Vumilia kila kitu kitakuwa sawaWakuu tangu nifungue biashara yangu ni wiki Sasa. Mazingira na miundombinu ya hapo ninapofanyia biashara yapo vizuri ila cha ajabu siuzi vile inavyotakiwa.
Yaani mtu anakuja anauliza kidali Tsh ngapi unamwambia bei anakigeuza geuza wee anakitathmini halafu anasema anarudi ndo imeisha hiyo. Nikasema ngoja nishushe bei miguu niuze 100 ila wananipita wanaenda kwingine!
Najiuliza nakosea wapi ila sioni kama Mungu namuomba Kila siku Kila muda hata nikiwa naweka kuku kwenye mafuta naomba pia ila wapi
Sawa sister ngoja nikazeVumilia kila kitu kitakuwa sawa
Sawa mkuu ntalifanyia kaziMjue mshindani wako nje ndani ikiwezekana mtume mtu wako wakaribu ambaye anaweza kukupa taarifa kamili yaani aende pale akanunue kwa huyo mshindani wako akupe full information kwanzia alivyohudumiwa had anaondoka na pia uone tofauti ya bidhaa yako na yake . Pili jua wateja wake haris ni watu wa aina gani kwan biashara nyingi huwa kwanza ina target customers na wengine ndio watafata .jua weakness na strength zake the go beyond.
Mimi nina miezi 3 naona jau siuzi wananipita tuNgoja nikuelezee alichokimaanisha.
Yaani amemaanisha kwenye biashara ukiachilia mbali ubora wa bidhaa na bei kuna mambo mengine ya ziada.
Mambo hayo ya ziada hutofautiana kila mtu huwa ana mbinu zake au mambo yake ya ziada tofauti ya kumchota mteja ili asimsahau,akili za mteja zipo kama akili za mtoto mdogo vile unavyomzoesha kitu fulani basi atataka aendelee hivyohivyo na hataki kingine.
Hapa ndio kunaingia mambo ya ucheshi,kutoa ofa/zawadi/nyongeza,kutengeneza kachumbari tamu,buni mbinu zako binafsi za kumchota akili mteja na baada ya miezi kadhaa wanakuzoea na hawatataka kwenda kwa mwingine.
Hujawahi kuona baadhi ya wauzaji wa maduka/duka la Mangi au Mgahawa kwa nje anaweka TV watu waangalie bure ile ni mbinu mojawapo ili wateja wasimsahau iwe muda wote wanawaza kwenda kwake.
Kwa hiyo vumilia ndugu wiki moja ni ndogo mno kuitathmini biashara unatakiwa upambane angalau miezi 6 ili uwe na wateja wako na wewe
MkuuBiashara zinahitaji uvumilivu sana, usione watu wanafanya biashara kila siku ukadhani ni rahisi, hapana biashara inahitaji moyo na kuwa na matumaini.
Tena kwa aina ya bishara unayoifanya wewe ndio kabisaa, kwa sababu inaharibika, ila usikate tamaa komaa
Yani we acha tu kakaMimi nina miezi 3 naona jau siuzi wananipita tu
ASante mkuu wacha nipambanePole sana ndo BIASHARA mkuu
Sawa mkuu wacha nikaze ila daah inapoelekea ntakula mtajiwasikuyumbishe kaza
usitegeme hiyo biashara ikulishe,kukuvisha,kodi nk hadi kwanzia miezi 10 ikuze biashara kila faida unayoipata tafuta chanzo kingine cha kipato kuimarisha hiyo biashara kwa miezi 8Sawa mkuu wacha nikaze ila daah inapoelekea ntakula mtaji
Nipo rangi 3 nauza viatu unakuta kwa siku nauza 3 au 2 dah halafu bado kodi nawazaYani we acha tu kaka
DoohNipo rangi 3 nauza viatu unakuta kwa siku nauza 3 au 2 dah halafu bado kodi nawaza
SijakuelewaNa ww nenda huko kwingine