Pamoja na kushusha bei wananipita wanaenda kwingine, najiuliza nakosea wapi?

Dah mfano kama mimi nauza viatu vya kike rangi 3 bei nayeuza elfu 6 nakutana na watu wanataka viatu vya 3500 na 4000 wengi wakati mimi nina elfu 6 na 7 dah hatari
 
Toa sadaka
Lipa zaka
Toa sadaka.
Lipa zaka

Hakika mambo yako yatanyooka.
 
Changamoto yako ni "customer base" (wateja) ambayo inahitaji muda ili watu wakuamini.

Kama biashara yako ni nzuri, mazingira masafi, una kauli nzuri kwa wateja, una haiba/mvuto wa kibiashara (yaani namna unavyojiwekaweka) na unamtanguliza Mungu basi jua tatizo lako ni patience (uvumilivu wa muda).

Mimi leo asubuhi nimeenda buchani kununua nyama kwa muuzaji niliyemzoea kabisa, hapo mahali kuna mabucha mengi sana, nikamkuta jamaa anamuhudumia mtu aliyehitaji kilo za kutosha, nadhani atakuwa ni mtoa huduma za vyakula, au sherehe, ikanibidi nisubiri ingawa nilikuwa nina haraka, pamoja na kwamba nyama ya leo haikuwa nzuri kihivyo ila nilisubiri, so kilichonifanya nisubiri ni ule UTEJA.

Nilivyokuwa naondoka, nikaona kuna nyama nzuri mpaka nikaitamani kwenye mabucha mengine, nikajisemea moyoni tu kuwa nimenunua kwa sababu ya UTEJA but hakuwa na nyama nzuri, na nikasema siku nyingine nitakuwa naangalia kwanza nyama iliyopo.

Hii maana yake ni kwamba, hiyo siku nyingine nitakayokuwa naangalia kama atakuwa na mboga nzuri ni kwamba mteja unaweza mvuta kwa huduma zako tu.

So jipe muda kuna wateja wanaendelea kukuchunguza, na ukifanikiwa kumteka mmoja basi jua mtaa mzima watahamia hapo. JIPE MUDA
 
Sala ya Bwana kwa kuinyambua
 
SAWA nimekuelewa
 
Biashara saa zingine unaweza kuona kama unarogwa kumbe huduma zako mbovu au unarogwa kweli lakin ukajipa moyo kuwa biashara yako ni changa ngoja nivumilie kidogo kumbe ndio mtaji unakatika huo. Na matokeo yake unafilisika na kuanz kuambiwa maneno na watu kuwa hujui biashara

Kuna sehemu nimefungua mtaani ya chips nimemuweka dogo ndio kila kitu ila kabla ya kufungua aliniambia tuende kwa fundi ili kutengeneza mazingira

Nikamwambia dogo jiamini picha chips safi kuwa msafi sehemu ivutie hapa nimeweka hela usiniambie mambo ya waganga kma huwezi sema kabisa

Tumeanza biashara siku ya kwanza kauza 26,000
Siku ya pili 21,000 siku ya tatu 19,000. Nikaona dogo kama anataka kurudi nyuma hivi kwa sababu matzo yanapungua.

Nikafuatilia kuna jiran anauza plate 1500 badala ya 2000 ya mwanzo kwahiyo raia wengi wanaenda kule kwa bei rahisi.

Akaja kulalamika tena boss nipe kiasi kadhaa niende porini kuna mtu namuamini nishaelekezwa nikienda huko fresh tu. Tena akaenda mbali zaidi akaniambiaje 'SHIDA YAKO WEWE MSIKITINI SANA HIZI BIASHARA HUTA ZIWEZA UBAYA UPO MITAANI HUMU.!

Nimebaki na msimamo wangu kuwa asiende kwa mganga mana sitampa hata kumi labda atumie hela yake, kiufupi nimemwambia hakuna aliekuroga maisha tu magumu watu wamepunguza anasa wanakula tu chips kavu tena za buku jero na ukizingatia gunia sasa limesimama 95,000
Sasa kwa namna hii lazima faida isipatikane kama ilivyokusudiwa.
 
Kuwa mbunifu tu, tengeneza code yako kwenye ladha.

Biashara ni mchezo wa faida na hasara, tunachofanya ni kupunguza/kuiondoa hasara ili tuipate faida, ili uiondoe hasara jifunze kupitia kufeli na sio kulalamika/kukata tamaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…