SI KWELI Papa amesema kuwa Wakatoliki wale chochote wanachokitaka wakati wa Kwaresima kwa kuwa dhabihu haipo tumboni bali moyoni

SI KWELI Papa amesema kuwa Wakatoliki wale chochote wanachokitaka wakati wa Kwaresima kwa kuwa dhabihu haipo tumboni bali moyoni

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Wadau hamjamboni nyote?

Taarifa kamili hapo chini kwa kimombo:

“Eat whatever you want during Holy Week, the sacrifice is not in the stomach but in the heart.

People abstain from eating meat, but they do not talk to their siblings and/or relatives, they do not visit their parents and do not take care of their children.

They do not share their food with those who need it most, they distance their children from their father/mother and/or grandparents, they criticize the lives of others, mistreat their partner, etc. Meat does not make you a bad person, just as a fish fillet will not make you a saint.

Better to seek a good relationship with God by doing good to others. Let us be less arrogant and more humble of heart.”

Pope Francis
1741336417520.png
 
Tunachokijua
Papa Fransisko ni kiongozi wa kanisa Katoliki duniani kote ambaye alianza majukumu yake tarehe 13 Machi 2024 akipokea kijiti hiko kutokea kwa mtangulizii wake Papa Benedict wa 16. Wakristo huwa na mfungo wa siku 40 ukitanguliwa na siku ya jumatano ya majivu ukijulikana kama Kwaresma. Papa Fransisko amekuwa akitoa ujumbe wa pasaka kuanzia mwaka 2014.

Madai

Kumekuwepo na ujumbe unaosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ukieleza kuwa Papa Fransisko ametoa ujumbe wake katika mfungo wa kwaresima akiwataka watu wale chochote katika kipindi hiki kwani mfungo siyo kufunga kula bali ni moyoni.

“Kula chochote unachotaka katika Wiki Takatifu, dhabihu haiko tumboni bali moyoni.

Watu wanajizuia kula nyama, lakini hawaongei na ndugu zao, jamaa zao, hawatembelei wazazi wao na hawawatunzi watoto wao.

Hawagawi chakula chao kwa wale wanaohitaji, wanawatenga watoto wao na baba/mama na/au babu zao, wanakemea maisha ya wengine, wanamtesa mwenzao n.k. Nyama haikufanyi wewe kuwa mtu mbaya, vile vile minofu ya samaki haitakufanya kuwa mtakatifu.

Afadhali kutafuta uhusiano mzuri na Mungu kwa kuwatendea wengine mema. Hebu tupunguze kiburi na tuwe wanyenyekevu zaidi wa moyo.”


Uhalisia wa Ujumbe huo

JamiiCheck imefuatilia na kubaini kuwa ujumbe huu unaosambazwa haujawahi kutolewa na Papa Fransisko na hivyo si wa kweli. Kupitia ufuatiliaji wa wa Jumbe za pasaka alizozitoa Papa kuanzia mwaka 2014 tumebaini hakuna ujumbe ambao papa aliongelea swala la watu kula chochote kipindi cha kwaresima. Tazama hapa kuona jumbe za papa Francis kuhusu kwaresma kuanzia mwaka 2014.

Ufuatiliaji pia umebaini kuwa ujumbe huo umekuwepo tokea Februari 2024, kutokea katika mtandao wa Facebook na baadae kusambazwa katika mitandao mingine ya ikiwemo X zamani, Twitter.

Ujumbe wa papa kuhusu kwaresima kwa mwaka 2025 kwenda kwa wakatoliki uliotolewa Februari, 6 una kichwa kinachosema “Tusafiri kwa pamoja kwa matumaini” ambapo katika ujumbe huo ameeleza ni kwa namna gani waumini wanaweza kushiriki katika safari ya matumaini. Tazama hapa
Wao wakila kitimoto sio shida ila walikuta mtu anakula Punda, Mmbwa, Panya au Fisi wanaanza kumsema vibaya sijui wanatumia andiko gani?
 
Wanafunga waislamu tu?!!!

Vipi mkuu ndugu yangu. Umeshiba makande sasa unakurupuka TU.
Walokole hawafungi?
Walutheri hawafungi?
Wahindu hawafungi?

Mbona huwaga mnajishtukia sana!??
Tupunguze unafiki angalau kipindi hiki cha Kwaresma!
 
Wao wakila kitimoto sio shida ila walikuta mtu anakula Punda, Mmbwa, Panya au Fisi wanaanza kumsema vibaya sijui wanatumia andiko gani?
Hii ni biblia:

📖 Marko 7:18-19
"Akawaambia, Hivi nanyi bado hamwelewi? Hamjui ya kuwa chochote kilichoingia ndani ya mtu kutoka nje hakiwezi kumtia unajisi; kwa sababu hakimwingii moyoni mwake, bali tumboni, naye hutoka kwenda chooni? – Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote."


📖 Matendo 10:13-15
"Kisha sauti ikamjia, Simama, Petro, uchinje ule. Lakini Petro akasema, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi. Sauti ikamjia mara ya pili, Vilivyo safi vilivyotakaswa na Mungu, usiviviite wewe najisi."


📖 Warumi 14:3
"Yeye alaye asimdharau yeye asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu yeye alaye; kwa maana Mungu amemkubali."


Kwa maandiko haya, Yesu mwenyewe alitangaza vyakula vyote kuwa safi, na Mungu alimfundisha Petro asihukumu chakula kwa sheria za Agano la Kale. Kwa hivyo, kula kitimoto si tatizo kwa mtu aliye huru katika Kristo. Kila mtu ana uhuru wa kula au kutokula kulingana na dhamiri yake.
 
Back
Top Bottom