Paroko kizimbani kwa tuhuma za wizi

Paroko kizimbani kwa tuhuma za wizi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Paroko.jpg
Paroko wa Parokia ya Haydom, Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara, Bartazari Margwe Sule (63) amefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Manyara kwa tuhuma za kuiba zaidi ya shilingi milioni 20 kwenye akaunti ya kaka yake, Dionice Margwe Sule ambaye inadaiwa kuwa ni mgonjwa wa kupoteza kumbukumbu.

Inaelezwa kwamba fedha hizo anazotuhumiwa kuziiba zimetokana na mirathi ya shemeji yake.

Kesi hiyo namba 44 ya mwaka 2022 imesomwa na hakimu Mariam Luselwa katika Mahakama ya Mkoa wa Manyara.

Kesi hiyo inawakabili washtakiwa wa tatu ambao ni Sule pamoja na watumishi wawili wa Benki ya NMB, Cynthia Nyamtiga (27) na Winfrida Rwakilomba (30) kwa pamoja wametajwa mahakamni hapo kuhusika na kesi hiyo.

Imeelezwa Mahakamani hapo, Paroko Baltazari anakabiliwa na makosa mawili, kosa la kwanza wizi kinyume na kifungu namba 258 kifungu kidogo cha kwanza na kifungu namba 265 vya kanuni ya adhabu sura namba 16 marejeo kama ilivyofanyiwa marejeo ya 2022.

Washtakiwa wengine ni watumishi wawili wa Benki ya NMB, Cynthia Nyamtiga pamoja na Winfrida Rwakilomba, ambapo Hakimu Mariam Luswelwa ameiambia mahakama washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na kosa la kushindwa kuzuia utendekaji wa kosa kinyume na kifungu 383 na kifungu cha 35 vya kanuni ya adhabu sura 16 kama ilivyofanyiwa marejeo 2022.

Washtakiwa hao watatu wamekana kutenda mashtaka yanayowakabili wote watatu wapo nje kwa sharti la kuwa na mdhamini mmoja kwa kila mshtakiwa na bondi ya milioni saba kwa kila mdhamini.

Shauri hilo limepangwa tena tarehe Desemba 21, 2022 kwa ajili ya kusomewa hoja za awali.

Chanzo: EATV
 
Inabid hata huku kanisani tuanze kuwashitak hawa m wa

Unakuta huku kanisani account mbalimbali wanazisimamia wao,ikitokea kuna mapungufu ya pesa viongoz wa kikundi ndo wanawajibika,lenyewe unakuta lipo tu limejibanza hakuna anaeweza kulisema maana waumini wote wanalinyenyekea
 
Paroko wa Parokia ya Haydom, Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara, Bartazari Margwe Sule (63) amefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Manyara kwa tuhuma za kuiba zaidi ya shilingi milioni 20 kwenye akaunti ya kaka yake, Dionice Margwe Sule ambaye inadaiwa kuwa ni mgonjwa wa kupoteza kumbukumbu.

Inaelezwa kwamba fedha hizo anazotuhumiwa kuziiba zimetokana na mirathi ya shemeji yake.
Ajabu sana. paroko anatunzwa na kanisa. hana mke wala watoto lakini anaiba pesa, anazipeleka wapi? au ana familia ya siri?
 
Acheni kuhukumu huu ni upande mmoja wa Taarifa umeshamsikia Yeye akitoa hoja zake?

Mnakumbuka Yule shekhe wa Arusha aliposingiziwa kuwa amebaka watoto wengi kwenye madrasa yake watu tulimtukana sana
Baadae ikajajulikana ni watu walikuwa wanamsingizia Tena walimu washule ya Msingi?

Kuna Padri mmoja Moshi kibosho alipata kesi ya kubaka na ikifika mahakamani kumbe tuu Padri wa watu wa Rombo baadhi ya watu walimtupia kashfa kwakuwa hawampendi

Tuweni makini sana kuwahukumu watu ni kama vile wewe mtaani au ofisini watu wanapokutupia maneno machafu ambayo wala hauna
 
Back
Top Bottom