Uchaguzi 2020 Paul Makonda achukua fomu ya Ubunge Kigamboni, kupitia CCM

Uchaguzi 2020 Paul Makonda achukua fomu ya Ubunge Kigamboni, kupitia CCM

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,393
Reaction score
3,237
RC MAKONDA ACHUKUWA FOMU KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KIGAMBONI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo Julai 15 amechukuwa Fomu ya kuomba ridhaa ya Kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Kigamboni kupitia tiketi ya Chama cha mapinduzi CCM.

Jimbo hilo lilikuwa chini ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile




619C696F-887A-4D79-B31B-3E057F03FCF5.jpeg


Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amechukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kigamboni, kitendo hicho kinaweza kuibua upya madai yake ya kughushi vyeti vya elimu na nyaraka zingine.

Kuna tuhuma kuwa Paul Makonda alitumia vyeti vya Daud Albert Bashite. Siasa ni mchezo mchafu, inaweza kupelekea kuwekewa pingamizi kwenye Tume ya Uchaguzi au ushindi wake kuja kupingwa mahakamani.

Mwaka 1995 Ramadhan Ali Kihiyo alishinda ubunge jimbo la Temeke kwa tiketi ya CCM, baadae NCCR Mageuzi ilienda Mahakamani kupinga kuwa Kihiyo alitumia vyeti visivyo vyake kuwania ubunge. Wakati kesi ikiwa inaendelea Mahakama kuu Kihiyo alijiuzulu ubunge.
 
Bila kujiuzulu Ukuu wa Mkoa?

Kwa hiyo ni Mkuu wa Mkoa pekee nchi nzima aliechukua fomu akiwa na madaraka yake yote ya Ukuu wa mkoa.

Mnaweza kuhisi amekuja kwenye kampeni kumbe yupo kwenye ziara ya kikazi, halafu mkaonyesa vidole vyenu vya Peoples.

Na atapiga kampeni huku akiwa na Chuo chake cha Ukuu wa Mkoa kama Kawaida.

Halafu Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi yupo chini ya Mkuu wa Mkoa.

Kuna hatari Makonda akawa Mbunge, Mkuu wa Mkoa na Waziri kwa wati mmoja.

Chalamila, Ole Sabaya mnajisikiaje huko mliko?
 
Back
Top Bottom