Pasaka hii twende tukapumzike Kisiba Campsite. Hautojutia, wewe na umpendaye

Pasaka hii twende tukapumzike Kisiba Campsite. Hautojutia, wewe na umpendaye

Mm hilo ziwa kwa story zake nimetokea kuliogopa..sijui kwanini..huwa naona kibao cha kuelekeza uelekeo wake..mwaka huu naweza kuja na familia tupaone panafananaje..
Zamani tulikuwa tunasimuliwa kuwa hilo eneo lilikuwa kavu tu yaani lilikuwa halina maji. Ikatokea siku moja Mtu mmoja wa Kabila la Wakinga alikuwa safarini alipita hayo maeneo akiwa na kiu ya maji na njaa, akawaomba watu wa eneo hilo wampe chakula na maji wakamtolea nje ila mtu mmoja katika watu wote wa eneo hilo ndiye alimpa chakula na maji Mkinga huyo. Basi mara baaada ya kupata chakula na kunywa maji Mkinga akamwambia mwenyeji wake huyo ahame eneo hilo maana atawaangamiza wale watu wote waliomnyima chakula na maji. Ndio ikatokea hivyo wakaangamizwa kwa kuletewa maji na kuzamishwa kwenye maji hayo. Ndio ukawa mwanzo wa hiyo kitu Kisiba. Hizo zilikuwa simulizi za Bibi zetu enzi hizo. Funzo la simulizi hiyo ni kuwa Tusiwe Wachoyo hasa kwa Wageni.
 
Zamani tulikuwa tunasimuliwa kuwa hilo eneo lilikuwa kavu tu yaani lilikuwa halina maji. Ikatokea siku moja Mtu mmoja wa Kabila la Wakinga alikuwa safarini alipita hayo maeneo akiwa na kiu ya maji na njaa, akawaomba watu wa eneo hilo wampe chakula na maji wakamtolea nje ila mtu mmoja katika watu wote wa eneo hilo ndiye alimpa chakula na maji Mkinga huyo. Basi mara baaada ya kupata chakula na kunywa maji Mkinga akamwambia mwenyeji wake huyo ahame eneo hilo maana atawaangamiza wale watu wote waliomnyima chakula na maji. Ndio ikatokea hivyo wakaangamizwa kwa kuletewa maji na kuzamishwa kwenye maji hayo. Ndio ukawa mwanzo wa hiyo kitu Kisiba. Hizo zilikuwa simulizi za Bibi zetu enzi hizo. Funzo la simulizi hiyo ni kuwa Tusiwe Wachoyo hasa kwa Wageni.
Hivi kwani Wanyakyusa ni wachoyo?
 
Hebu taja majira rafiki bhana manake Rungwe na yenyewe ina sifa sana manake usikute kuna majira ukipiga mbizi, unaanza ku-freeze huko huko ndani.
Mwezi wa sita na wa saba ndio kuna baridi sheikh. Pasaka haiwi miezi hiyo
 
Hujazungumzia malazi na chakula ? Au lazima sisi watalii tufanye day trip na lunch box zetu?
 

Kisiba Campsite Ni Eneo la Kitalii linalopatikana Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Shughuli unazoweza kufanya, Uwapo eneo la kisiba unaweza kufanya shughuli mbalimbali za kitalii ikiwemo kuogelea (Swimming) kupumzika , Kuendesha boti la muanzi (canoeing with bamboo boat) matembezi ya kulizunguka ziwa, kupunga upepo, matembezi ndani ya msitu wa Kisiba, lakini pia mtalii anaweza kufurahia kufanya kambi.

Ukiachana na muonekano wa eneo hili la kitalii, pia ni eneo mojawapo lililojaa masimulizi mbalimbali ya wajerumani ikisadikika kwamba ndani ya ziwa hili wajerumani waliweza kutupa vitu vyao vya Thamani.

Vivutio vya kitalii vilivyo Karibu, Kisiba campsite pia iko karibu na vivutio mbalimbali vya kitalii ambapo mtalii akilala hapa ataweza kuvitembelea kwa uharaka sana ikiwemo, Maporomoko ya Maji Kapologwe, Majengo ya kale ya Wajerumani, Mti mkubwa wa katembo ambao unauwezo wa kuzungukwa na watu nane (8) mpaka kumi na mbili (12), Maji moto pamoja na maziwa mengine yaliyotokana na milipuko ya kivolkeno kama (Ziwa Ikapu, kyamba ngungulu, Itende, Ilamba, Kiungululu na Kingili lakini pia ni miongoni mwa njia fupi na ambazo utaweza kuona vivutio Vingi kuelekea Ziwa Nyasa (Matema Beach)

Namna ya Kufika, Kisiba Campsite inafikika kirahisi sana kwa usafiri binafsi unaweza kuingilia Tukuyu Mjini ama Ushirika pana umbali wa kilomita 18, lakini kwa usafiri wa Uma unaweza kushukia Tukuyu Mjini kisha ukapanda Noah zinazoelekea Lwangwa ama Itete Nauli Tsh 4,000/=, kwa pikipiki ni Tsh 7000/= mpaka 10,000/=

KARIBU TUKUYU RUNGWE KARIBU MBEYA TANZANIA
Mbeya never disappoint ni vile Utalii wa Tanzania wamekariri huko Arusha
 
Back
Top Bottom