Paul Kagame: Nashangaa Afrika mashariki tunalima pamba na kuuza Nje ila tunaagiza nguo za mitumba kutoka nje

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
12,835
Reaction score
23,584
Baada ya Kifo cha John Magufuli Africa ya mashariki kiongozi imara na mwenye maono aliyebaki ni Paul Kagame Rais wa Rwanda.

Akihojiwa na mwandishi wa habari Mario Nawfal hivi karibuni kagame amesikitishwa na kitendo cha Afrika mashariki kuendelea kuingiza nguo zilizotumika maarufu kama mitumba kutoka nchi za nje wakati nchi hizo zinalima pamba na kuuza Nje.

Anasema walikaa kikao kama viongozi wa Afrika mashariki na wakakubaliana kusitisha biashara ya kuagiza nguo chakavu kutoka nje na kuanzisha pamoja na kuendeleza viwanda vya nguo katika ukanda wa mashariki ya afrika. Anasema marekani ilipopata habari hizo walitoa taarifa kwa nchi za afrika mashariki ni marufuku kuzuia uagizaji wa nguo chakavu kutoka marekani. Viongozi wetu baada ya kuelezwa hayo walinywea na kukubaliana na masharti ya Marekani.

Viongozi wetu wakishindwa kufanya maamuzi magumu tutaendelea kutawaliwa na mataifa haya yenye nguvu hata kufikia kutwezwa utu wetu kwa mambo ambayo tunayaweza sisi wenyewe.
 
Najaribu kufikiria, kama Marekani alipiga mkwara wa kuendelea kuingiza mitu.ba kwa nchi za Africa mashariki. Je ni kweli hakuna mbinu nyingine ya kufanya kukwepa hiki kikwazo. Mfano serikari za Africa mashariki wakiamua kuwapa watu binafsi mitaji na kuanzisha viwanda vya nguo, je still marekani atakuwa na nguvu ya kuzuia hizo projects the private sector ambao watakuwa ni wana Africa mashariki?
 
Nadhani wao ndio walio kosea hawatakiwi kupiga marufuku. Walitakiwa kujikita kwenye uzalishaji wa nguo mpya zenye ubora unaoweza kushindana na nguo za mitumba. Waziuze kwa bei rahisi watu wataacha kununua hiyo mitumba watanunua nguo walizo zalisha wao.
Kupiga marufuku ni kupingana na sera za biashara na soko huria.
 
Huyo mshamba wako alikuwa na maono gani, kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa Chato? Yule alikuwa mshamba katili, Na huyo lofa skeleton maono yake ni kuua wakongomani na kuwaibia madini yao? We kwl ni bwege
 
Marekani anatishia kuvunja baadhi ya mikataba ya kibiashara kama AGOA ikiwa afrika mashariki itazuia mitumba isiingie. Lakini cha kujiuliza sisi afrika tuna uhaba huo wa masoko kiasi kwamba tukubali kuwa dambo la kupokea nguo chakavu.? Binafsi naamini ni utashi wa viongozi wetu na kuamua kufanya maamuzi tu.
 
Huyu jamaa na kinchi chake kidogo kama piriton anataka kutupelekesha🤔
Ndugu usiwe na mawazo mgando. Mawazo hayapigwi rungu. Ukiona mtu anakushauri jambo zuri lichukue. Wewe unaona ni sawa Tanzania kuingiza mitumba wakati tunalima pamba ya kutosha na viwanda tuna uwezo wa kuzalisha nguo?
 
Huyo mshamba wako alikuwa na maono gani, kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa Chato? Yule alikuwa mshamba katili, Na huyo lofa skeleton maono yake ni kuua wakongomani na kuwaibia madini yao? We kwl ni bwege
Naheshimu mawazo Yako hata kama ni ya kipumbavu.
 
Ndugu usiwe na mawazo mgando. Mawazo hayapigwi rungu. Ukiona mtu anakushauri jambo zuri lichukue. Wewe unaona ni sawa Tanzania kuingiza mitumba wakati tunalima pamba ya kutosha na viwanda tuna uwezo wa kuzalisha nguo?
Kuna kipindi cha nyerere tulivaa nguo za viwandani ukifua inakuwa pekosi.Hata mitumba na zenyewe zilikuwa mpya kipindi fulani!
 
Biashara huria haiwezi kuwa huria kwa Kila kitu. Hivi sasa marekani anaongeza Kodi kwa bidhaa za nje ili kulinda soko la ndani na viwanda. Lakini pia tukumbuke siyo Kila biashara ni ya kufanya mbona sisi hatupeleki nguo zilizotumika marekani wakavae?
 
Kuna kipindi cha nyerere tulivaa nguo za viwandani ukifua inakuwa pekosi.Hata mitumba na zenyewe zilikuwa mpya kipindi fulani!
Wakati wa Nyerere na sasa ni tofauti. Hivi sasa Kuna viwanda vya kisasa vya kutengeneza nguo kubwa ni tuwe na malighafi ambayo ipo sasa uoga wa Nini?
 
Kwani hiyo mitumba mnapewa bure au mnanunua. Afrika mnataka kutumia sera za kijamaa badala ya kutumia sera za biashara huria bora wamewapiga marufuku. Mnaweza kusababisha matatizo sio wote wanaweza kununua nguo mpya.
 
Biashara huria haiwezi kuwa huria kwa Kila kitu. Hivi sasa marekani anaongeza Kodi kwa bidhaa za nje ili kulinda soko la ndani na viwanda. Lakini pia tukumbuke siyo Kila biashara ni ya kufanya mbona sisi hatupeleki nguo zilizotumika marekani wakavae?
Lakini hajapiga marufuku. Ametumia mbinu ya kuongeza kodi.
 
Na bado itafika sehemu watasema bonokeni tuwalenge mikundu yenu na tutabonoka kweli
 
Kwani hiyo mitumba mnapewa bure au mnanunua. Afrika mnataka kutumia sera za kijamaa badala ya kutumia sera za biashara huria bora wamewapiga marufuku. Mnaweza kusababisha matatizo sio wote wanaweza kununua nguo mpya.
Mbona kama unakuwa mzito kuelewa aise. Kuagiza substandard products maana yake ni kuagiza uchafu. Ndio nikakuuliza Kuna ulazima wowote wa sisi kuagiza nguo na pamba tunalima hapa hapa kwanini tusiwe na viwanda vyetu tukatengeneza nguo za kuvaa wenyewe na kuuza katika ukanda wa wetu kwa maana ya soko?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…