Papa Francis amteua Padre Romanus Elamu Mihali wa Jimbo la Mafinga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Iringa

Papa Francis amteua Padre Romanus Elamu Mihali wa Jimbo la Mafinga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Iringa

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Baba Mtakatifu Fransisko ameridhia ombi la kustaafu Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa, na kumteua Padre Romanus Elamu Mihali wa Jimbo la Mafinga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Iringa, leo tarehe 28/01/2025.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali, alizaliwa tarehe 10/06/1969 Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Baada ya masomo na majiundo ya kipadre, alipewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 13/07/2000 Jimboni Iringa, na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume Jimboni Iringa. Mnamo mwaka 2010 alitunukiwa Shahada ya Uzamili, katika fani ya Sayansi ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kerala nchini India.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali tangu mwaka 2024 hadi sasa, amehudumu nafasi ya Makamu wa Askofu kwa Waklero Jimboni Mafinga.

Aidha, Mhashamu Askofu Mstaafu Tarcisius Ngalalekumtwa atakuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo la Iringa, hadi Askofu Mteule atakapowekwa Wakfu na Kusimikwa Jimboni humo.

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, linamwombea Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali afya ya mwili na roho katika utume huo mpya.

Imetolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

IMG-20250128-WA0003.jpg
 
Baba Mtakatifu Fransisko ameridhia ombi la kustaafu Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa, na kumteua Padre Romanus Elamu Mihali wa Jimbo la Mafinga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Iringa, leo tarehe 28/01/2025.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali, alizaliwa tarehe 10/06/1969 Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Baada ya masomo na majiundo ya kipadre, alipewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 13/07/2000 Jimboni Iringa, na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume Jimboni Iringa. Mnamo mwaka 2010 alitunukiwa Shahada ya Uzamili, katika fani ya Sayansi ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kerala nchini India.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali tangu mwaka 2024 hadi sasa, amehudumu nafasi ya Makamu wa Askofu kwa Waklero Jimboni Mafinga.

Aidha, Mhashamu Askofu Mstaafu Tarcisius Ngalalekumtwa atakuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo la Iringa, hadi Askofu Mteule atakapowekwa Wakfu na Kusimikwa Jimboni humo.

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, linamwombea Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali afya ya mwili na roho katika utume huo mpya.

Imetolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

View attachment 3216497
Hongera baba
 
Baba Mtakatifu Fransisko ameridhia ombi la kustaafu Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa, na kumteua Padre Romanus Elamu Mihali wa Jimbo la Mafinga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Iringa, leo tarehe 28/01/2025.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali, alizaliwa tarehe 10/06/1969 Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Baada ya masomo na majiundo ya kipadre, alipewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 13/07/2000 Jimboni Iringa, na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume Jimboni Iringa. Mnamo mwaka 2010 alitunukiwa Shahada ya Uzamili, katika fani ya Sayansi ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kerala nchini India.

Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali tangu mwaka 2024 hadi sasa, amehudumu nafasi ya Makamu wa Askofu kwa Waklero Jimboni Mafinga.

Aidha, Mhashamu Askofu Mstaafu Tarcisius Ngalalekumtwa atakuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo la Iringa, hadi Askofu Mteule atakapowekwa Wakfu na Kusimikwa Jimboni humo.

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, linamwombea Mhashamu Askofu Mteule Romanus Elamu Mihali afya ya mwili na roho katika utume huo mpya.

Imetolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

View attachment 3216497
Hongera sana kwake
 
Nakumbuka Ngalekumutwa wakati amekuja kukaimu huku kwetu baada ya Mtega kujihudhuru,. Siku ya kipaimara alitukalisha kanisani hadi jioni sanaaa yani niseme tu ulikuwa usiku,. Hatukurudi hata nyumbani kusherekewa nilikasirika kweli😑😑
 
Nakumbuka Ngalekumutwa wakati amekuja kukaimu huku kwetu baada ya Mtega kujihudhuru,. Siku ya kipaimara alitukalisha kanisani hadi jioni sanaaa yani niseme tu ulikuwa usiku,. Hatukurudi hata nyumbani kusherekewa nilikasirika kweli😑😑
Alikuwa mtemi sana

Walio enda kwa mwamposa wote alimwambia waungame zambi hiyo ya kwenda kwa mwamposa

Alifaa kuwa kadinali huyu
 
Kwa njia yake yeye pamoja naye na ndanii yake

Wewe Mungu baba Mwenyezi katika umoja wa Roho Mtakatifu unavitia vitu vyote heshima na utukufu ....

Eeh bwana ulikumbuke kanisa lako linalosafiri hapa duniani..... Ulikamilishe katika upendo pamoja na Umkumbuke Baba Mtakatifu wetu , maaskofu, mapadri na maklero wote

KWa wema usikilize Sala za jamaa
Iliyokusanyika mbele yako kwa maombezi ya bikra maria mama Mungu na Mtakatifu Yosefu mchumba pamoja na watakatifu waliokupendeza tangu hapo kale...

Uwakumbuke ndugu zetu waliofariki wakiwa na tumaini la kukutana nawe

Hiki kipande nakipenda sana nakuwa na utulivu mno japo Kuna maneno nimeruka!! sikumbuk yote!
 
Back
Top Bottom