Pantsir-SM | Mfumo mpya wa ulinzi wa anga kuzinduliwa nchini Urusi

Pantsir-SM | Mfumo mpya wa ulinzi wa anga kuzinduliwa nchini Urusi

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
5,500
Reaction score
8,060
Habari!

Pantsir-SM, mfumo wa ulinzi wa anga (short-medium range mobile air defense system) unaosubiriwa kwa hamu, unatarajiwa kuzinduliwa panapo Juni 24 katika gwaride la kijeshi jijini Moscow katika sikukuu maalumu inayofahamika kama Siku ya Ushindi ama Victory Day nchini Urusi.

Mfumo huu wa Pantsir-SM ni toleo jipya na lililoboreshwa zaidi kutoka lile la awali la Pantsir-S1.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya serikali ya Urusi, toleo la Pantsir-SM litakuwa na makombora madogo kwa ajili ya kushambulia ndege ndogo zisizo na rubani (mini-drones) pia makombora mapya ya masafa marefu, mfumo ambao unatarajiwa kuonesha uwezo mkubwa wa kukabiliana na makombora na ndege zisizo na rubani.

Matayarisho ya uzinduzi wa zana hiyo mpya ya kiulinzi yangali yakiendelea kama inavyoonekana katika picha (picha ni kwa hisani ya Wizara ya Ulinzi ya Urusi):

1592635256713.png
 
Matayarisho yangali yakiendelea kuelekea sikukuu ya kitaifa ya Siku ya Ushindi.

Maadhimisho haya yalikuwa yafanyike tarehe yake mahususi Mei 9 lakini kutokana na janga la virusi vya corona yakasogezwa mbele hadi Juni 24.

Maambukizi ya virusi vya corona bado ni changamoto kubwa hasa kuelekea sikukuu hii ya kitaifa.

Mitaa mbalimbali ya jiji la Moscow imekuwa ikisheheni foleni za hapa na pale hususani kuelekea Red Square ambapo zana mbalimbali vikiwemo vifaru na magari ya kijeshi yamekuwa yakikatika barabarani.

1592654858129.png

1592654908414.png

1592654950758.png
 
Russia nchi kubwa namna hiyo sio sahihi kabisa wazidiwe kiuchumi na nchi nyingi za magharibi, sio haki kabisa.

Wajitizame na wajitathmini vizuri waangalie kama kweli watu wenye tamaa ya madaraka kama Putin kweli wana uhalali wa kuitawala nchi kama Russia.

Russia ndio nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lkn eti inazidiwa kiuchumi na China nchi ambayo inategemea zaidi Intellectual Property Theft kunyanyua uchumi wake...!!!

Kwa rasilimali walizonazo na Technical Know-how, walitarajiwa wawe namba mbili nyuma ya Marekani, hiyo ndiyo ilipashwa iwe position halali ya Russia kiuchumi lkn kwa kuwa na watawala wasiojua vipaumbele stahiki ndio maana wapo hapo walipo leo hii.
 
Matayarisho yangali yakiendelea kuelekea sikukuu ya kitaifa ya Siku ya Ushindi.

Maadhimisho haya yalikuwa yafanyike tarehe yake mahususi Mei 9 lakini kutokana na janga la virusi vya corona yakasogezwa mbele hadi Juni 24.

Maambukizi ya virusi vya corona bado ni changamoto kubwa hasa kuelekea sikukuu hii ya kitaifa.

Mitaa mbalimbali ya jiji la Moscow imekuwa ikisheheni foleni za hapa na pale hususani kuelekea Red Square ambapo zana mbalimbali vikiwemo vifaru na magari ya kijeshi yamekuwa yakikatika barabarani.

View attachment 1484221
View attachment 1484224
View attachment 1484225
Hamvai barajoa?!😲
Corona njoo wako huku 😀😀😀
 
Russia nchi kubwa namna hiyo sio sahihi kabisa wazidiwe kiuchumi na nchi nyingi za magharibi, sio haki kabisa.

Wajitizame na wajitathmini vizuri waangalie kama kweli watu wenye tamaa ya madaraka kama Putin kweli wana uhalali wa kuitawala nchi kama Russia.

Russia ndio nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lkn eti inazidiwa kiuchumi na China nchi ambayo inategemea zaidi Intellectual Property Theft kunyanyua uchumi wake...!!!

Kwa rasilimali walizonazo na Technical Know-how, walitarajiwa wawe namba mbili nyuma ya Marekani, hiyo ndiyo ilipashwa iwe position halali ya Russia kiuchumi lkn kwa kuwa na watawala wasiojua vipaumbele stahiki ndio maana wapo hapo walipo leo hii.
vipenzi vyako wao kila siku vikwazo sasa ulidhani Russia atafikaje kipato cha juu?

Halafu nchi maendeleo key determinant si eneo kubwa

Canada,USA na Australia licha ya maeneo makubwa lakini kipato chao(per capita) kiko chini ya kipato cha nchi za Skandinavia,Switzerland,Singapore,Luxembourg etc
 
Russia nchi kubwa namna hiyo sio sahihi kabisa wazidiwe kiuchumi na nchi nyingi za magharibi, sio haki kabisa.

Wajitizame na wajitathmini vizuri waangalie kama kweli watu wenye tamaa ya madaraka kama Putin kweli wana uhalali wa kuitawala nchi kama Russia.

Russia ndio nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lkn eti inazidiwa kiuchumi na China nchi ambayo inategemea zaidi Intellectual Property Theft kunyanyua uchumi wake...!!!

Kwa rasilimali walizonazo na Technical Know-how, walitarajiwa wawe namba mbili nyuma ya Marekani, hiyo ndiyo ilipashwa iwe position halali ya Russia kiuchumi lkn kwa kuwa na watawala wasiojua vipaumbele stahiki ndio maana wapo hapo walipo leo hii.
Uko sahihi mkuu, Urusi inatakiwa iwe inachuana na Marekani kwenye kila nyanja muhimu ikiwemo kiuchumi ili kuweka mizani sawa,asiwepo mwenye nguvu mmoja.

Ila cha ajabu wamepokonywa hiyo nafasi na China, ila kwenye kutumia rasilimali zao vizuri wamejitahidi sana maana wamezua sana gesi huko Ulaya magharibi na imewatajirisha sana.
 
kwa kuwa na watawala wasiojua vipaumbele stahiki ndio maana wapo hapo walipo leo hii.
Russia nchi kubwa namna hiyo sio sahihi kabisa wazidiwe kiuchumi na nchi nyingi za magharibi, sio haki kabisa.

Wajitizame na wajitathmini vizuri waangalie kama kweli watu wenye tamaa ya madaraka kama Putin kweli wana uhalali wa kuitawala nchi kama Russia.

Russia ndio nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lkn eti inazidiwa kiuchumi na China nchi ambayo inategemea zaidi Intellectual Property Theft kunyanyua uchumi wake...!!!

Kwa rasilimali walizonazo na Technical Know-how, walitarajiwa wawe namba mbili nyuma ya Marekani, hiyo ndiyo ilipashwa iwe position halali ya Russia kiuchumi lkn kwa kuwa na watawala wasiojua vipaumbele stahiki ndio maana wapo hapo walipo leo hii.
Eti wasiojua vipaumbele/vipaombele stahiki

Hv uko serious kabisa MKUU ama Unatania ?!

Kama vipaumbele vyao namba moja ndio hivyo hapo unavyoviona je ?!

Halafu ukubwa wataifa wala sio ukubwa wakiuchumi

Halaf changamoto zakiuchumi wanazozipitia RUSSIA kuepo hapo walipo wanatakiwa wapongezwe sanaa

Siungi mkono kitendo cha PUTIN kung'ang'ania madaraka ila kama ataamua iwe hivyo juu yao pia sawa pia ila mpaka sasa PUTIN kaipeleka vyema sana RUSSIA zaidi yaunavyotaka kuwaaminisha watu


PUTIN kwailipo RUSSIA pale kwasasa nikiongozi zaidi yasahihi kwao naanatakiwa apatikane kiongozi mwengine mwenye UPUTIN PUTIN flan ndani yake.
 
Uko sahihi mkuu, Urusi inatakiwa iwe inachuana na Marekani kwenye kila nyanja muhimu ikiwemo kiuchumi ili kuweka mizani sawa,asiwepo mwenye nguvu mmoja.

Ila cha ajabu wamepokonywa hiyo nafasi na China, ila kwenye kutumia rasilimali zao vizuri wamejitahidi sana maana wamezua sana gesi huko Ulaya magharibi na imewatajirisha sana.
Kwenye hii mijadala umekuwepo kwa muda kiasi usichokifahamu ni kipi? Hufahamu kwa nini China imekuwa juu? Kweli? Au unachokoza mjadala? Hata kama kuchokoza mjadala kwako itakuwa haujawatendea watu haki, hatua uliyofikia ni ya kutoa darasa.
 
Uko sahihi mkuu, Urusi inatakiwa iwe inachuana na Marekani kwenye kila nyanja muhimu ikiwemo kiuchumi ili kuweka mizani sawa,asiwepo mwenye nguvu mmoja.

Ila cha ajabu wamepokonywa hiyo nafasi na China, ila kwenye kutumia rasilimali zao vizuri wamejitahidi sana maana wamezua sana gesi huko Ulaya magharibi na imewatajirisha sana.
Uchumi wa urusi hautegemei wizi na unyonyaji wa rasimali za nchi nyingine.
Marekani mpaka kufikia hapo ilipo imeiba na kudhulumu sana rasilimali za nchi za Afrika, Asia pamoja na ulaya.
Uchumi wa Urusi unatokana na rasilimali za nchi yao wenyewe ndio maana unaona kuna gape kubwa la uchumi kati yake na Marekani.
 
vipenzi vyako wao kila siku vikwazo sasa ulidhani Russia atafikaje kipato cha juu?

Halafu nchi maendeleo key determinant si eneo kubwa

Canada,USA na Australia licha ya maeneo makubwa lakini kipato chao(per capita) kiko chini ya kipato cha nchi za Skandinavia,Switzerland,Singapore,Luxembourg etc
Swala sio eneo kubwa, swala ni kuwa Russia wana rasilimali nyingi sana kuliko nchi yoyote ile duniani lkn hilo haliendani na kiwango cha maendeleo waliyo nayo.

Ndio maana tunakuja kugundua kwamba kuna tatizo ktk uongozi, hili la Russia inafanana sana na scenario yetu Tanzania, tunasujudia kuimba mapambio wakati umaskini unazidi kutamalaki.
 
Uchumi wa urusi hautegemei wizi na unyonyaji wa rasimali za nchi nyingine.
Marekani mpaka kufikia hapo ilipo imeiba na kudhulumu sana rasilimali za nchi za Afrika, Asia pamoja na ulaya.
Uchumi wa Urusi unatokana na rasilimali za nchi yao wenyewe ndio maana unaona kuna gape kubwa la uchumi kati yake na Marekani.
Hizo ni propaganda za walioshindwa. Marekani amemdhulumu nani, hakuwahi kuwa na makoloni kama ilivyokuwa kwa mataifa mengine ya Ulaya.

Marekani wametoka mbali sana kuja kufika walipo leo, ni mikakati bora, sera nzuri, kufanya kazi kwa bidii na kuacha fikra huru zitawale ndizo zimekuwa nguzo za taifa hilo kuibuka na kuwa kinara wa mambo mengi duniani.

Kwa kuwa wamedumisha hizo tunu wataendelea kuwa kinara kwa karne nyingi zijazo. Ni kawaida kwa watu waliofeli kimaisha kuwaona wenzao waliofaulu kama wezi au Freemasons.
 
vipenzi vyako wao kila siku vikwazo sasa ulidhani Russia atafikaje kipato cha juu?

Halafu nchi maendeleo key determinant si eneo kubwa

Canada,USA na Australia licha ya maeneo makubwa lakini kipato chao(per capita) kiko chini ya kipato cha nchi za Skandinavia,Switzerland,Singapore,Luxembourg etc
Ok, sasa hiyo GDP (Per Capita) ya Russia ni dola ngapi.
 
Back
Top Bottom