Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Tamko la aina hiyo limeshatolewa huko nyuma na makamanda wa jeshi la Marekani na ikaonekana kama ni utani.Kwa mara nyengine limetolewa na kamanda mkuu wa vikosi vya wanamaji wa Marekani eneo la mashariki ya kati,vice admiral George Wikoff.
Katika hoja zake kamanda huyo amekumbusha kuwa vikosi vya Houth vimeshashambuliwa kwa nguvu kwa takriban miezi 10 lakini bado vikosi hivyo vina uwezo wa kuendelea kuzishambulia meli za kibiashara na za kimarekani zinazopita kwenye bahari yao.
Kauli hiyo imetolewa mara baada ya kurejea kwa kasi kwa mashambulizi ya Houth katika wiki hii ikiwa ni wiki ya tatu tangu vikosi vya Israel vilipoishambulia bandari ya Hodeada inayodhibitiwa na wanamgambo wa Houth
Katika tahadhari zake vice admiral Wikoff,amesema jeshi hilo limetumia zana nzito kupambana na silaha nyepesi za Houth kama vile droni za pigo moja na droni za baharini lakini bado wameshindwa kuzizuia silaha hizo na kutoa hakikisho la usalama kwa meli zinazopita bahari nyekundu na ile ya Yemen.
Kuonesha ugumu wa kupambana na Houth kiongozi huyo wa ngazi za juu wa jeshi la Marekani amesema jukumu la kupambana na Houth ni la ulimwengu wote kwani kila nchi ina maslahi yanayohusiana na eneo hilo.
Katika hoja zake kamanda huyo amekumbusha kuwa vikosi vya Houth vimeshashambuliwa kwa nguvu kwa takriban miezi 10 lakini bado vikosi hivyo vina uwezo wa kuendelea kuzishambulia meli za kibiashara na za kimarekani zinazopita kwenye bahari yao.
Kauli hiyo imetolewa mara baada ya kurejea kwa kasi kwa mashambulizi ya Houth katika wiki hii ikiwa ni wiki ya tatu tangu vikosi vya Israel vilipoishambulia bandari ya Hodeada inayodhibitiwa na wanamgambo wa Houth
Katika tahadhari zake vice admiral Wikoff,amesema jeshi hilo limetumia zana nzito kupambana na silaha nyepesi za Houth kama vile droni za pigo moja na droni za baharini lakini bado wameshindwa kuzizuia silaha hizo na kutoa hakikisho la usalama kwa meli zinazopita bahari nyekundu na ile ya Yemen.
Kuonesha ugumu wa kupambana na Houth kiongozi huyo wa ngazi za juu wa jeshi la Marekani amesema jukumu la kupambana na Houth ni la ulimwengu wote kwani kila nchi ina maslahi yanayohusiana na eneo hilo.