Papa Francisco aridhia ombi la Askofu Telesphor Mkude wa Jimbo Katoliki Morogoro kung'atuka kutoka madarakani

Wakatoliki naomba mnijibu 1.Padri wa RC anastaafu akiwa na miaka mingapi?

2.Kwanini askofu anazikwa Kanisani,baada ya miaka kadhaa kanisa si linaweza kujaa makaburi ya maaskofu?
Upadre ni wa kudumu, wa maisha! Uaskofu pia vile vile, ukisikia askofu amestaafu ujue tu kaacha majukumu ya kuongoza jimbo lakini daraja lake la uaskofu lipo pale pale.

Askofu anazikwa pale anapochagua yeye, kuzikwa kanisani ni sehemu tu ya utamaduni wa kanisa wa kumhifadhi kiongozi wao wa muda mrefu katika makao yake makuu, yaani kanisa lake kuu.

Kuhusu kujaa kwa makaburi, makanisa ya wenzetu huko nje yanakua designed na chembers za kutosha kwa kazi hiyo, huku kwetu bado hatujamaliza nafasi zilizopo. Na uwezekano ni kuwa huenda zikapatikana nafasi kwa njia ya kuchimba underground, huu ni mtazamo wangu.
 
Hata mfumo wa jumuiya nao wameanza kuiga hivi karibuni
 
Huyo siyo mlutheri ni wale wapinga kambale, Bata, na mbuzi wetu pendwa
Ha ha ha ha na wao huwa wanatumia washarika kumbe? Yaani naogopa kuongea kwa confidence hv jamani. Khaaa.... huwa wasabato waliona sehemu ya kutoboa ndo wapitie kwetu?

Mwambie Jumamosi ni siku tulizochagua za kumsifu Mungu, kujuana zaidi, kusaidiana kwa karibu na kushirikiana. Hii siku hutumika kwakua ndo siku ambayo wengi wetu hupata nafasi ya kuabudu hizi Jumuiya. Miaka ya 90 tulikua tunasali Alhamis. Kuna wengine Jtano. Na hata sasa kuna ambao wana siku yao ambayo kwao ni rahisi kukutana.
 
Huu utaratibu wa KKKT kusali Jumuia siku ya Jumamosi unanikera sana yani!

Umehangaika kila siku kuamka saa 11 kuwahi kibaruani ukitarajia Jumamosi walau upumzike na Jumapili walau uamke saa nne uende ibadani, lakini kanisa likaona litunyang'anye hata siku moja tu ya Jumamosi kupumzika kwa kuwa na ibada za kijumuia!

Sasa kama nitasali na kutoa sadaka Jumamosi, Jumapili niende kanisani kufanya nini?...yani niwe na siku mbili za kuabudu?

Huku kwenye Jumuia ndipi sehemu Kanisa limewekeza nguvu katika kukufanya sadaka na Michango ya miradi mbalimbali ya kanisa!...yani huchomoki!

Baada ya kusali ni maelezo ya kiasi gani mtaa unadaiwa pesa za kufanikisha hostel au gari la Mchungaji!...inaudhi na Jumapili kanisani sadaka na michango ileile inatolewa tena!

Ni kweli kabisa linatakiwa likue, lakini kukua kwa kanisa kusiendane na kupotea kwa "Misingi" ya kanisa!
 
Unajua kuhusu muda wa kusali ni wanajumuiya wenyewe kuamua si lazima asubuhi. Enzi hizo tulikua tukisali jioni.

Waluther mulichelewa sana kujua njia ya jumuiya jinsi ilivyo rahisi kukusanya michango[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] poleni na hongereni sana. Yaan mimi nazaliwa naukuta huu utaratibu. 90s tunasali na chai ya maandazi kabisa tunakunywa mpk early 2000s. Hapa tuu parokia ya kimara tumeshajitenga kuna eneo tumenunua huku korogwe. Licha ya kwamba tuna kigango kizuri mno. Tumenunua eneo kubwa mil 500. Na ni hivi wauzaji wamejua ni roman tunanunua basi wanataka mpunga huo. Kimbo wametupa mil 300. The rest ni jumuiya sasa za korogwe hapa na bucha. Basi tulivyo wachache jumuiya yetu we acha tu. Sijui ndo mil ngapi hata sikumbuki maana sijahudhuria jumuiya recently. Yaan hutoboi. Utatoa tu. Acha kuchangia sasa ukakumbane na ya Ruge kuzikwa na katekista[emoji23][emoji23] na hakuna kanisa lina msimamo kama Roman. Yaan wakikutema wamekutema yaan hawaangalii ni nani. Kingunge naye si alizikwa na katekista? Ni kwakua hawaishi ukatoliki. Yaan maswali yanaulizwa, alikua akihudhuria jumuiya? Hapana. Zaka unatoa? Hapana. Michango ya junuiya? Hapana. Maswali ya kutosha. Halaf hapo mwishon ubaulizwa, je kwa majibu haya mhusika anastahili kupata huduma ama hastahili[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119] yaan utapata aibu mwenyewe. Bashite si aliendaga muombea ruge kuzikwa na kanisa? Unajua alijibiwaje? Heshima sana kwa Roman kwa hili. Hawaangalii asilani nani ni nani. Utapata huduma kutokana na ulivyoishi ndani ya imani yako. Ndo maana bado kanisa limesimama mpaka kesho. Yote hii ni kusimamia principals zao
 
Mie Jumuia siiipendi kwa kweli!...umbea umbea tu!
 
Hivi mkuu monsinyori rev Patrick Kung'alo bado yupo jimboni? Nakumbuka alikuaga monsinyori huko Morogoro baada ya kutoka kua rector wa seminari flani ya jimbo hapo Moro
 
Kwani akizikwa na katekista kuna utofauti akizikwa na Papa achilia mbali askofu?
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787], mkuu nimeipenda hii. Haswa huyo Happy, ni nani mkuu? Tuhabarishe maana..........!
 
Kwani akizikwa na katekista kuna utofauti akizikwa na Papa achilia mbali askofu?
Mkuu... ikiwa wewe si wa Imani hii wala huhitaji kuhangaika kujua sana. Ila hakuna mkatoliki anayetaman kuzikwa hivyo. Tofauti ipo kubwa sana. Unapewa huduma accordingly kwa jinsi ulivyohudumika na kuishi ukatoliki wako. Umekua muumini wake kwa kukubali kufata matakwa ya kanisa. Na kila mmoja anajua afanye ninu ili iweje. Hao hawakuuishi ukatoliki ipasavyo. Kwakua ndo walikua wanarudi kundini na ziko ngazi kwa ngazi basi ndo huduma waliyostahili
 
Kwa wakatoliki hakuna sharika
 
Afrika imejaa Vimbwaga na bado vinaendelea kushamiri kama Nyasi au Magugu yaliyoko kwenye Chemichemi wakati Viongozi wa Dini wanaamua kustaafu huku Viongozi wa Kisiasa wao wanaona ndio fursa wanadhiriki hadi kuvunja Katiba ili waendelee kutawala kimabavu. Ahsante Askofu Mstaafu Telesphor Mkude kwa Utumishi wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…