To yeye
JF-Expert Member
- Oct 4, 2022
- 35,686
- 86,968
Angeweka karoti bhanaUme[emoji2089][emoji2089]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Angeweka karoti bhanaUme[emoji2089][emoji2089]
Kwani Mwanakerekwe pacha wa Kizimkazi ishakuwa nchi kamili?Nikirudi tz nitakuja kutembea
Zamani tulikuwa tunasimuliwa kuwa hilo eneo lilikuwa kavu tu yaani lilikuwa halina maji. Ikatokea siku moja Mtu mmoja wa Kabila la Wakinga alikuwa safarini alipita hayo maeneo akiwa na kiu ya maji na njaa, akawaomba watu wa eneo hilo wampe chakula na maji wakamtolea nje ila mtu mmoja katika watu wote wa eneo hilo ndiye alimpa chakula na maji Mkinga huyo. Basi mara baaada ya kupata chakula na kunywa maji Mkinga akamwambia mwenyeji wake huyo ahame eneo hilo maana atawaangamiza wale watu wote waliomnyima chakula na maji. Ndio ikatokea hivyo wakaangamizwa kwa kuletewa maji na kuzamishwa kwenye maji hayo. Ndio ukawa mwanzo wa hiyo kitu Kisiba. Hizo zilikuwa simulizi za Bibi zetu enzi hizo. Funzo la simulizi hiyo ni kuwa Tusiwe Wachoyo hasa kwa Wageni.Mm hilo ziwa kwa story zake nimetokea kuliogopa..sijui kwanini..huwa naona kibao cha kuelekeza uelekeo wake..mwaka huu naweza kuja na familia tupaone panafananaje..
Vintage wine.....View attachment 2889323
Hiyo wine ihifadhi tafadhali, acha iendelee kuchachuka, nikija Daslam ntawakaanga prawns pembeni mihogo ya coco na kachumbari kisha tunashushia mvinyo uliokaa.
Hivi kwani Wanyakyusa ni wachoyo?Zamani tulikuwa tunasimuliwa kuwa hilo eneo lilikuwa kavu tu yaani lilikuwa halina maji. Ikatokea siku moja Mtu mmoja wa Kabila la Wakinga alikuwa safarini alipita hayo maeneo akiwa na kiu ya maji na njaa, akawaomba watu wa eneo hilo wampe chakula na maji wakamtolea nje ila mtu mmoja katika watu wote wa eneo hilo ndiye alimpa chakula na maji Mkinga huyo. Basi mara baaada ya kupata chakula na kunywa maji Mkinga akamwambia mwenyeji wake huyo ahame eneo hilo maana atawaangamiza wale watu wote waliomnyima chakula na maji. Ndio ikatokea hivyo wakaangamizwa kwa kuletewa maji na kuzamishwa kwenye maji hayo. Ndio ukawa mwanzo wa hiyo kitu Kisiba. Hizo zilikuwa simulizi za Bibi zetu enzi hizo. Funzo la simulizi hiyo ni kuwa Tusiwe Wachoyo hasa kwa Wageni.
Bahati mbaya Bibi alishafariki ningemuuliza anipe ukweli.Hivi kwani Wanyakyusa ni wachoyo?
Carrot si ndogo hiyo unapenda size ya kidole hufaidi🤣🤣Angeweka karoti bhana
Vintage wine.....
Njoo Dar, Njooo
Hii ndio swimingi yenyewe au hili ni ziwa.
Hebu taja majira rafiki bhana manake Rungwe na yenyewe ina sifa sana manake usikute kuna majira ukipiga mbizi, unaanza ku-freeze huko huko ndani.
Mwezi wa sita na wa saba ndio kuna baridi sheikh. Pasaka haiwi miezi hiyoHebu taja majira rafiki bhana manake Rungwe na yenyewe ina sifa sana manake usikute kuna majira ukipiga mbizi, unaanza ku-freeze huko huko ndani.
Klariti ndio kalikiti?Hii ndio swimingi yenyewe au hili ni ziwa.
Bandiko halina klariti.
Nilitaka kukujibu lakini baada ya kuona unatumia tecnonf7 nimeghairiKwani Mwanakerekwe pacha wa Kizimkazi ishakuwa nchi kamili?
Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
ClarityKlariti ndio kalikiti?
MashallahInshallah....🙏.
Mbeya never disappoint ni vile Utalii wa Tanzania wamekariri huko Arusha
Kisiba Campsite Ni Eneo la Kitalii linalopatikana Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Shughuli unazoweza kufanya, Uwapo eneo la kisiba unaweza kufanya shughuli mbalimbali za kitalii ikiwemo kuogelea (Swimming) kupumzika , Kuendesha boti la muanzi (canoeing with bamboo boat) matembezi ya kulizunguka ziwa, kupunga upepo, matembezi ndani ya msitu wa Kisiba, lakini pia mtalii anaweza kufurahia kufanya kambi.
Ukiachana na muonekano wa eneo hili la kitalii, pia ni eneo mojawapo lililojaa masimulizi mbalimbali ya wajerumani ikisadikika kwamba ndani ya ziwa hili wajerumani waliweza kutupa vitu vyao vya Thamani.
Vivutio vya kitalii vilivyo Karibu, Kisiba campsite pia iko karibu na vivutio mbalimbali vya kitalii ambapo mtalii akilala hapa ataweza kuvitembelea kwa uharaka sana ikiwemo, Maporomoko ya Maji Kapologwe, Majengo ya kale ya Wajerumani, Mti mkubwa wa katembo ambao unauwezo wa kuzungukwa na watu nane (8) mpaka kumi na mbili (12), Maji moto pamoja na maziwa mengine yaliyotokana na milipuko ya kivolkeno kama (Ziwa Ikapu, kyamba ngungulu, Itende, Ilamba, Kiungululu na Kingili lakini pia ni miongoni mwa njia fupi na ambazo utaweza kuona vivutio Vingi kuelekea Ziwa Nyasa (Matema Beach)
Namna ya Kufika, Kisiba Campsite inafikika kirahisi sana kwa usafiri binafsi unaweza kuingilia Tukuyu Mjini ama Ushirika pana umbali wa kilomita 18, lakini kwa usafiri wa Uma unaweza kushukia Tukuyu Mjini kisha ukapanda Noah zinazoelekea Lwangwa ama Itete Nauli Tsh 4,000/=, kwa pikipiki ni Tsh 7000/= mpaka 10,000/=
KARIBU TUKUYU RUNGWE KARIBU MBEYA TANZANIA
Umeona ehhMbeya never disappoint ni vile Utalii wa Tanzania wamekariri huko Arusha