Paul Makonda awataje hadharani Watu Wanaomroga Rais ili asije akafanya Maamuzi Makubwa kwa Kulogwa na hao watu

Paul Makonda awataje hadharani Watu Wanaomroga Rais ili asije akafanya Maamuzi Makubwa kwa Kulogwa na hao watu

Huyu Mwamba anakubalika ,kupendwa,kuaminika na kibali mbele za watu alichopewa na Mungu Mwenyewe.
Bandiko zima limejaa:

mahaba

hali ya kuingiwa moyoni na mtu au kitu na kukithamini zaidi ya vingine

Ni maandamano yaliyogusa hisia za mamilioni ya watu ambao wameonyesha kuguswa sana
Kisha likabebwa zaidi na:

propaganda

habari zilizotiwa chumvi sana au za uongo zitolewazo kwa lengo la kushawishi watu kuamini au kukubali jambo fulani

Ni maandamano ambayo yamewahusisha viongozi mbalimbali wa dini kutoka madhehebu mbalimbali
Huyu mwandishi alikuwa ndani ya Vatican,kwa siri alizoziona ndani, akatoa kitabu kilichouza sana na kupata umaarufu mkubwa!

Alitoa nukuu zifuatazo kuhusu watu aina ya Makonda na wakuu wa dini:

"The most dangerous of men are those who appear very religious".Dr. Rivera

"They have the deep respect of the people who are ignorant of their ungodly push for power behind the scenes"
.Dr. Rivera

"These religious men, who pretend to love God, will resort to murder, incite revolution and wars if necessary to help their cause". Dr. Rivera

"They are crafty,intelligent, smooth religious politicians who live in a shadowy world of secrets, intrigue, and phony holiness".Dr. Rivera

Tusome hiki kitabu kisha tumpime bwana Makonda na watu wa dini!
 

Attachments

Aiseeee you can't believe you're eyes unless you add another two eyes , yaani mtu anaamini imani za dark ages , according to history of Europe those days people believed witchcraft at the maximum ( 15th century) mtu analeta Tena imani hizo hadharani karne ya 21 .
 
Ina maana Ikulu hapakaliki kuna hirizi au nini? Wana sayansi mtuambie kama ulozi unapimika kwa kutumia nini?
 
Aiseeee you can't believe you're eyes unless you add another two eyes , yaani mtu anaamini imani za dark ages , according to history of Europe those days people believed witchcraft at the maximum ( 15th century) mtu analeta Tena imani hizo hadharani karne ya 21 .
Uchawi upo na utaendelea kuwepo na umekuwepo kwa miaka mingi sana iliyopita.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Leo Tanzania na Dunia nzima imeshuhudia maandamano na matembezi makubwa sana ya amani kuwahi kushuhudiwa kanda ya kaskazini yakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mwamba Mwenyewe Paul christian Makonda kijana Jasiri kuwahi kutokea katika ukanda wa kusini Mwa jangwa la Sahara.

Ni maandamano ambayo yamewahusisha viongozi mbalimbali wa dini kutoka madhehebu mbalimbali hapa Nchini. ni maandamano yaliyokuwa na lengo ya kuliombea jiji na mkoa mzima wa Arusha.ni maandamano Makubwa yaliyotikisa ukanda wote wa Afrika mashariki na habari zake kusambaa katika vyombo mbalimbali ndani na nje ya Nchi.

Ni maandamano yaliyogusa hisia za mamilioni ya watu ambao wameonyesha kuguswa sana na ubunifu wa kiongozi huyo kijana na mwenye Kalama ya uongozi na ambaye amekuwa akitabiliwa makubwa kwa siku za usoni.

Ni maandamano ambayo yameonyesha namna Mwamba Mwenyewe Paul Makonda alivyo na ushawishi mkubwa hapa Nchini kumpita kijana yeyote yule wa umri na rika lake kwa hakika unaweza kumchukia na kuwa na chuki na Mwamba huyu lakini ni ngumu kukataa na kupinga ukweli kuwa huyu Mwamba anapendwa na kukubalika na watu kupita maelezo.

Huyu Mwamba anakubalika ,kupendwa,kuaminika na kibali mbele za watu alichopewa na Mungu Mwenyewe ni kijana ambaye ukimchukia ndio ni kama unamuongezea hatua katika mioyo ya mamilioni ya watanzania.anapendwa mpaka Dunia inashangaa huyu siyo mtu wa kawaida na kuna kitu Mungu amekusudia kuja kumpa kijana huyu juu ya ardhi ya Tanzania ili aweze kutimiza kijana huyu ambaye hawezi kutamka sentesi tano bila kumtaja Mungu na ukuu wake.

Amepigwa kila aina ya mishale na kila aina ya fitina na kila aina ya Majungu lakini amebakia kuwa imara kuliko jana na juzi na wakati wowote ule ni kijana jasiri ,imara,madhubuti,shupavu mpaka maadui zake wanamhaha na kuogopa hata kusikia Sauti yake ikiunguruma kama Simba.

Sasa leo Mwamba amesema kuna watu Wanaomroga RAIS wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan shujaa wa Afrika. Ambapo kwa ujasiri kabisa ametamka maneno hayo hadharani maneno ambayo yametikisa na kuleta mijadala mitaani kote.

Sasa nilikuwa naona kama ingewezekana awataje watu hao hadharani ili waweze kujulikana kwa watanzania. Maana wakati mwingine mchawi anakosa nguvu ukimwambia na kumuweka wazi na peupe.

Maana hawa wachawi wanaweza kuungana na kumroga Rais wetu mpaka kuathiri hadi katika maamuzi afanyayo RAIS .ikumbukwe ya kuwa uchawi upo na umetajwa hadi katika biblia.

Hawa wachawi wanaweza kumroga Rais wetu hadi akajikuta anateua watu ambao hawana sifa kabisa ya kupewa uteuzi au akatengua wengine ambao wana sifa na uchapakazi uliotukuka AU kufanya maamuzi makubwa yenye athari kwa Taifa letu kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo.

Kwa hiyo ni muhimu hawa wachawi watajwe kabisa ili wajulikane kabisa ni maadui wa Taifa letu maana kama ambavyo baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere alivyosema katika kitabu chake cha uongozi wetu na hatima ya Tanzania kuwa ukimtikisa Rais unakuwa umetikisa hadi Nchi.

Mwamba Makonda najua ni jasiri na ndio maana sote tuliona namna alivyowataja majina wale wote waliokuwa wanajihusisha na masuala ya madawa ya kulevya.

Japo ushahidi haukupatikana kwa baadhi ya watu kwa kuwa kesi zilikuwa hazijaenda mahakamani na hivyo wengine kudai kuwa walikuwa wanachafuliwa na kukomolewa na wengine kudai kuwa alikuwa anapewa kibuli cha kuwakomoa baadhi ya watu na aliyekuwa Rais wetu wa awamu ya Tano Mheshimiwa Hayati Daktari Mwalimu John Pombe Joseph Magufuli.

Kutowataja watu hao Wanaomroga RAIS inaweza leta taharuki na kuanza kutajwa kwa majina ya watu hovyo hovyo au kuanza kuchafuana kwa baadhi ya watu.

Ngoja niweke kalamu yangu chini mara moja.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Duu yaani nyie mnaamini katika ulozi SIHIRI??🤣😀🤣😀
 
Acheni ushirikina nyie
Inaonekana na wewe una chale mpaka kwenye unyayo
Mimi namuamini Mungu sana na huu ujinga wa uchawi wenu hauwezi kumpatq Rais
Acheni ujinga huu hauwasaidii
Eti jicho la tatu lipi hilo
Siamini upumbavu wa mambo ya kichawi hata siku moja
Wewe uko upande gani
Huyo naye ni mshirikina tu kama alivyo Makonda. Ukoo wa Mwashambwa ni maarufu kwa mambo ya ndumba na uchunaji ngozi huko pande za Nyanda za juu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Leo Tanzania na Dunia nzima imeshuhudia maandamano na matembezi makubwa sana ya amani kuwahi kushuhudiwa kanda ya kaskazini yakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mwamba Mwenyewe Paul christian Makonda kijana Jasiri kuwahi kutokea katika ukanda wa kusini Mwa jangwa la Sahara.

Ni maandamano ambayo yamewahusisha viongozi mbalimbali wa dini kutoka madhehebu mbalimbali hapa Nchini. ni maandamano yaliyokuwa na lengo ya kuliombea jiji na mkoa mzima wa Arusha.ni maandamano Makubwa yaliyotikisa ukanda wote wa Afrika mashariki na habari zake kusambaa katika vyombo mbalimbali ndani na nje ya Nchi.

Ni maandamano yaliyogusa hisia za mamilioni ya watu ambao wameonyesha kuguswa sana na ubunifu wa kiongozi huyo kijana na mwenye Kalama ya uongozi na ambaye amekuwa akitabiliwa makubwa kwa siku za usoni.

Ni maandamano ambayo yameonyesha namna Mwamba Mwenyewe Paul Makonda alivyo na ushawishi mkubwa hapa Nchini kumpita kijana yeyote yule wa umri na rika lake kwa hakika unaweza kumchukia na kuwa na chuki na Mwamba huyu lakini ni ngumu kukataa na kupinga ukweli kuwa huyu Mwamba anapendwa na kukubalika na watu kupita maelezo.

Huyu Mwamba anakubalika ,kupendwa,kuaminika na kibali mbele za watu alichopewa na Mungu Mwenyewe ni kijana ambaye ukimchukia ndio ni kama unamuongezea hatua katika mioyo ya mamilioni ya watanzania.anapendwa mpaka Dunia inashangaa huyu siyo mtu wa kawaida na kuna kitu Mungu amekusudia kuja kumpa kijana huyu juu ya ardhi ya Tanzania ili aweze kutimiza kijana huyu ambaye hawezi kutamka sentesi tano bila kumtaja Mungu na ukuu wake.

Amepigwa kila aina ya mishale na kila aina ya fitina na kila aina ya Majungu lakini amebakia kuwa imara kuliko jana na juzi na wakati wowote ule ni kijana jasiri ,imara,madhubuti,shupavu mpaka maadui zake wanamhaha na kuogopa hata kusikia Sauti yake ikiunguruma kama Simba.

Sasa leo Mwamba amesema kuna watu Wanaomroga RAIS wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan shujaa wa Afrika. Ambapo kwa ujasiri kabisa ametamka maneno hayo hadharani maneno ambayo yametikisa na kuleta mijadala mitaani kote.

Sasa nilikuwa naona kama ingewezekana awataje watu hao hadharani ili waweze kujulikana kwa watanzania. Maana wakati mwingine mchawi anakosa nguvu ukimwambia na kumuweka wazi na peupe.

Maana hawa wachawi wanaweza kuungana na kumroga Rais wetu mpaka kuathiri hadi katika maamuzi afanyayo RAIS .ikumbukwe ya kuwa uchawi upo na umetajwa hadi katika biblia.

Hawa wachawi wanaweza kumroga Rais wetu hadi akajikuta anateua watu ambao hawana sifa kabisa ya kupewa uteuzi au akatengua wengine ambao wana sifa na uchapakazi uliotukuka AU kufanya maamuzi makubwa yenye athari kwa Taifa letu kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo.

Kwa hiyo ni muhimu hawa wachawi watajwe kabisa ili wajulikane kabisa ni maadui wa Taifa letu maana kama ambavyo baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere alivyosema katika kitabu chake cha uongozi wetu na hatima ya Tanzania kuwa ukimtikisa Rais unakuwa umetikisa hadi Nchi.

Mwamba Makonda najua ni jasiri na ndio maana sote tuliona namna alivyowataja majina wale wote waliokuwa wanajihusisha na masuala ya madawa ya kulevya.

Japo ushahidi haukupatikana kwa baadhi ya watu kwa kuwa kesi zilikuwa hazijaenda mahakamani na hivyo wengine kudai kuwa walikuwa wanachafuliwa na kukomolewa na wengine kudai kuwa alikuwa anapewa kibuli cha kuwakomoa baadhi ya watu na aliyekuwa Rais wetu wa awamu ya Tano Mheshimiwa Hayati Daktari Mwalimu John Pombe Joseph Magufuli.

Kutowataja watu hao Wanaomroga RAIS inaweza leta taharuki na kuanza kutajwa kwa majina ya watu hovyo hovyo au kuanza kuchafuana kwa baadhi ya watu.

Ngoja niweke kalamu yangu chini mara moja.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kati ya hao walozi Lucas Mwashambwa yumo na mauchawi ya Mbeya.
 
Kitu sijaelewa unatoa wazo au unapiga kampeni!! Hiyo kauli ya mwisho ya nani sijui muhura wa pili, ww umekua nani kutuamlia nani tumpe 2025??
 
Ni hatari sasa kama Taifa linaongozwa na mtu aliyerogwa!
Kama Paulo hampigi vijembe Mama aje atweleze ni nani hao wanaomloga Kiongozi wetu wa nchi!
 
Back
Top Bottom