Paul Makonda aipasua CCM, kigogo ndani ya chama atishia kujiuzulu

Kwahiyo makonda aliitiwa nini mahakamani kama hakuwa mshitakiwa
 
Nafurahi sana kuona usiye na maisha una chuki dhidi ya mwenye maisha na ni jambo la kawaida Kwa masikini kuchukia waliofanikiwa ,tafuta hela ,utaacha makasiriko 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂🤣Makonda at the wheel usiyempenda karudi
 
Hii ni kweli?
 
Tafuta Hela utaacha kuchukia waliofanikiwa bila sababu ,usiyempenda kaja Kula chuma hiko ,tusio na stress za maisha hatutukani hovyo hovyo🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Alifanya nini mkuu kustahili jela?
 
Makonda ataipasua CHADEMA. Ujio wa Makonda umefanya Mbowe na wahuni wenzake wafute mikutano yao ya unafiki. Mabeberu waliokuwa wanawapa pesa kupinga mkataba wa bandari wameacha baada ya mkataba kusainiwa. Mbowe na genge lake wamebaki kuhaya haya tu
Mwanaume ukimiliki shape kama mwanamke,huwezi kua n akili
 
Samia huyu sijui uwa anawaza nini.

Sisi wananchi tulio wengi tumemuheshimu sana Mama kwa uteuzi huu. Mama anaupiga mwingi sana. Makonda ni kiongozi mzuri sana, mbunifu, ana uthubutu, ni mchapakazi. Mtu wa kazi kazi. Kiufupi ni ‘hana mbambamba’, kama wasemavyo vijana wa leo.
 
Mnawapa umaarufu wajinga,
badala liongee siasa za maendeleo kuassure umeme,maji,elimu,AFYA,AJIRA linamuwaza Mbowe na upinzani!
Vijana duni namna hii ni anguko Kwa taifa.
 
Sisi wananchi tulio wengi tumemuheshimu sana Mama kwa uteuzi huu. Mama anaupiga mwingi sana. Makonda ni kiongozi mzuri sana, mbunifu, ana uthubutu, ni mchapakazi. Mtu wa kazi kazi. Kiufupi ni ‘hana mbambamba’, kama wasemavyo vijana wa leo.
We jimama unamimba mbona unajiita sisi badala ya Mimi? Uwenda unamahabati kivyako tusikuingilie lkn kama huyu ndiyo kijana Bora Tz Kwa nafasi hii basi majimama kamawewe mnatukoseaa saana.
Mf. Alipoachia mkoa alihojiwa akasema anachojutia kutofanya Dar ni kutowapima tezi dume nyumba Kwa nyumba!!!
Kwa akili Yako shida kubwa ya dar ni tezidume we jimama??
Muadabike acheni mambo yakiushuzi unaoweza kutaka kutoka hata ukweni!!!
 
Ya Makonda kurudi tena uongozini CCM sijayashangaa kabisa!
CCM haileweki kama wadada rusha roho!
Ila kwenye vichwa vya habari kuna taarifa inasema...
VIGOGO WANAVYOJILIMBIKIZIA UTAJIRI KWA UFISADI AMBAO HAUJAWAHI TOKEA NCHINI ndio imenistuwa...
 
Mimi nadhani hii imefanywa kwa makusudi ili kuwaumiza gang fulani linaloonekana kutaka kumzuwia Mwenyekiti kwenye kinyang’anyiro cha 2025 ! Hii ni calculated move sio bahati mbaya !!
HALI NDANI YA CCM siyo shwari baada ya Paul Makonda kuteuliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM katika kikao ambacho kilijaa masikitiko na lawama nyingi sana kwa nini na sababu zipi zinafanya apewe hiyo nafasi. Wajumbe wengi wa NEC wametafsiri kuwa ubabe ukitumika kumsimika kwenye nafasi hiyo na wakidai hana sifa za kuwa Mwenezi wa CCM kuna ambao walidiriki kusema bora angeridishwa Polepole au Shaka lakini siyo Makonda.

Chanzo chetu toka ndani ya kikao cha NEC zinasema wa kwanza kabisa kupinga uteuzi wa Makonda alikuwa ni waziri mkuu mstaafu Mzee Mizingo Pinda ambaye alisema " kijana huyu katukana wastaafu wote na kafanya kila aina ya makosa na uovu lakini leo anafaaje kuwa na cheo kikubwa kiasi hiki ndani ya chama" Pinda aliendelea kusema kama kuna ulazima sana wa kurudishwa kwenye serikali au kupewa madaraka basi atafutiwe cheo kingine lakini siyo kuwa mwenezi wa chama kwa sababu ana historia chafu na ya hovyo sana ndani ya chama na nje ya chama na kwa watanzania CCM haitaeleweka kuteua mtu mhalifu kiasi kile kuwa kiongozi tena wa nafasi ya mwenezi.

Hali ilikuwa mbaya zaidi pale wajumbe wengi walipoonekana kutoridhishwa na kuletwa jina la Makonda na wengine mpaka wakaonya kwa nini kunakuwa na mabadiliko ya nafasi ya Katibu Mwenezi wa chama mara tatu ndani ya miaka 2 tu? Kuna mjumbe alihoji kuwa "mwenyekiti ulituletea Shaka ulipoingia,baada ya muda ukamtoa ukamleta Mjema na sasa unamtoa unamleta Makonda shida ni nini"

Baada ya kuona majibizano ni makali sana na wajumbe hawataki kabisa jina la Mkonda tunataarifiwa kuwa Mwenyekiti akaamua kura ipigwe kwa majina mawili aliyopendekeza ambayo yalikuwa nai jina la CHALAMILA na MAKONDA na baada ya kupigwa kura Makonda akamzidi CHAKAMILA kwa kura moja na akawa mwenezi kama ulivyotangwazwa.

Baada ya kikao cha NEC tunaarifiwa Kinana na JK na kundi la vjana wao wanaojiita wamekulia kwenye chama walikubaliana kukutana Dar Es Salaam nyumbani kwa Kinana na kikao kilifanyanyika na moja ya mambo waliyoazimia ni kuwa MAKONDA PAUL hafai kuwa Mwenezi wa CCM na watahakikisha kazi yake inakuwa ngumu sana na wameshaanza chini kwa chini kupeleka sumu mikoani na wilayani kuwashawishi wana CCM kutompa ushirikiano atakapoanza kuzunguka mikoani na mawilayani kwa ajili ya kukitangaza chama.

Suala la pili ni kuwa wamempa jukumu Chenge kuhakikisha kanda ya ziwa CCM inakataliwa kwa kiasi kikubwa na dalili zianze kuonekana kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 ili mwaka 2025 kwa pamoja wamtake mwenyekiti wao apishe mtu mwingine asimame kwenye urais kwa kuwa chama kimemkataa na kimepasuka kwa sababu ya maamuzi yake.

Kinana kapewa jukumu la kujiuzulu umakamu uenyekiti kabla ya mwezi December 2023 na aweke wazi kuwa hakubaliani na mwenyekiti kwenye maamuzi mengi na hasa ya kumteua Makonda kuwa Katibu Mwenezi na kuwa hakumshirikisha na hivyo bora akae pembeni kulinda heshima yake na heshima ya chama.

Kwa hiyo muda wowote kuanzia sasa Kinana ataomba kujiuzulu umakamu mwenyekiti wa chama na kukaa pembeni sasa kuratibu mipango ya kumuondoa Rais 2025 akishirikiana na akina Chenge na JK na January Makamba yeye kapewa jukumu la kukusanya fedha za kukamilisha mipango hiyo na anashirikiana na Luhanga Mpina sasa kuoroshesha na kuzunguka majimbo yote ya kanda ya Ziwa ambayo CCM ni lazima ishindwe ili kuwe na sababu ya kumtaka mwenyekiti wao asiwe mgombea 2025 na kwa kifupi wanajipanga kufanya mapinduzi na hawataki Rais Samia awe mgombea 2025.

Sasa wenye kusikia wasikie na wenye kukaa kimya wakae kimya lakini HABARI NDIYO HIYO..

#KigogoMedia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…