Pantoni moja tu ndio linafanyakazi Kigamboni leo, nyingine ziko wapi? Kashikashi ya kusukumana kuwahi kuingia ni balaa!

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Wakuu,

Hali ya usafiri Kigamboni leo sio shwari. Kama mnavyoona watu wapo wa kutosha. Pantoni linalotumika ni moja tu, likipakia tunasubiri ligeuze kuja kutufate wengine huku. Utafikiri sio weekend.

Hakuna backup ikitokea kuna shida kama hivi? Maana jinsi watu wanasukumana kuingia ni balaa, yanaweza kutokea maafa hivihivi kimasihara huku tunaangalia.

Ikiwa hatuna backup basi kuwe na utaratibu mzuri kusimamia watu yasitokee mengine, hasa ukuzingatia kuna watoto, wanawake, wazee na wenye ulemavu ambako kwenye msongamano kama huu bila usimamizi mzuri kuna uwezekano mkubwa wa tatizo kutokea.

 
Hakika ni AIBU kwa SERIKALI iliyovunja Rekodi ya MAKUSANYO yenye TOZO na Mikopo mingi kushindwa KUNUNUA Kivuko kipya kwa Wananchi wa KIGAMBONI.LEO hii Tarehe 27/1/2024 kuna Kivuko kimoja tu ndicho kinachotoa Huduma.
Ni DHAHIRI SERIKALI imeshindwa kabisa KUTOA HUDUMA hiyo kinachohitajika ni UBINAFSISHAJI tu
Serikali imeshindwa kabisa kupambana na Changamoto za VIVUKO

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Tunataka kufanya Kafara Kubwa la Vifo ili Nyota iliyofifia kwa Nuksi na Kutokukubalika ianze Kung'aa na Mambo yaende vyema hasa kwa Mwezi Oktoba, 2025.
 
Hiyo inayofanya kazi ichomeni moto, wahusika wote watahamia hapo ferry kupata ufumbuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…