Paul Makonda amtaka Waziri wa Ujenzi kuharakisha ujenzi wa njia nne za barabara Mwanza yenye urefu wa km 32

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2019
Posts
1,521
Reaction score
4,381
MWENEZI MAKONDA ABAINISHA KUWA SERIKALI YA CCM CHINI YA RAIS SAMIA YAIELEKEZA WIZARA YA UJENZI KUJENGA BARABARA ZA NJIA NNE - MWANZA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Paul Makonda ameendelea na ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa ambapo leo tarehe 12 Novemba, 2023 amefika katika Mkoa wa Mwanza.

Akiwa Jijini Mwanza, Mwenezi Makonda amezungumza na Wananchi na kuwajuza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na Chama Cha Mapinduzi na kuongozwa na Mwenyekiti wa Chama hiko ambaye ni Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshatoa maelekezo kwa Wizara ya Ujenzk kuhakikisha inafanya usanifu wa kina wa barabara za Mwanza Mjini hadi Usagara na Barabad ya Mwanza Mjini hadi Igoma ili zipewe kipaumbele katika mpango wa Bajeti ya Mwaka wa fedha wa 2024/25 kwa ajili ya kujengwa kwa njia nne.

Mwenezi Makonda amebainisha hayo mara baada ya kumtaka Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa kuwaeleza Wananchi juu ya mkakati wa Serikali kuhusiana na barabara hizo.

“Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mpenda maendeleo haswa ba amekuwa akiendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali, niwaambie tu Wana Mwanza kuwa tayari amenielekeza kufanya haraka sana usanifu wa kina wa barabara mbili, barabara ya Mwanza Mjini Kwenda Usagara yenye urefu wa Kilometa 22 na Mwanza Mjini kuelekea Igoma ili ziwekwe kwenye vipaumbele vya bajeti ya 2024/25 ili ziweze kujengwa kwa njia nne,” alisema Waziri Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia, inatambua vema umuhimu wa daraja la JP. Magufuli katika kuunganisha ushoroba wa Ziwa Viktoria unaoanzia Sirari mpakani mwa nchi ya Tanzania na Kenya hadi Mutukula Mpakani mwa Tanzania na Uganda, barabara hiyo itapanuliwa na kuwa na njia nne ili kupunguza msongamano wa magari.

Mwenezi Makonda ameisisitizia Serikali haswa upande wa watumishi kuhakikisha wanafanya kazi kwa uzalendo na kwa kutambua Serikali inayotakana na CCM imepwa imani kubwa na Watanzania hivyo ni lazima kutekeleza ilani yake ya uchaguzi ya 2020/25 kwa vitendo.

#CCMKazini
#VitendoVinaSauti
#KaziIendelee

 

Attachments

  • 1699857399547.jpg
    102.7 KB · Views: 5
  • 1699857387333.jpg
    98.3 KB · Views: 4
Lakini hili ndio kipaombele Cha watu au mnataka miradi ya kupigia picha?

Binafsi Huwa naona kujenga Jenga ni kitu rahisi kuliko ku address real issues zinazowafanya watu kuwa maskini.

Tufikirie Nje ya kujenga,hayo ni matumizi madogo ya akili
 
Hizi fedha tungejenga barabara ya igoma kishiri fumagila kwa lami, tungejenga mahina buhongwa kwa lami, tungejenga kayenze kongolo kisesa tayari foleni ingeisha, sasa hivi mtu anaekwenda igoma kutokea buhongwa inamlazimu kuja mjini badala ya kupitia mahina au fumagila
 
Kweli Makonda babalao
 
HHi
Hii Barabara ya Buhongwa - Igoma kupitia Sahwa/Kishiri, ilisemekana itaanza kujengwa mwezi wa kumi mwanzoni, mbona sasa haisemwi?
 
Barabara njia nne ninaafiki. Wacha tuone utekelezaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…