ALIYEKUWA Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam nchini Tanzania, Paul Christian Makonda, sasa ameamriwa kufika mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kinondoni, Dar es Salaam, tarehe 3 Februari 2022, kujibu mashitaka ya jinai yanayomkabili.l
Taarifa kutoka Mahakama hapo na ambazo zimethibitishwa na mwandishi wa habari mwandamizi, Saed Kubenea, ambaye ndiye aliyefungua shauri hilo zinasema, tayari mhimili huo umetamtaka Makonda kufika siku hiyo.
Katika kesi hiyo ambayo imevuta hisia za wengi na kuibua mjadala mzito kila kona ya nchi hususani katika mitandao ya kijamii, Kubenea anamtuhumu Makonda kwa makosa mbalimbali.