Paul Kagame Amteua Major Gen Alex Kagame Kuwa Chief of Staff wa Reserve Forces na Maj Gen Andrew Kagame kuwa Commander wa Div 1

Watakuwa ni ndugu tu
 
Wakati Samia anampa Mkwe wake, Bwana Mohamed Mchengerwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI mbona sikuona hizi nyuzi!? Au Kagame ndo mtu pekee ambaye ameonesha upendeleo!??
 
Power corrupts..Huyu jamaa ndo kwisha habari yake. Mtu lazima ucheze na nyakati - huyu jamaa angeishajistaafia kitambo sana - angekua kajipumzikia zake..anatengeneza maadui tu..atakuwa na mwisho mbaya sana..
Mwisho mbaya? Hiyo inabakia kama best wishes tu. Paul Biya yupo madarakani since 1981, ana mwisho mbaya upi? M7 katulia zake state house since 1986, mwisho mbaya upi? Na anafanya haya haya ya PK and of course PK ni kama anajifunza kwa M7. Mwisho mbaya is just dua la kuku, halimpati mwewe abadani
 
View attachment 3125654

Halafu kasema uteuzi unaanza mara moja. Huu sasa ni uchuro na dharau kwa Wanyarwanda wote
Mimi sioni tofauti kabisa hata hapa kwetu ni hivyohivyo ...
Mkwe ni waziri mtoto ni mbunge na watoto wengine ni washauri waandamizi wa rais tena bila uteuzi wowote..

Tofauti ya tanzania na nchi za congo, rwanda, burundi na uganda ni huku hakuna mtoto wa kiongozi anapelekwa jeshini ila wanapewa vyeo kwenye chama na kupewa teuzi ingawa bada ni la muda tu 10 years kwisha..
 
Na mimi nina mawazo kama yako. Nimemjibu kuwa Bongo ilishafanyika.
 
Heri hao siyo wanafiki.

Nchi ya Kusadikika mtoto pendwa hana cheo chochote lakini nyuma ya pazia ana vyeo vyote
 
Meritocracy; government or the holding of power by people selected according to merit.

Professor Mahbob anasema tatizo kubwa la nchi za dunia ya tatu,ni Kwenye nafasi Za uteuzi huwa wanateua watu kwa upendeleo wa kujuana,kirafiki au kindugu..

Akatoa Hadi formula ya wao Singapore kufanikiwa walitumia kanuni ambayo waliita MPH


M=Meritocracy
P=Plagiarism
H=Honest..

So hili kwa afrika sio geni..

Nasikia familia ya Mwinyi Ina rais bara na visiwani...
 
Ni Paul Kagame gani aliyetawala Rwanda toka 1981. Moja ya makosa yaliyofanywa na JF ni kuruhusu watoto kama nyie kuandika humu na matokeo yake ndio mnaandika huo utumbo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…