezaji ni watu Hawa Hawa wa Leo na kesho wanaotaka madaraka na pesa..

Don't exaggerate mambo au kuwa na matumaini makuubwa ambayo hayawezi tokea.
 
Kati ya watu wajinga na ufinyu wa tafukuri ni huyu jamaa... Kwahiyo uliambiwa ndani ya katiba mpya Kuna hoja ya maandamano pekee?, Kwamba kwasababu Kenya polisi wanezuai maandamano basi Tz haihitaji katiba mpya?. Wewe ni sawa na kangi Lugola mkata viuno wa Magufuli....!
 
Sasa Katiba Mpya ya nini hasa ikiwa kile mnalalamikia Bado hakiletwi na Katiba Mpya?
 
Mbwiga hujambo lakini"

Wapi nimesema Tanzania haihitaji Katiba mpya?

Kama mbege huwezi kunywa kangara!
 
Halafu Ruto ameteua ma CAS kinyume na katiba ya Kenya! Kaweka na cheo Cha Waziri Mkuu (Musalia Mudavadi) wakati hakimo katika katiba.
Bob aliwaambia kuwa na Katiba Mpya ni jambo Moja na kuitekeleza ni jambo jingine..

Mfano Rais anamiliki Central Intelligence Unit ambao huwezi kuwajua akitaka kumshinikiza Spika au Jaji anaweza na ushahidi hakuna maana anawatumia hao hao Jamaa kuwatisha hawataki wanakufa kweli..

Mpaka hapo Katiba zenu zinakuwa zimewasaidia nini?
 
Unaopingana na mkt wako wa chama kuhusu Katiba mpya ndugu Mhafidhina?
 

Ruto aliongoza kundi la kupinga katiba mpya, hivyo usishangae.
 
Watu wanafanya uhalifu kwa kujificha kwenye katiba, hakuna sheria inayo ruhusa kufanya vitendo vya vurugu na kuathiri haki za watu wengine kwenye jamii kama maandamano yawe ya amani kinachotokea kenya ni vurugu na kupambana na Serikali iliyopo madarakani kimsingi unavyodai haki haitakiwi uathiri haki za watu wengine Polisi lazima wazuie hayo maandamano sababu yana mlengo wa kuvuruga amani kwenye jamii kwenye katiba kuna haki za msingi na exemption zake ikiwemo sababu za kiusalama huku bongo lazima uchakae waulize akina fulani.
 
Aisee. Naona unaifanya kazi yako kwa weledi mkubwa. Huku unaeneza taarifa zinazoonyesha utendaji wa hali ya juu wa serikali ya CCM kwa maslahi ya nchi.

Halafu huku unawakatisha tamaa wapinzani kwamba katiba mpya, siasa na wanasiasa kwa ujumla havina maana! Kwamba nchi imeoza (nothing works). Hivyo, wasijusumbue bali wahangaikie maslahi yao binafsi; watafute hela tu kwa njia yoyote ile na kuachana na “ujinga wa katiba mpya”!

Yaelekea kitengo cha propaganda cha CCM kinazidi kuwa njema sana siku hizi. Kimeshajua Watanzania wengi hawana akili. Fikra zimepinda kweli! Hawana uwezo wa kuona mantiki. All the best.
 
Naona unateseka sana na CHADEMA.
Hauna mambo ya kuandika zaidi ya CHADEMA?
 
Watatandikwa kama last time ,Dunia itaona na haitafanya kitu [emoji12][emoji12][emoji12][emoji12]

Katiba Mpya ni scarm I have been telling you,tafuta pesa tuu ndio walau kuna unafuu.
Huyajui madhila yanayowapata watu kutokana na uendeshaji wa nchi kwa katiba hii tuliyo nayo iliyopitwa na wakati.
Pengine hujakumbana na maovu hayo ndio maana unaona Katiba mpya ni porojo.
 
Wahafidhina, katiba mpya inawapa shida sana....!!
 
Wanaodai katiba mpya kuna maswali ukiwauliza hutopata majibu ya maana. Moja ya swali ni kama hili alilouliza mleta thread.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…