Niombe wasomaji wangu muelewe kuwa sina nia mbaya ninapojaribu kuja na uchambuzi wa namna hii. Lengo langu ni kuoneshana kuwa nchi yetu iko hatarini hasa pale taaluma moja ambayo Taifa linawategemea wanaposigana katika jamii nani anayeumia zaidi!
Nakumbuka siku za hivi karibuni gazeti la the Economist lilikuja na habari ambazo Mkuu Pascal aliziita kuwa ni habari za uongo dhidi ya Rais wetu wa Tanzania.
Gazeti ilo liliwahi kuja na habari kuwa "Rais wa Tanzania hapendi kukosolewa"
Gazeti ilo baada ya kuchapishwa Pascal Mayalla alikuja na bandiko la kupinga habari ile huku akionesha jinsi ambavyo sio kweli Rais wetu anapenda kukosolewa.
Alikwenda mbali zaidi akamnukuu Rais wetu kuwa aliwahi kuwaambia wanahabari kuwa yeye anapenda kukosolewe ila akosolewe kwa Staha na kwa hoja.
Pascal Mayalla kwenye andiko lake anatolea mfano kuwa yeye Pascal Mayalla ni moja ya wanahabari ambao waliwahi kumkosoa Rais na Rais alikubali kukosolewa kwa kumjibu huku akimtania.
HOJA.
Kwanza lazma watu mjue kuwa andiko la Pascal kupinga habari ya the Economist ndio iliyoamsha watu na kuanza kufuatilia ni nani na yuko wapi anae ripoti habari hizo katika gazeti la the Economist?
Hapa naomba nieleweke,hata watumishi idara nyeti walianza kufatilia gazeti ilo baada ya kusoma bandiko la Pascal Mayalla hapa JF, na ndipo wakaja kugundua kuwa kumbe mwandishi wa habari zile na nyeti kupitia gazeti lile ni ndugu yetu Erick Kabendera.
Kwanini walifuatilia,kiukweli kilichoandikwa na mwandishi huyo wa habari kilikuwa na ukweli wa 100%ingawa huyu Ndugu Mayalla alikipinga kwa lengo la kujipendekeza kwa msukuma mwemzake.
Je, Pascal Mayalla alijua tangu awali kuwa Kabendera ndie anayeandika habari nyeti na kuziripoti The Economist na alishindwa kumuita kama mdogo wake na kumpa onyo?
Kimsingi kifungo cha Kabendera nadhani ni furaha kwa Mayalla kwani alimjua tangu awali na alishindwa kabisa kumuita na kumuonya ingawa wote wanatoka kanda ya ziwa.
Je, Pascal alijua Erick akifungwa tegemezi wake watalia na kusaga meno na wengine watajitokeza mitandaoni wakimlilia kwa kukosa hata fedha ya kununua Dawa?
Nadhani yote aliyajua ndio maana tangu Kabendera awekwe korokoloni hajawahi jitokeza popote kulaani kukamatwa kwa kijana huyu zaidi inasemekana ndio kwanza anatafuta makala zote zilizoandikwa huko nyuma na kuzisoma na kuzifafanua kwa vijana wa idara nyeti ili kijana azidi kubanwa.
Andiko la Mayalla dhidi ya kumtetea ndugu yake liko hapa JF linaudhi linaumiza kwani humo ndani anawataja wakosoaji wakubwa wa nchi hii ambao leo hii wamegeuziwa rangi ya unga wa ndere wao wanaita unga mweupe sasa huku wakila kuku kwa mirija.
Nasisitiza waandishi wa habari mtengeni Mayalla na waandishi wote wenye vinasaba vya ukabila na wanaoshindwa kusimamia taaluma badala yake wanaishia kujipendekeza kwa kuhofia uhai wao.
Natoa rai kwa Serikali ya Jamhuri kumwachia huru Kabendera. Tusipomdai kwa kiswahili tutawataka kwa kilugha, na hapo ndipo tutakapozuia kiongozi yeyote kuingia mkoa wa Kagera mpaka "omwana weitu mumutaishure.""
Wewe ni mnafiki, mchawi, mzushi na muuaji kabisa na uzuri umejishtukia sana, tena mno kwenye uzi wako huu
1. Usalama wa Taifa na vyombo vyake vyote vinasoma kila kinachoendelea mitandaoni, magazetini ndani na nje ya nchi, KUSEMA Pascal alikuwa anashadadia ni sawa na kusema vyombo vya usalama vinamtegemea Pascal Mayala??? kuwa hawao hawajui ila wameamshwa na Pascal??? HAPA umekosea
2. JF ni familia kubwa, Pascal MAYALA ni mwanafamilia humu, HAPA tuna dare kuongea kwa uwazi, IKITOKEA KILA MAADA YA mtu humu ikahusishwa na kila kinachoendelea serikalini na uraiani UTAPATA mpaka wachawi humu; wako waliowahi kusema fulani atakufa mwisho wa mwaka na ikawa!! wako waliowahi kusema fulani ajiangalie, na IKAWA, wako waliowahi mpaka kusema mbovu juu ya mahusiano ya wenza wawili na wenza hao uhusiano wao ukafa!!! wako mpaka ambao tushawahi sema waziri fulani hana siku nyingi ofisini na ikawa!!
Pascal alikuwa ana post kwa mawazo yake, na mitazamo wako akiwa kwenye mood zake na uwanja wake binafsi!! kumuhusisha na Kibendera sio sawa kabisa
How come leo unamkaanga member mwenzio? alipotoa ile post that very time uliipinga? ulisema italeta matatizo? HUKUWEZA KUSEMA maana zilikuwa post za kawaida za kila siku kama zingine; umekuja kuwaza baada ya kuanza kutafuta mchawi??? usitafute wachawi humu.. NA NI UKO WARD, haupingi wala hauangaiki Kibenedera atoke, unaangalia nani ni chanzo?? seriously??
akina Maxence wanakesha mahakamani wewe na mimi tuwe huru, watu wanasema chochote na hakuna PERSONAL humu!! weka hoja mezani na usiongee KUFIRIKA kwa ku assume fulani ni mbaya unamchafua..
yakupasa uombe radhi
3. Sidhani kama kila ulichosema wewe katika maisha hakikuwahi kutokea na hakuna aliyekuhusisha nayo, why kwa member mwenzako
Pamoja na uzoefu wako humu ume loose sense of unity, sense of protection unamtoa mwenzako achafuke mtaani, jina lake waliseme vibaya, pengine hata wengine kumuua, KISA umefikiria tu mkuu
zamani humu, tulikuwa na utaratibu wa kuweka attachments, kama proof ya unachokisema...siku hizi imebaki ku assume tu
Nimeamka vizuri leo, ningeingia deep kukufafanua. ACHA hiyo tabia