Paul Makonda kufikishwa Mahakamani Februari 3, 2022 katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka

Paul Makonda kufikishwa Mahakamani Februari 3, 2022 katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka

ALIYEKUWA Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam nchini Tanzania, Paul Christian Makonda, sasa ameamriwa kufika mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kinondoni, Dar es Salaam, tarehe 3 Februari 2022, kujibu mashitaka ya jinai yanayomkabili.l

Taarifa kutoka Mahakama hapo na ambazo zimethibitishwa na mwandishi wa habari mwandamizi, Saed Kubenea, ambaye ndiye aliyefungua shauri hilo zinasema, tayari mhimili huo umetamtaka Makonda kufika siku hiyo.

Katika kesi hiyo ambayo imevuta hisia za wengi na kuibua mjadala mzito kila kona ya nchi hususani katika mitandao ya kijamii, Kubenea anamtuhumu Makonda kwa makosa mbalimbali.
“Wizara ina taarifa za uhakika kuwa Makonda amehusika katika uvunjifu huo wa haki kupitia nafasi yake kama Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Katika nafasi yake hiyo, pia amelaumiwa kwa kukandamiza upinzani wa kisiasa, kukandamiza haki ya kujieleza, na kushambulia makundi yasiyo na sauti,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
 
Hivi jinai mshtakiwa anaombwa kufika mahakamani tarehe tajwa au anatakiwa atokee mahabusu ndani ya karandinga? Sijaelewa.
Summons (samansi) imeshatoka akikaidi anakamatwa.. Lakini hata hiyo siku akienda anaweza asirudi uraiani
 
We jamaa una kichwa kizito sana. Ulikua unajua uhusiano wa Makonda na Clouds before hizo Propaganda za uvamiz?Nape kama Waziri ana mamlaka gani ya kuunda tume ya kumchunguza RC?RC anawajibika kwa Rais, Waziri ni mamlaka ya uteuzi ya RC?Usinchukulie makonda kama makonda, mchukulie Makonda kama RC.Waziri hana mamlaka ya kunchunguza RC hili weka KICHWANI.
Waziri ni sehemu ya serikali anao uwezo wa kuunda tume kuhusu wizara yake na si kuhusu mtu
 
Summons (samansi) imeshatoka akikaidi anakamatwa.. Lakini hata hiyo siku akienda anaweza asirudi uraiani
... wamempedelea kweli; hadi nafasi ya kuaga na kuweka baadhi ya mambo yake sawa wamempa; akabidhi kabisa na mke kwa rafiki yake anayemwamini ili amsaidie kumtunza. Bwire akiwa hana hili wala lile ndani ya daladala gari iliingizwa Kituo cha Polisi pale Chang'ombe akabebwa na hakuwahi kurudi nyumbani hadi leo. Makonda amepewa kabisa muda!
 
Tukio lilikua wazi Makonda (RC)Akiwa na walinzi wake walienda Clouds usiku. Unataka uchunguzi wa nani kafanya tukio kivipi tena?Hoja yako ingekua na LOGIC kama makonda angekuwepo sehemu ya wafanya uchunguzi. Kinyume cha hapo ni kwamba Makonda na walinzi wake walikua wanachunguzwa, Sio kitu kibaya kuchunguzwa lkn je WAZIRI ana mamlaka ya kuunda tume ya kuchunguza tukio ambalo RC yumo ndani yake?
Twambie sasa kuwa mjibu wa sheria na kanuni nani alipaswa kuunda tume ikiwa tukio limefanywa katika sekta ikiyo chini ya wizara ya habari?
 
... wamempedelea kweli; hadi nafasi ya kuaga na kuweka baadhi ya mambo yake sawa wamempa; akabidhi kabisa na mke kwa rafiki yake anayemwamini ili amsaidie kumtunza. Bwire akiwa hana hili wala lile ndani ya daladala gari iliingizwa Kituo cha Polisi pale Chang'ombe akabebwa na hakuwahi kurudi nyumbani hadi leo. Makonda amepewa kabisa muda!
Labda kwakuwa imefunguliwa na mtu binafsi kwenye kifungu cha mengineyo.. Lakini mpaka mahakama kuu kutoa kibali cha kuendelea na kesi basi imethiibitisha pasipo na shaka kuna kesi ya kujibu..
 
mahakama inaweza kusajili kesi kama mlalamikaji hasa sifa?
Ndio swali langu lilipo pia hizi mahakama zinaanza kuwa za ovyo, raia anawezaje kufungua criminal case wakati hizo ni case za jamuhuri pekee.


For what is worth ☝️tofauti ya plaintiff na prosecutor.

Ndio maana hakuna mtu humu anaweza cite a criminal case iliyofunguliwa na plaintiff sio Tanzania tu ata duniani.

Hizi siasa zinaaribu namna mihimili inavyotakiwa kufanya kazi, jinai ya kufunguliwa na raia only in Tanzania.

Kubenea awezi ata mfungulia civil case Makonda maana hana direct relation na Clouds Media sio shareholder wala mfanyakazi.
 
25236A6D-AB6B-47B5-B557-1EDDB54C57D2.jpeg


☝️Hiyo ni moja ya case inayochukua global headlines. Accusation za prince Andrew ni criminal offence in US.

It is very serious Buckingham Palace wamemvua Prince Andrew title zote za HRH na kumtaka asijiusishe na shughuli zozote including kujivua ukanali wake wa jeshi.

Lakini kwa sababu kesi imefunguliwa na plaintiff not a government prosecutor inasikilizwa kama civil case. Because only a government prosecutor can open a criminal case.

Hizi mahakama zetu zinaanza kuwa za kipuuzi raia anafungua jinai; the nonsense behind that is beyond me.

Upuuzi mwingine duniani unawezekana Tanzania tu.
 
MAKONDA RASMI MAHAKAMANI

Mahakama ya Kinondoni imemwandikia Paul Christian Makonda kufika mahakamani tarehe 3 February 2022 kujibu Miscellaneous Criminal Application Na. 1 ya mwaka 2022 na imepangwa kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi, Aron Lyamuya.

Makonda anashitakiwa kwa kuvamia kituo cha clouds tarehe 17 March 2017 saa nne usiku.

Siku ya tukio alifika akiendesha gari yake mwenyewe yenye usajili T 553 BFM akiwa na Askari wanne waliovaa sare za majeshi mbalimbali.

Lengo lilikuwa ni kushinikiza watangazaji warushe kwenye kipindi video ya mwanamke aliyefahamika kwa jina la GRACE ATHUMANI akifanya tendo la ndoa na Askofu Gwajima.

Muaandaaji wa video ile hakuwa anafahamika.

Makonda kuvamia Clouds, ni matumizi mabaya ya madaraka, chini ya kifungu cha 96 ya Kanuni ya adhabu (Penal Code), Sura ya 20 na kuingilia moja kwa moja, mawasiliano ya Kieletroniki.

Wengine anaoshitakiwa nao ni DPP na DCI kwa kushindwa kumchukulia hatua.

Vielelezo vitakavyotumika ni ripoti ya NAPE na katazo la @usembassytz la kumkataza Makonda na mkewe Marry Massenge kuingia Marekani kwa kunyima watu haki ya kuishi.

Imeandikwa na Fotunatus Buyobe kutoka mtandao wa Twitter.
 
Pia tunaomba ajibu haya

1. Nani alimuua Ben, Azory, Mawazo Lwajabe.

2. Nani alimteka, Roma, Nondo, Mo,

3. Waliookotwa kwenye viroba ufukweni walikuwa akina nani

Kumbukeni huyu ndiye aliyekuwa anatoa taarifa kuwa Fulani atapatikana siku Fulani.
Nani alimpiga risasi Tundu Lissu?
 
Kiongozi mkuu wa kikosi cha utekaji na mauaji akisaidiwa kwenye top list na Kinga, Jumane, Mahit na Badluck.
Kitu nashangaa kwanini hawa wauaji wote walichukuliwa kutoka Arusha? Mikoa mingine haina askari wenye roho mbaya?
 
Waziri ni sehemu ya serikali anao uwezo wa kuunda tume kuhusu wizara yake na si kuhusu mtu
Hiyo tume ilikua inachunguza tukio ambalo makonda ndio muhusika. Je kiutawala Waziri ana mamlaka hayo?
 
Ujinga huu.
unapoteza muda, fedha na akila zako kwa jambo la kijinga kama hili!!
mwishowe utabanwa umlipe gharama za kumsumbua.....halafu utaqnza kuchanhisha usaidiwe.
 
Katika video hiyo, ambayo haijulikani nani ameiandaa, mwanamke huyo alidaiwa kuonekana akifanya tendo la ndoa na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
Gwajima mwenyewe anasemaje kuhusu suala hili
 
Ukiangalia kwa jicho la kawaida unaweza fikiri kama Kubenea jasiri ila kwa wanao juwa this is deep state....

Na nia yao wala sio hii tunaiyona ila kumbukeni Sababu za USA kumuekea vikwazo bishite.... Tunasafari ndefu sana as nation....
The state ina deal na makonda Baada ya ku deal na baba yake Alie nyuma siyo!!!USA ban ya makonda the state ilihusikaje???how?na lengo ni kuharibu Mpango gani Hadi makonda apigwe US ban??
 
Back
Top Bottom