Panya road wanauawa kwa risas. Je, wezi wa mabilioni ya kodi za Watanzania wanabakije salama?

Panya road wanauawa kwa risas. Je, wezi wa mabilioni ya kodi za Watanzania wanabakije salama?

Paulsylvester

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2021
Posts
1,464
Reaction score
3,379
Kundi la vijana wanaojulikana kama Panya road' limekuwa ni tishio kwa wananchi kwa siku za hivi karibuni!

Vijana hawa wamekuwa wakitishia usalama wa jamii na hata kufanya mauwaji mbalimbali kwa lengo LA kuiba na kupora kila kilicho mbele ya macho yao!

Tunapenda kulishukuru Jeshi la police kwa kuanza kudhibiti hawa vijana na kuanza kurudisha amani katika mitaa iliyokuwa ikivamiwa Mara kwa Mara kwa kuwakamata hawa vijana alimarufu kwa jina la Panya road

Mbali na kuwakamata, wengine wamekuwa wakipigwa risasi na kufa papo hapo, adhabu hii ndiyo inayopelekea kuuliza juu ya wezi wa Mabilion ya fedha za kodi za wananchi

Wezi hawa wa kodi zetu, ndio wauwaji wakubwa wa watu wanaokufa kwa kukosa huduma mahospitalini!

Watu wanaokufa kwa kukosa gari la wagonjwa ili tu kuwahi huduma katika hospital zetu kuu!

Wajawazito wanakufa kutokana na mtu mmoja tu kuiba kodi ambazo zingeondoa kero hiyo, halafu police wetu wana ng'aa ng'aa sharubu badala ya kutandika risasi liuwaji kama hilo

Badala yake, anauliwa kijana mwenye njaa tuu, kaiba kuku ili akale na wanae, anatandikwa risasi badala ya kukamatwa ili akajibu makosa yake

Ni lini yataanza kupigwa risasi majizi na mauwaji ya wananchi haya yanayoiba kodi zetu ambapo zingewezesha upatikanaji wa huduma nzuri mahospitalini na kuweza kupatiwa bima kwa watanzania wote?

La hatutaki kuwashuti hawa wezi wa mabilioni yetu, tusiwauwe na hawa wanaoiba Mchele ili wakakidhi njaa zao
 
Watanzania ni wajinga ,na ujinga huo wamejazwa na CCM yaani wezi wa tozoooo wanasifiwa wezi wa pikipiki wanapigwa risasi huku vijana Kwa wazee wakisifiana kuwa huyu aliyeiba fedha nyingi ni mtu mzuri ,watanzania acheni ubinafsi tubadilike tunagawanywa kama paka na CCM huku wao na watoto wao wakisoma shule za ulaya
 
Wezi wa mabilioni hawashiki mapnaga na kuua wasio na hatia,wezi wa mabilioni hawakato watoto wachanga miguu kisa kupora simu. Acheni kutetea upumbavu
Ila ni upumbavu pia kumtetea MTU anayeiba hela huku watu wanahitaji madawa na huduma za afya bora,wanakufa Kwa kukosa Barabara nzuri za kuwafikisha vituo vya afya,wanapata shida Kwa kukosa maji Safi na salama ya uhakika,wafanyakazi kulipwa hela kidogo ila huku watu wengine wakiiba mabilioni ya hela.
 
Wezi wa mabilioni hawashiki mapnaga na kuua wasio na hatia,wezi wa mabilioni hawakato watoto wachanga miguu kisa kupora simu. Acheni kutetea upumbavu
Mkuu samahani kwako wewe wezi wa mabilioni wapo sahihi na wala wizi wao hauna madhara ?

Nchi hii kweli nimeamini wananchi wake wamejaa roho mbaya saana ,unawezaje kuhalalisha wizi wa mabilioni ambayo ilikuwa inaweza kwenda kujenga vituo vya afya ama kununua madawa hospitalini.

Hujawahi kujiuliza vifo vinavyosababishwa na ukosefu wa huduma kuwa mbali ama ukosefu wa dawa vipi vingapi ?
 
Kundi la vijana wanaojulikana kama Panya road' limekuwa ni tishio kwa wananchi kwa siku za hivi karibuni!

Vijana hawa wamekuwa wakitishia usalama wa jamii na hata kufanya mauwaji mbalimbali kwa lengo LA kuiba na kupora kila kilicho mbele ya macho yao!

Tunapenda kulishukuru Jeshi la police kwa kuanza kudhibiti hawa vijana na kuanza kurudisha amani katika mitaa iliyokuwa ikivamiwa Mara kwa Mara kwa kuwakamata hawa vijana alimarufu kwa jina la Panya road

Mbali na kuwakamata, wengine wamekuwa wakipigwa risasi na kufa papo hapo, adhabu hii ndiyo inayopelekea kuuliza juu ya wezi wa Mabilion ya fedha za kodi za wananchi

Wezi hawa wa kodi zetu, ndio wauwaji wakubwa wa watu wanaokufa kwa kukosa huduma mahospitalini!

Watu wanaokufa kwa kukosa gari la wagonjwa ili tu kuwahi huduma katika hospital zetu kuu!

Wajawazito wanakufa kutokana na mtu mmoja tu kuiba kodi ambazo zingeondoa kero hiyo, halafu police wetu wana ng'aa ng'aa sharubu badala ya kutandika risasi liuwaji kama hilo

Badala yake, anauliwa kijana mwenye njaa tuu, kaiba kuku ili akale na wanae, anatandikwa risasi badala ya kukamatwa ili akajibu makosa yake

Ni lini yataanza kupigwa risasi majizi na mauwaji ya wananchi haya yanayoiba kodi zetu ambapo zingewezesha upatikanaji wa huduma nzuri mahospitalini na kuweza kupatiwa bima kwa watanzania wote?

La hatutaki kuwashuti hawa wezi wa mabilioni yetu, tusiwauwe na hawa wanaoiba Mchele ili wakakidhi njaa zao
Subiri wakuvamie na kukucharanga kama fillet ya kitimoto ndio utajua tofauti ya hawa wauaji wanaojiita panya. Kibaya zaidi ukikutana nao hawajui kuwa wewe ndio mtetezi wao unaowatetea nyuma ya keyboard na jina bandia. Elfu kumi tu au simu ya kitochi instosha kuondoa roho yako au kukufanya ķilema mbele ya wavuta bange hao
 
Back
Top Bottom