Part II: Bado safari yangu ya kusaka utajiri wa nguvu za giza inaendelea

Part II: Bado safari yangu ya kusaka utajiri wa nguvu za giza inaendelea

Status
Not open for further replies.
Hata wewe ulpozaliwa hukutokea bure, kuna kazi ilifanyika kubwa. In my world everything comes with a price.
Vizuri kwamba unafahamu hilo. Na huko utakapopewa utajiri uwezekano ni mkubwa mbeleni wakatataka vya kuzaliwa, hivyo hakikisha unafanya kazi haswa uwe na stock ya kutosha.
 
Mimi nimeshafanikiwa, ila Jibu swali, ni lazima au kuna ulazima wa kuleta mirejesho? Je kila kitu kinafaa kuleta mrejesho?! Itakusaidia nini kuujua mrejesho ilihali sio member, freemason wana msemo wao mzuri sana naupenda unasema "to be one, ask one".
Kwa muandiko huu ni dhahiri bado hujafikia lengo.
Na kutakia mafanikio mema.
 
Kama ambavyo awali nilikwisha jitokeza kuomba 'Connection' ya mtaalam au wataalam wa ndagu za utajiri au utajiri wa nguvu za giza.

Nasikitika kusema kuwa bado sijapata haswa sehemu ambayo mhusika anaweza kunishika mkono kunipeleka au kuwa kama 'Godfather' kuniinguza katika ufalme huo wa giza haswa kupata utajiri.

Mwanzoni uzi wangu nilishuhudia walioniunga mkono, nilipata madalali wengi, matapeli pia walikuepo, wachache walionielekeza sehemu asilimia kubwa nilikuta mtaalam amehama / kufariki kwahio kuniwia vigumu.

Najua pia ilivyo ngumu mtu kuamini haswa kwa dhati kwamba huyu mtu kweli anataka kuchukua njia hio na kupelekea hata aliyekua na connection au alie upande huo kuwa na ugumu sana kukupa connection. Wengine tu hawataki, hakuna sababu maalum lakini hawataki tu na huwezi kumlazimisha.

Mimi bado naendelea na safari yangu ya kuutafuta utajiri wa nguvu za giza au ufalme wa giza, hakuna ubaya katika hilo, ni imani kama imani nyingine, umasikini ni laana, umaskini hauzoeleki, siutaki umaskini, nimeulaani umaskini, na mpendwa wangu Lucifer alisema wazi kuwa ukinisujudia nitakupa mali zote za dunia hii, nami nataka ku claim hiyo power.

Hivyo naendelea kujitokeza kwa wale ambao wataweza kunisaidia kunipa.connection ya UHAKIKA ama kunipeleka basi waweze kunisaidia katika hilo.

Hail Lucifer!

ANGALIZO: Wale walokole na wafia dini nawaomba mtulie, siwahitaji kwenye uzi wangu.
Mtafute Lwanda magere akupe connection
 
Hao unaowasemea ni wahuni wavuta bangi wale wanaobandika matangazo barabarani au wanaotuma msg za kitapeli. Kama wana nia kweli they should keep searching and searching bila kuchoka until they will find my dearest devil and give them what they want and in return they will offer what they have. Simple!
90% ya watz wanaserch still not yet thus Ingekuwa ni rahisi watz wengi wangekuwa matajiri
 
Utajiri wa dini ya nguvu za Giza sio wa kila mtu jombaa, it's not childs play. By the way lini umefanya sensa ya kujua tuna mamilionea wangapi na vyanzo vyao vya utajiri ni vipi bila kupepesa macho.
Waafrika uamini shortcut ya waganga.
Mungu umpa mtu kwa wakati wake ukifika, Hakuna cha mganga wala kuombewa,vyote hivyo wengi wamefanya,ufanya still maisha yao ni magumu
 
Yule kuku wa mbeya bado yupo, alivuma sana mwanzoni mwa miaka ya 2000, vijana wengi wameondoka kupitia yeye
Uko utajiri ila wa punje uko tayari!!?[emoji1787]

Yaani kuku anatengewa punje idadi atakayokula ni miaka yako ya kuishi baada ya kupewa miburungutu ya fwedha.

Akila punje 5 utafaidi hizo hela kwa miaka 5 tu na hela hela kwei sio vijihela
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom