Patrick Mfugale katika umri wa miaka 71 alikuwa anafanya nini ofisi ya umma?

Ala, kumbe jamaa alitakiwa awe analea wajukuu toka mwaka 2010.
 
Mwacheni apumzike. Haya ulikuwa na uwezo wa kuyasema akiwa hai.
Ni kweli sio vyema kumsema marehemu lakini lipo Jambo la kujifunza au kuuliza hapo kwa faida ya wengi. Kwa sababu ilkuwa sio rahisi watu kujua umri wake wakati akiwa hai, Sasa wamefanikiwa kujua umri wake baada ya kuandikwa tarehe ya kuzaliwa kwenye msalaba ndio mleta thread anataka kujua ilikuwaje akaendelea kutumikia ofisi wakati ilibidi astaafu Miaka nane iliyopita? Hatuwezi jua lamda kunasheria ilimpa uwezo wa kuendelea, au raisi alikuwa na mamlaka ya kubadilisha kustaafu kwake au chochote kile ilimradi kiwe na mantiki ili watu kujifunza yaliyojificha kwenye Sheria za watumishi wa uma.
 
Serikal iliwah kupitisha ruhusa kwa kada flan kuendelea kufanya kwa maana ktk serikal baada ya ule umri wa kustaafu kufika ..nafikir pia ilikuwa kwa wanazuoni Dkts,profs ..nafikir na exceptional professionals .....correct me if i am wrong
 
Info yako ina walakin.
Mfugale kazaliwa 1953 December.
Jipange sasa uulize upya upate info sahihi.
 
Kwa ufupi marehemu mwendazake alikuwa mpumbavuuuu!! Alikuwa haangalii kabisa sheria zinasemaje maana yeye aliamini ndiye sheria mama!
 
Usichanganye mada,katiba inasema Urais ni vipindi viwili nyie mkataka atawale milele,kwenye utumishi wa umma sheria ya kazi(sio katiba) ni miaka 60 unless kuna sababu za msingi ndio unapewa mkataba miaka miwili miwili
Sababu ya msingi ni mtu kuwa na uwezo mkubwa wa kazi. Urais mtu anaongezewa baada ya katiba kurekebishwa
 
Anapoongezewa mkataba ulitaka wakupigie simu kukupa wewe taarifa?
 
Sikumwelewa Mwendazake kwenye moja ya hotuba zake za mwisho akiwa kwenye uzinduzi wa daraja la Kijazi kama sijakosea, alisema "...namwomba Mungu asimchukue Mhehe huyu kabla hajamaliza kazi za ujenzi zinazoendelea nchini..."
 
Mambo ya dikteta magufuli hayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…